Gsana
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 4,383
- 1,340
Nafurahi kusikia kuwa mh.waziri mkuu umekuja kuzindua miradi karatu,ila nakuomba usaidie aya : karatu kuna maji ila si masafi alaf sio kila sehemu ina maji,tunaomba utuhakikishie maji,tunachoka na maji machafu na maji ya kununua kwani matajiri wa hapa wanauza maji na serikali yako haijaleta juhudi za kutosha ktk maji. Pili,tunaomba kujua ni kwa nini hasa apa karatu hakuna mawimbi ya redio?ukienda mlimani unapata redio ila mjini hakuna eti kisa hakuna mitambo wakati hata porini biharamulo kuna network. Fikiria leo tar19 sept hakuna network ya airtel tangu kuche,ndo nini jamani? la mwisho ,tv hazishiki etí hakuna vingamuzi labda kwa kutumia dish na karatu cable!mwaka jana serikali yako sikivu ilikata analogy na kuleta digital,mbona sasa karatu hatuna vyote,analogy na digital?sina shaka na utendaji mzuri wa karatu cable kwan ni zaidi ya startime,ila je wengine hatuna haki ya kupata mawimbi ya service provide wengne?sitaongelea barabara za vumbi kwa kuwa karatu licha ya kupangiliwa vema kimitaa,haijua hata lami ina rangi gani.! Mwisho ,salam sana toka kwa rais wetu wa mioyoni, dr slaa...kwani apa upo kwenye taifa lake,ni busara to pay respect. Karibu karatu!