Ukaccm vs ukawa

Ukaccm vs ukawa

Serikali mbili au tatu ni kipengele tu ndani ya Katiba Mpya, hakiwezi kuvuruga Mchakato, labda kama Wapinzani wao wanafikri Katiba mpya ni mjadala juu ya aina ya serikali.

hayo ni mawazo yako mgando ya kiCCM. juzi kikwete kaongea hoja ngapi bungeni? hukumsikia akiwatetea wazanzibar kwa kuvunja muungano baada ya kuunda nchi ya Zanzibar kutoka kwenye muungano wa awali?
 
Kinachoonekana kuendelea katika Bunge Maalumu la Katiba ni mashindano kati ya Umoja wa Katiba ya Wanachi (ukawa) dhiddi ya Umoja wa katiba ya CCM (ukaccm). Lakini tukizingatia kwamba katiba inayoandaliwa ni ya wananchi, utaona kwamba CCM wamepotoka na hawako na dhamira ya dhati katika kuandaa katiba ya Tanzania itakayosimamia maslahi ya wananchi wote bila ubaguzi. Wanachofanya wao (ccm) ni kupigania katiba ya CCM na mafisadi wachache wachumia tumbo na ambao kila siku wanatamani kuvuna na kutumia rasilimali za nchi kwa manufaa yao binafsi.

Endapo CCM wataendelea na msimamo wao wa kuwahonga baadhi ya wajumbe wa makundi mengine ili wakubaliane na matakwa yao, kuna hatari ya wajumbe wa upinzani na makundi mengine kujitoa wabakie CCM na wasaliti wachache wenye njaa wakaandae katiba yao kwa jinsi wanavyoona na wanavyotaka. Mungu aepushie mbali hili lisitokee kwani mpaka hapa tulipofikia mamilioni ya pesa za wananchi yameishatumika katika mchakato wa kuandaa katiba mpya tangu, kukusanya maoni ya wananchi, kugharimia mabaraza ya katiba na bunge hili linaloendelea sasa.

Mwelekeo mpya bungeni, Pinda atoa hoja kutuliza hali ya hewa - Kitaifa - mwananchi.co.tz

Swali la kujiuliza: Ikiwa CCM wanadhani kwamba kura ya siri nay a wazi zina nguvu sawa, ni kwa nini basi wang’ang’anie kura za wazi na kusababisha mvutano usiokuwa na kichwa wala miguu? Hawaoni kwamba wanapoteza muda wa wanachi na mwisho wa siku bunge litakuchukua zaidi ya siku 70 zilizopangwa na hatimaye kuiingiza nchi katika hasara ya kutumia pesa za ziada kuandaa katiba? Ni lini CCM wataanza kuheshimu maoni ya wananchi waliotoa maoni juu ya aina ya katiba wanayoitaka lakini sasa hivi CCM wanalazimisha kutaka kuichakachua katiba nzima kwa kufuta vifungu vyote na kuchomekea vya kwao na ambavyo vinawanufaisha wao na wachumia tumbo wachache?

Ngoja tusubiri tuone mwisho wa tamthilia hii lakini nina wasiwasi kama tutapata katiba ya wananchi kwani naona CCM wamedhamiria kwa dhati kutaka kupora katiba ya wananchi na kuigeuiza kuwa katiba ya CCM.
:target:
Umeandika vema, nimekuelewa.
 
Mashirika ya kimataifa hayana nafasi katika mstakabali wa Taifa letu.

mashirikaka gani unayoongelea ndugu yangu? na yamekuwaje na mustakabali wa nchi? nahishi elimu ya shule za kata itakuwa imekuathiri ubongo wako, sio bure!
 
