kamili nadhani hukuipata vema hoja ya
Shayu , napenda nichangie kidogo
Shayu anasema ukweli, Rais ni kiongozi wa wote hata waliopo magereza
Ni mlezi wa kila mmoja, si masikini , si tajiri si mfungwa n.k.
Kauli yake hayupo upande wa matajiri ni ya kibaguzi. Je, atasemaje kuhusu wafungwa?
Utajiri si kosa au dhambi. Hivi Bill Gate, Warren Buffet, Bakheresa au Dangote wana makosa gani kutumia bongo zao kupata utajiri! Ni nani asiyetaka utajiri dunia hii?
Matajiri ndio wanaoitwa wawekezaji, wawe wa nje au wa ndani.
Kuwatenga kwa lugha ni kuwatisha na hiyo haifai kwa mlezi wa Taifa
Tujiulize, matajiri wameajiri watu kiasi gani?
Na mchango wao kupitia kodi ni kiasi gani, au kupitia biashara zao ni kiasi gani?
Tusisahau moja ya sifa za matajiri ni uwezo wa kushawishi 'lobbying' kwa masilahi yao.
Kwa bahati mbaya viongozi wamegeuza hilo kuwa rushwa.
Ndio hao anaosema mkuu wanatoa pesa za kugharamia siasa.
Swali, wale wanaopokea wana maadili gani ya kufanya hivyo?
Hatari ya kauli ya Rais ni aliyosema Nyerere,dhambi ya ubaguzi haikomi inaendelea
Akimaliza matajiri atawatenga wapinzani.
Nako akimaliza atawatenga watu kwa kitu kingine. Fikiria itakapofika ktk ukabila au dini
As long as Tajiri anatimiza wajibu wake, hakuna sababu wala kosa la kuwatenga