Ukarimu wangu umeniponza

Ukarimu wangu umeniponza

Basi umeshajua kinachoendelea sasa usiongee zaidi wala kumuuliza kitu juu ya uamuzi wake, kaa kimya fanya yako lea familia yako. Wasalimu kama kawaida

Ndio mambo ya lift hayo na kuzoeana kupiga mastori na wake za watu.
 
Bro, kimekuuma kuona jamaa kamkimbiza? Shukuru Mungu kamuondoa kimya kimya kuliko angeweka misumali njiani.
 
acronomy

Pole sana na umshukuru Mungu kwa kuepusha ambayo yangetokea japo wewe ilikua na nia njema, ikiwezekana kuwa busy na yako ili kupunguza ukaribu uliokwisha jengeka baina ya hizo familia zenu.
 
Last edited by a moderator:
Oa nawewe halafu mi niwe nampa nkeo lifti uone uchungu wake,nashangaa haya mambo umeyaleta huku huu ni umbeya,kipi kimekuuma,huu ni uamzi wangu binafsi

HAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHAHA....tena mfuate umuulize jiran vipi, umeamua kunianika JF,we mwanaume nichane live..
 
Eee mke wa mtu huyo, hata ningekuwa mimi aisee kwanza ni aibu kumwacha jirani ndio ampeleke mke kazini wakati nami nina gari, kama hakuna ubaya uliofanya we potezea tu.. jirani analinda mali yake.
 
Ukikutana na mke wake mwambie aache habari hizo..unaweza kuhisi yameisha baada ya huduma ya lifti kusitishwa kumbe wife kule akawa anaendelea kukumwagia misifa kwa mume wake..mwisho wa siku unakuja kufanyiwa kitu mbaya
 
Sasa bora umtafune huyo mkewe Ili tuhuma ziwe za kweli.........inauma sana kusingiziwa.............bora shari kamili kuliko shari nusu nusu kama hivyo...........
 
Wewe acronomy ni mtu wa ajabu sana jamaa kachukua maamuzi kuhusu familia yake wewe unakuja kulialia hapa.
 
Sasa bora umtafune huyo mkewe Ili tuhuma ziwe za kweli.........inauma sana kusingiziwa.............bora shari kamili kuliko shari nusu nusu kama hivyo...........

usimshauri hivyo. itamletea balaa kubwa zaidi ya hilo
 
Pole sana , ila kwa ushauri mzuri wa bure , nakushauri uhame hiyo nyumba kabisa ,, sio pahala pazuri tena kukaa hapo
 
Hahaaa…, bibie kakudondokea kiaina na kashindwa kuficha maana jina lako halikauki mdomoni mwake! Mwenye mke kaona isiwe tabu, heri nusu shari…!

Mkuu inaoekana we ni mkarimu kwa kuzaliwa!!
 
Back
Top Bottom