Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,914
Habari zenu ........
Natumai ni wazima kwa wale ambao ni wagonjwa poleni sana na nawaombeeni mpone haraka
Kuna jambo ambalo limekuwa linawasumbua sana wadad wengi ambao wako kwenye mahusiano a vijana,jambo hilo ni kuwa wadada wamekuwa wakiingia kwenye madhila makubwa kwenye mahusiano yao na kujikuta wakijilaumu sana na wengine kujutia mahusiano yao
Madhila ninayoyazungumzia hapa sio mengine bali ni ujauzito
Kuna binti mmoja alipewa ujauzito na kijana mmoja na mara binti huyo kujua hilo aliamua kumwambia kijana huyo,baada tu ya kumuambia tu mawasiliano na kijana yalianza kupungua na hatimae kwisha kabisa na binti akaachwa na ujauzito.Binti alijaribu kumtafuta kijana lakini hakufanikiwa kwani alikuwa akimkwepa mara kwa mara
Binti aliamua kuitoa mimba na bahati mbaya alipata matatizo sana kwa kuugua wiki 2 bila msaada wowote ule lakini bahati nzuri alipona
Matukio ya kutelekezwa wasichana huku wakiwa na ujauzito au kutelekezwa kwasababu ya kupata ujauzito ni mengi sana na yameharibu sana maisha ya mabinti wengi sana.Kipindi kile ambapo binti alipokuwa amepata ujauzito na shule kuishia hapo wengi sana walipata hasara na wazazi pia kwani mabinti wengi sana walifukuzwa shule
Napenda kuwaambia tu kuwa wale ambao wanasoma ni bora wakaacha kabisa kushiriki ngono maana hao mnaojidai mnawapenda ni kujidanganya tu,hakuna cha upendo wala nini na hao wapo kwasababu ya kuwaharibia maisha yenu tu.Kama kuna kijana anajidai anakupenda mwambie asubiri umalize masomo yako ndipo mengine yaendelee,kama hataki mkimbie kama vile umeona mnyama mkali sana
Nyie ambao either mna shughuli zenu au mko katika vyuo,hao wanaojidai wanawapenda kuweni nao makini sana.Usikubali kubeba ujauzito hivi hivi tu bila ya kuwa na ndoa.Anaweza kukuambia maneno mengi sana matamu kumbe hamaanishi hayo anayosema,jihadharini sana na hawa watu
Kama utaamua kuzaa basi hakikisha kuwa umejipangia kulea mwanao wewe mwenyewe bila ya msaada wa huyo jamaa,kama ukijifungua na akawa pamoja na wewe mshukuru Mungu na leeni mtoto,lakini nakushauri usizae kabla ya ndoa na kama utaamua kuzaa basi zaa kwasababu unajiweza,kumtegemea huyo anaejidai kuwa anakupenda imekula kwako dada yangu
Kuna wanaume wa ajabu sana kwenye hii dunia,soon tu anajua kuwa umepata ujauzito atakukimbia na kukuacha huna pa kwenda,kuwa makini sana wewe unaesoma hapa
Kama unataka uije kujuta baadae au kuja kulia mwenyewe bila ya msaada basi epuka sana haya kwani wengine wamejaribu hata kujiua kwa kunywa vidonge ili kuepuka hii kadhia
Jipende na yapende maisha yako,epuka kuja kujutia na kutamani kujiua kwasababu ya raha au mtu mwingine ambae alikulaghai tu.Kama utamuambia asubiri na akakataa au utamuambia mfunge ndoa kwanza na akakataa achana nae dada yangu maisha yako yana thamani kubwa sana kuliko huyo jamaa
Inaniuma sana kuona akina dada wakiteseka na kuharibiwa maisha na watu ambao nao wana maisha yao
Jumapili njema ..........!!
Natumai ni wazima kwa wale ambao ni wagonjwa poleni sana na nawaombeeni mpone haraka
Kuna jambo ambalo limekuwa linawasumbua sana wadad wengi ambao wako kwenye mahusiano a vijana,jambo hilo ni kuwa wadada wamekuwa wakiingia kwenye madhila makubwa kwenye mahusiano yao na kujikuta wakijilaumu sana na wengine kujutia mahusiano yao
Madhila ninayoyazungumzia hapa sio mengine bali ni ujauzito
Kuna binti mmoja alipewa ujauzito na kijana mmoja na mara binti huyo kujua hilo aliamua kumwambia kijana huyo,baada tu ya kumuambia tu mawasiliano na kijana yalianza kupungua na hatimae kwisha kabisa na binti akaachwa na ujauzito.Binti alijaribu kumtafuta kijana lakini hakufanikiwa kwani alikuwa akimkwepa mara kwa mara
Binti aliamua kuitoa mimba na bahati mbaya alipata matatizo sana kwa kuugua wiki 2 bila msaada wowote ule lakini bahati nzuri alipona
Matukio ya kutelekezwa wasichana huku wakiwa na ujauzito au kutelekezwa kwasababu ya kupata ujauzito ni mengi sana na yameharibu sana maisha ya mabinti wengi sana.Kipindi kile ambapo binti alipokuwa amepata ujauzito na shule kuishia hapo wengi sana walipata hasara na wazazi pia kwani mabinti wengi sana walifukuzwa shule
Napenda kuwaambia tu kuwa wale ambao wanasoma ni bora wakaacha kabisa kushiriki ngono maana hao mnaojidai mnawapenda ni kujidanganya tu,hakuna cha upendo wala nini na hao wapo kwasababu ya kuwaharibia maisha yenu tu.Kama kuna kijana anajidai anakupenda mwambie asubiri umalize masomo yako ndipo mengine yaendelee,kama hataki mkimbie kama vile umeona mnyama mkali sana
Nyie ambao either mna shughuli zenu au mko katika vyuo,hao wanaojidai wanawapenda kuweni nao makini sana.Usikubali kubeba ujauzito hivi hivi tu bila ya kuwa na ndoa.Anaweza kukuambia maneno mengi sana matamu kumbe hamaanishi hayo anayosema,jihadharini sana na hawa watu
Kama utaamua kuzaa basi hakikisha kuwa umejipangia kulea mwanao wewe mwenyewe bila ya msaada wa huyo jamaa,kama ukijifungua na akawa pamoja na wewe mshukuru Mungu na leeni mtoto,lakini nakushauri usizae kabla ya ndoa na kama utaamua kuzaa basi zaa kwasababu unajiweza,kumtegemea huyo anaejidai kuwa anakupenda imekula kwako dada yangu
Kuna wanaume wa ajabu sana kwenye hii dunia,soon tu anajua kuwa umepata ujauzito atakukimbia na kukuacha huna pa kwenda,kuwa makini sana wewe unaesoma hapa
Kama unataka uije kujuta baadae au kuja kulia mwenyewe bila ya msaada basi epuka sana haya kwani wengine wamejaribu hata kujiua kwa kunywa vidonge ili kuepuka hii kadhia
Jipende na yapende maisha yako,epuka kuja kujutia na kutamani kujiua kwasababu ya raha au mtu mwingine ambae alikulaghai tu.Kama utamuambia asubiri na akakataa au utamuambia mfunge ndoa kwanza na akakataa achana nae dada yangu maisha yako yana thamani kubwa sana kuliko huyo jamaa
Inaniuma sana kuona akina dada wakiteseka na kuharibiwa maisha na watu ambao nao wana maisha yao
Jumapili njema ..........!!