MWAKATA KWETU
JF-Expert Member
- Mar 25, 2015
- 560
- 320
Mji wa Kahama ni miongoni mwa miji inayokua kwa kasi Tanzania. Shughuli kuu ya kiuchumi ni biashara ya Mazao, maduka ya jumla na rejareja, uchimbaji wa madini, kilimo na ufugaji. Idadi ya watu inaongezeka kila siku.
Shughuli za kiserikali
Kuna baadhi ya taasisi mjini hapa zina hadhi sawa na Mikoa au Manispaa. Taasisi hizo ni Mamlaka ya Maji KUWASA, Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) na TAKUKURU.
Pia Mji wa Kahama umeingizwa katika orodha ya miji inayofadhiliwa na mfuko wa Benki Kuu ya Dunia kujenga miundombinu kwenye Manispaa na Majiji. Chanzo cha habari hii ni Kwizera FM ilipokuwa ikifanya mahojiano na Meya wa mji wa Kahama bwana Abery Shija.
Viwanda
Katika kuunga mkono juhudi za Rais katika sekta ya Viwanda, Kahama inakua katika sekta ya viwanda huku tukishuhudia ujenzi wa viwanda na ufunguzi.
Tumeshuhudia ufunguzi wa kiwanda cha Mabati, Nondo n.k. Pia kiwanda cha kutengeza bidhaa za plastiki na kiwanda cha kukamua Mafuta. Pia kuna ujenzi mwingine unaendelea wa kiwanda cha kutengeneza Mifuko.
Mawasiliano na Uchukuzi
Kahama ni kati ya miji nane Tanzania ambayo ina viwanja vya ndege. Hivyo ukiwa Kahama unaweza safiri kwa basi au ndege.
Sent using Jamii Forums mobile app
Shughuli za kiserikali
Kuna baadhi ya taasisi mjini hapa zina hadhi sawa na Mikoa au Manispaa. Taasisi hizo ni Mamlaka ya Maji KUWASA, Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) na TAKUKURU.
Pia Mji wa Kahama umeingizwa katika orodha ya miji inayofadhiliwa na mfuko wa Benki Kuu ya Dunia kujenga miundombinu kwenye Manispaa na Majiji. Chanzo cha habari hii ni Kwizera FM ilipokuwa ikifanya mahojiano na Meya wa mji wa Kahama bwana Abery Shija.
Viwanda
Katika kuunga mkono juhudi za Rais katika sekta ya Viwanda, Kahama inakua katika sekta ya viwanda huku tukishuhudia ujenzi wa viwanda na ufunguzi.
Tumeshuhudia ufunguzi wa kiwanda cha Mabati, Nondo n.k. Pia kiwanda cha kutengeza bidhaa za plastiki na kiwanda cha kukamua Mafuta. Pia kuna ujenzi mwingine unaendelea wa kiwanda cha kutengeneza Mifuko.
Mawasiliano na Uchukuzi
Kahama ni kati ya miji nane Tanzania ambayo ina viwanja vya ndege. Hivyo ukiwa Kahama unaweza safiri kwa basi au ndege.
Sent using Jamii Forums mobile app