Ujumbe kwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Makonda - Ongeza juhudi za kuifanya Dar iwe ya kijani na maua, mabati yenye kutu yapakwe rangi

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
NIngependa kutoa wito kwa Mkuu wa MKoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, aongeze bidii katika kuufanya mkoa wa Dar es Salaam uwe wa kijani zaidi kwa kufanya kampeni ya upandani miti na maua eneo la ndani ya jiji. NImeangalia kwa mfano, hili eneo la flyover Tazara na kuona kwamba linaweza kupendezeshwa hata zaidi. Sehemu nyingi duniani barabara inayokwenda airport huwa inapendezeshwa sana kwa miti ya maua.

Ningependa kumkumbusha Makonda kwamba kwa kuwa jiji la Dar es Salaam linazidi kujengwa mchana na usiku, jitihada hizi zifanywe kupanda miti pamoja na ile ya maua ili isije ikatokea jiji letu likageuzwa kuwa concrete city.

Na pia bwana Makonda, ikibidi basi amri na itolewe kwamba nyumba zote za Dar es Salaam ziezekwe kwa mabati ya rangi au yaliyopakwa rangi. Unapoingia Dar kwa ndege nyumba zinaonekana chafu sana, unachoona ni kutu tu ya mabati. Inatia aibu sana kwa sababu kwa wageni wengi hiyo inakuwa first impression ya Dar es Salaam, kwamba sisi ni wachafu hatu-fanyii nyumba maintanance. Na huenda mabati yenye kutu yana athari kiafya kwa maji yanayotiririka toka kwenye bati.

Kwa ujumla ningependa Raisi Magufuli ahimize jambo hili kwa wakuu wote wa mikoa na wilaya. Kuna miji ukienda inatia aibu kwa kuwa unachoona ukiwa mjini ni majengo tu hakuna miti ya kupendezesha mandhari. Majengo ni machafu hata rangi hayapakwi na wala hakuna miti wala maua.

1538033818036.png
 
Swala la miti nakuunga mkono kwa asilimia 100,tena ningependekeza iwe ya matunda na iwe na uangalizi,matunda yatasaidia hata wagonjwa wetu kupata vitamin.
Ile miti mifupi ya machungwa, maembe, parachichi,stafely, topetope. .
Nilikua na wazo la kuandika proposal nimpelekee mkuu wetu wa Mkoa. ...Ila kutokana na nature ya kazi yangu muda unabana sana.
Natumaini Mkuu mara moja moja anapata wasaa wa kupita huku,au wasaidizi wake watalifanyia kazi,na wakinihitaji kwa ushauri zaidi,mimi kama mzalendo nipo tayari kuitumikia Nchi yangu kwa garama yoyote.
Hilo la bati mkuu tunatofautiana vipato
 
hela za wananchi unadhani hazina kazi ya maana mpka tupoteze kwa sababu ya KUPAKA rangi bati??
Kupaka rangi nyumba unaona sio kazi ya maana? Hivi unajua kwamba sheria ya jiji inataka majengo yapakwe rangi kila wakati? Nadhani huna asili ya usafi wewe. Ndio mnaotupa maganda ya ndizi barabarani au takataka nje ya gari linalotembea
 
ww hujanishawishi
Kupaka rangi nyumba unaona sio kazi ya maana? Hivi unajua kwamba sheria ya jiji inataka majengo yapakwe rangi kila wakati? Nadhani huna asili ya usafi wewe. Ndio mnaotupa maganda ya ndizi barabarani au takataka nje ya gari linalotembea
 
Swala la miti nakuunga mkono kwa asilimia 100,.
Hilo la bati mkuu tunatofautiana vipato

Mkuu, kuna kanuni inayotumika katika serikali kwamba kama una gari basi unaweza kulipia kodi ya stika ya wiki ya uslama barabarani.

Sasa kama umeweza kujenga nyumba Dar es Salaam basi unaweza kumudu gharama ya kupaka bati rangi nyumba yako. Kwani ndoo moja ya rangi ya bati ni shilingi ngapi, sio 35,000/- kweli? Yaani tukikupa miezi sita uwe umepaka bati rangi utashindwa kweli?
 
ww hujanishawishi
Unajua bei ya ndoo moja ya rangi ya bati? Haizidi shs 40,000. Ni suala la kujinyima kiasi kitu fulani tu, kama bia kwa mwezi mmoja. Umeweza kuwa na nyumba ushindwe hela ya kupaka rangi bati?

Lakini kama ikibidi, basi hiyo hela iwekwe kwenye ada ya plot ili serikali "iwagawie rangi bure". Maana Watanzania bwana, concept ya kupewa bure tunaipenda sana.
 
Watu wanafkiria pakupata hela ya kula wewe unawazia mabati kupakwa rangi
Hii ni dalili tosha kwako kuonekana hauna Majukumu
naunga mkono hoja

Nyie bwana mnakuwa kama wale wanasiasa wanaokataa kuchangia fedha au nguvu kazi mambo ya maendeleo wakidai hilo ni jukumu la serikali. Hamfai kabisa katika nchi yetu hii.

Ngoja siku niteuliwe kuwa mpika chai ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar, mtapaka rangi hayo mabati kwa nguvu.
 
Mkuu, kuna kanuni inayotumika katika serikali kwamba kama una gari basi unaweza kulipia kodi ya stika ya wiki ya uslama barabarani.

Sasa kama umeweza kujenga nyumba Dar es Salaam basi unaweza kumudu gharama ya kupaka bati rangi nyumba yako. Kwani ndoo moja ya rangi ya bati ni shilingi ngapi, sio 35,000/- kweli? Yaani tukikupa miezi sita uwe umepaka bati rangi utashindwa kweli?
Utumbo mtupu
 
Wazo la kijinga hili umeleta
Lazima utakuwa una nyumba ina bati lenye kutu sana, hata kuwajengea wapangaji wako choo na bafu la maaana umekataa!

Halafu tatizo la watu kama nyie ni kwamba hamjasafiri. Sidhani hata hapa Moshi na Arusha mmefika, acha mbali nchi nyingine. Mmeganda katika mawazo ya kutoendelea kwa sababu mnaona maendeleo ni gharama sana. Mtu unajisifia una nyumba mlango wa choo na bafu ni gunia halijabadilishwa miaka mitatu. Mnatia kinyaa.
 
Huo ushauri wako kawape shangazi zako huko kijijini,Sisi hatudeal na rangi za mabati tunadeal na kusaka mlo
Mbona nilishakuelewa saa nyingi sana - watu mnaoishi ili mle

Hata hivyo ujumbe huu ni kwa ajili ya Makonda, sio nyie kula kulala

Amini nakuambia, kuna watu ambao watakaa pembeni ya kinyesi na hata kula chakula bila kuona tatizo. Anakuambia kwani kinyesi kinanizuia kumeza chakula. Sasa hao ndio watu kama wewe. Tunatofautiana sana. MIe nitaangalia Dar toka angani nione mlundikano wa mabati yenye kutu kama uchafu, wewe utaangalia Dar toka angani uone uone mlundikano wa mabati yenye kutu kuwa Dar imeendelea ina nyumba nyingi.
 
Back
Top Bottom