DOKEZO Ukarabati wa barabara ya Arusha - Moshi unatia walakini; uchunguzi ufanyike

DOKEZO Ukarabati wa barabara ya Arusha - Moshi unatia walakini; uchunguzi ufanyike

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Barabara ya Arusha - Moshi mwaka jana ilikuwa inafanyiwa ukarabati maeneo ya KIA, King'ori na Kikatiti.

Ukiangalia maeneo yaliyokarabatiwa sio yale yenye mashimo sana na kuna maeneo walikarabati kama mara tatu wanamaliza, barabara inapita then wanabomoa wanaanza tena ukarabati.

Inakuwa ni kero kubwa sana, maana maeneo ya ukarabati ni yale yale huku wanaacha ukarabati wa maeneo yanayonitaji ukatabati kweli kama lile eneo la kuingia Maji ya Chai lenye mashimo mengi na haliguswi hata kidogo.

Majuzi tena wameanza ukarabati wa eneo lililokuwa tayari limekamilika.

Nashindwa kuelewa, huwa Serikali haioni ni upotezaji wa kodi za wananchi kwa kipande kimoja kufanyiwa ukarabati zaidi yamara mbili?
 
Back
Top Bottom