Hv hawa wanaojiita ukawa wana hoja gani inayowaondolea ccm kuwa sehemu ya wananchi wa Jamhuli ya Muungano wa Tanzania? Kwanza hilo ni kosa na ni ubaguzi mkubwa sana, bunge la katiba lilihitaji zaidi ya wajumbe 600 na kupitia mchakato halali tulipendekeza uwakilishi kupitia vyama vya siasa , makundi maalum na Taasisi mbalimbali, Sasa iweje leo wazo la kundi fulani au msimamo uwe dhambi? na kwa utaratibu katika michakato hii ya kuandika katiba kuna kupiga kura kuunga mkono hoja fulani sasa hofu inatoka wapi? Ni uhuni tuu na nia mbaya kwa baadhi ya makundi fulani kutaka kuvuruga mchakato huu wa kupata katiba.

mkuu, CCM hawakatazwi kutoa maoni yao, kama ilivyo kwa makundi mengine. tatizo ni pale CCM wanapolazimisha mawazo yao ndiyo iwe katiba mpya. wanakuja na hoja ya serikali 2 ambayo haimo kwenye rasimu ili iweje? kwanini wasitoe maoni jinsi ya kuboresha serikali 3 badala ya kuzipinga? hoja ya serikali 2 haimo kwenye rasimu. kwa nn CCM wanataka kuichomeka kwenye rasimu?
 
Tatizo la CCM ni kupinga kila kitu kilichomo kwenye rasimu. Hayo yaliyomo kwenye rasimu ndiyo maoni ya wananchi. Sasa kama CCM wanayakataa kulikuwa na haja gani kuunda tume kutafuta maoni ya wananchi? Na kuna haja gani ya kuendelea na mchakato wa uundaji wa katiba? Tunapoteza muda na fedha za wananchi bure!
 
sasa iko wazi kwamba CCM wanataka kuvuruga mchakato kufuatia msimamo wa CCM uliotolewa na Rais Kikwete kipindi anazindua bunge la katiba siku ya tarehe 21-03.2014. maCCM hawana nia ya kuandaa katiba mpya. Nia waliyo nayo ni kutaka kuona kwamba mchakato wa utunzi wa katiba unakwama ili waendelee kutumia katiba mbovu iliyopo kwa ajili ya kujichotea na kutafuna mali za umma bila kunawa. cursed be CCM and their supporters!

UKAWA NAWAAMINI SANA WANALINDWA NA NGUVU YA UMMA WANASEMA NGOJA MJADALA UANZE ,HOJA ZA ------ NI DHAIFU SANA NA ZOTE ZINAJIBIKA KIRAHISI SANA HAZIWEZI KUSHINDANA NA ZA WARIOBA said (UKAWA TEAM)
 
Mimi bado naamini CCM ndiyo itakatupa Katiba zuri, wana nia ya dhati na Muugano wetu.

CCM inawanachama milioni tano tanzania nzima,na tanzania ina kadiliwa kuwa na idadi ya watu milioni 45 so toa milioni 5 ya CCM wanabaki milioni 40 so interest za watu milloni 4 haxiwezi kukandamiza hawa milioni 40
 
serikali tatu haziepukiki kuna mambo mengi hayakuingizwa kwenye rasimu hii kwa kuwa siyo mambo ya muungano na kwa kuwa rasimu hii ni ya serikali tatu

tume imeyaacha makusudi ili yaende kwenye katiba za nchi washirika wa shirikisho, mfano mambo kama aridhi, kodi, elimu maliasili madini,

ukilazimisha serikali mbili inabidi urudi tena ili kujumuisha mambo ya muungano na yasiyo ya muungano kwenye katiba moja,

hii haiwezi kuwa kazi ya bunge maalumu la katiba kisheria inagoma kabisa.

sijui kama CCM hilo wanaliona, maana yake ni kwamba tume irudi tena kwa wananchi mara ya pili, kitu ambacho ni kupoteza muda kwa kutafuta matokeo ambayo hayabdiliki
 
basi tuambie tatizo la muungano lipo kwa kiasi gani na utushawishi kwa hoja mpaka tukuelewe. na hiyo 80% uliyoipachika kwenye maelezo yako ni kitu gani na umeipataje? usikariri kila jambo kama kasuku.

Mkuu naona Hotuba maridadi ya JK imekupiga chenga! Hiyo 80% imeelezwa humo, sina haja ya kurudia rudia! Muungano una matatizo, lakini solution sio kuongezea tena tatizo kwa kuunda nchi mbili zijipachike ndani ya nchi moja! Tukifanya hivyo Historia itatuhukumu milele!!
 
Serikali mbili au tatu ni kipengele tu ndani ya Katiba Mpya, hakiwezi kuvuruga Mchakato, labda kama Wapinzani wao wanafikri Katiba mpya ni mjadala juu ya aina ya serikali.

UKAWA wanafikiri Katiba mpya ndio tiketi ya kwenda Ikulu!
 
Mkuu naona Hotuba maridadi ya JK imekupiga chenga! Hiyo 80% imeelezwa humo, sina haja ya kurudia rudia! Muungano una matatizo, lakini solution sio kuongezea tena tatizo kwa kuunda nchi mbili zijipachike ndani ya nchi moja! Tukifanya hivyo Historia itatuhukumu milele!!

mkuu, wananchi wanataka serikali 3. sasa serikali 2 unazongangania ni za nani? hicho kikundi kinachotaka serikali 2 waende wakaziingize kwenye katiba ya kikundi chao. katiba ya wananchi inayojadiliwa bungeni ni ya serikali 3.
 
Mkuu naona Hotuba maridadi ya JK imekupiga chenga! Hiyo 80% imeelezwa humo, sina haja ya kurudia rudia! Muungano una matatizo, lakini solution sio kuongezea tena tatizo kwa kuunda nchi mbili zijipachike ndani ya nchi moja! Tukifanya hivyo Historia itatuhukumu milele!!

Solution yake ni nini kumbe?
Z

Una hakika kwamba muungano huu sio wa nchi mbili ndani ya nchi moja? Kwani hujui kwamba Zanzibar ni nchi?
 
Tatizo hapa ni baadhi ya watu kutokufahama mantiki ya hoja zao. Kuna baadhi wanadhani hoja zao ndiyo za wananchi bila kufahamu kuwa CCM ni sehemu ya wananchi.

CCM, kama baraza la katiba, ilishatoa maoni yake tayari na yakaingizwa kwenye rasimu. Sasa wasubiri wajumbe wa bunge la katiba wayafanyie kazi. Kwanini wanataka kulazimisha mambo ambayo hayamo kwenye rasimu inayojadiliwa bungeni yaingie kwenye rasimu. Suala la serikali 2 halimo kwenye rasimu. Kwanini wanataka kuliingizamo kimabavu? Huoni kwamba wanatishia uhai wa bunge la katiba?
 
Na ni kwa nini pia wengine wang'ang'anie kura ya siri... na ule umoja unaitwa Tanzania Kwanza na si ukaccm hii ni yako... mwanauzi usiweke ushabiki weka hoja yenye mantiki na watu wachangie kwa hoja lakini si kutoa hoja elekezi kwa yale tu unayotaka wanauzi huu wajielekeze.
Asante!
 
Tujikite kuhamasisha watu waikatae hiyo katiba ya CCM itakapokuja kura ya maoni
 
Mbona mnaongea kama vile CCM sio sehemu ya wananchi na vilevile hawawakilishi wananchi? Kumbukeni kuwa zaidi ya 80% ya wananchi hawakuzungumzia Muungano wakati wa kukusanya maoni kwa kuwa hawakuona tatizo na Muundo wa Muungano! Sasa ya nini ku-create tatizo huku mkijua kuwa halipo kwa kiasi hicho?

Acheni unafiki serikali yenu ndiyo iliyoratibu suala zima la tume ya maoni mwanzo mwisho je hamkuona umuhimu wa kuchukua maoni ya hiyo 80% au yanakuwa na umuhimu kwenu kwa kuwa matakwa yenu hayajatimizwa? je ingekuwa hao mnaodai ni wachache wamependekeza serikali 2 mngetoka kusema 80% hawakusema juu ya muungano, hakika mwisho wenu umefika hamtashinda nguvu ya umma nyamazeni waacheni wananchi watengeneze katiba yao:tape:
 
Mkuu naona Hotuba maridadi ya JK imekupiga chenga! Hiyo 80% imeelezwa humo, sina haja ya kurudia rudia! Muungano una matatizo, lakini solution sio kuongezea tena tatizo kwa kuunda nchi mbili zijipachike ndani ya nchi moja! Tukifanya hivyo Historia itatuhukumu milele!!

Matatizo ambayo ccm imeshindwa kuyatatua ndani ya miaka 50 na yanazidi kuongezeka kila uchao wapisheni wananchi wafanye maamuzi magumu juu ya maslahi yao na vizazi vyao vijavyo sio kumfurahisha ------😛eace:
 
Back
Top Bottom