Ujinga wa wananchi chanzo cha Serikali kutapanya pesa ya umma

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,566
41,085
Nchi hii haitakuja kupata maendeleo kwa sababu wananchi tumekuwa wajinga. Na viongozi kwa sababu wanajua wanatawala Taifa la wajinga, hawana wasiwasi kabisa wala woga kwa sababu wanajua udhaifu wa watu wanaowatawala.

Pesa zinaibiwa, sisi cha kwanza tunaangalia ni nani anayetuhumiwa kuiba, nani aliyefichua huo wizi, nani aliyelalamika, au nani anayetuhumiwa kuiba, ni wa kundi gani na wa chama gani, kama vile kodi inapokusanywa kodi inaangaliwa wewe ni wa mlengo gani, na ni wa chama gani, na ni shabiki wa nani, na hivyo ulipe au usilipe kodi.

Viongozi wa upinzani na baadhi ya wananchi wa kawaida, mara kadhaa wamelalamikia matumizi mabaya na ya anasa ya Serikali, kama vile kununua magari ya kifahari, kuwa na ofisi za Serikali ambazo zingeweza kufutwa na mambo yakaenda bila matatizo, lakin kwa sababu labda hoja imetolewa na viongozi wa upinzani au kundi hasimu ndani ya CCM, basi wapenzi na mashabiki wa CCM au kundi jingine hawaangalii uzito wa hoja, wao ni kupinga tu kwa sababu watu wao wapo ndani ya Serikali, kama vile hayo matumizi ya anasa yanafanywa kuwakomoa wapinzani na yatawaathiri wapinzani pekee.

Pesa imeibiwa na kuporwa na utawala wa marehemu Magufuli, lakini kwa sababu ametajwa Marehemu Magufuli, kwa ujinga tu, mashabiki wa marehemu kwa sababu tuhuma zimetolewa na utawala wa Samia, wanasema ni uwongo. Yaani watu wameamua kupigania kulinda wizi na uporaji kwa sababu ulifanywa na wanayempenda.

Leo kuna tuhuma za upoteve au wizi dhidi ya Serikali ya Samia kuhusiana na pesa za mikopo, kwa sababu inaguswa Serikali ya kiongozi tunayempenda, basi weledi wa kujadili ili kuupata ukweli unakuwa hamna. Kitakachofanyika ni kupigania kuitetea Serikali na Waziri wa fedha.

Wakati wa utawala wa Mkapa, yeye mwenyewe marehemu kwenye kitabu chake amekiri kuwa CCM iliiba pesa ya umma dola milioni 100, sawa na zaidi ya shilingi bilioni 230, kwa sababu hoja imeibuliwa na Lisu, na tuhuma ni dhidi ya CCM, basi wanaCCM, na maadui wa Lisu na CHADEMA, wataungana kutetea ule wizi kwa sababu ulifanywa na chama chetu au chama tunachokipenda.

Kwa upumb.avu wetu huu wa sisi wananchi; viongozi na watendaji wa Serikali wataendelea kuchezea pesa zetu kama wanavyotaka maana kila anayefanya hivyo ana walinzi na watetezi. Hatima ya Tanzania daima imekuwa mashakani kutokana na kuwa na jamii ya watu wanafiki, waongo, walaghai na wasio na misimamo, wasiojielewa wanapigania na kutaka nini.

Mbaya zaidi hizi tabia mbaya unafiki, uwongo, ulaghai na kukosa misimamo, tunawarithisha na wazaliwa wetu. Mtu yupo UVCCM, bado hajawa kiongozi wala kupevuka sawasawa akili, anaanza kufundishwa namna ya kuwa mnafiki, mlaghai, mwongo na mtetezi wa uovu alimradi uovu huo umefanywa na mwenzetu ndani ya chama au ndani ya Serikali ya chama chetu.

Hatuwarithishi watu wetu matendo mema kama ujasiri, ukweli, uaminifu, kuchukia rushwa, kuchukia uobevu, kupigania haki na kuwa watu wenye maadili mema. Chipukizi wanafundishwa kuabudu na kusifia watawala, na siyo kuhoji.

Laiti kama tungekuwa na Taifa ambalo, MWIZI huwa ni mwizi bila ya kujali ni wa chama gani, kundi gani, au mwelekeo gani, hakika watawala wangeogopa na kuiheshimu hela ya umma maana wangejua kuwa wananchi wote ni adui wa wizi, tukifanya wizi au kutapanya pesa ya umma tunakuwa maadui wa Taifa zima.

Kama kuvunja katiba, au kugandamiza haki za watu au kugandamiza demokrasia na haki za watu, kwa sisi wananchi wote tungeyaona matendo hayo ni uovu dhidi yetu na jamhuri yetu, bila ya kujali anayefanya au kufanyiwa uovu huo ni wa chama gani, kundi gani au mwelekeo gani; hakika watawala na vyombo vya dola, wote wangeogopa kutenda uovu maana wangejua katika uovu wao hawana wa kuwatetea, na hawana rafiki katika huo uovu.

Lakini ujuha wa wananchi ndio unaofanya watawala na vyombo vya dola wasione shida kukanyaga haki za watu maana wanajua wakikanyaga haki za kundi fulani, kuna kundi litafurahia sana. Akishambuliwa au kutekwa au kuuawa mtu wa mlengo fulani, anajua atapongezwa na pengine kupandishwa hata cheo na kundi jingine.

Na hayo tuliyaona wakati wa awamu ya 4 kuhusiana na kifo cha Mwangosi, kamanda wa polisi alipandishwa cheo na kupelekwa makao makuu ya polisi kama vile akahakikishe nchi nzima inafanyiwa uovu ule, tumeyaona mengi zaidi wakati wa awamu ya 5, kwa polisi na mahakimu waliopandishwa vyeo kwa sababu waliwatesa na kuwakomoa wapinzani.

Tunaoongozwa, ndio tunaotakiwa kui=shape Serikali. Hata huko tunakoona kuna utawala mzuri, siyo kwamba watawala wanazaliwa ni watu wema sana, hapana, bali wananchi hawakubali kutendewa yasiyo sahihi na viongozi wao.
 
Tatizo siyo Wananchi bali Vyama vya Upinzani

Wanakula kodi zetu kwa njia ya Ruzuku na hatupati mrejesho wowote wa Huduma ya kutetewa!
 
Acha unaa,uzi umewapiga dongo watu kama nyie, kazi kutetea majizi kisa tu wa itikadi yako,na kuwavunja moyo watetezi na wanaopambana na majizi kisa tu wa itikadi tofauti na wewe🤔
Hapo Chadema hapajajaa majizi?

Mbona Mbowe analalamika mabilioni yake mliyokula?
 
Tatizo siyo Wananchi bali Vyama vya Upinzani

Wanakula kodi zetu kwa njia ya Ruzuku na hatupati mrejesho wowote wa Huduma ya kutetewa!
Hivyo vyama vya upinzani ni nani? Ni Mbowe, Lisu, Mnyika, Zito, n.k.? Au ni wananchi ndio wanaotengeneza vyama vya upinzani? Wao kama viongozi, hata wakiwa na msimamo thabiti, bila ya jitihada za wananchi kuwaunga mkono katika kupigania haki, watafanya nini?

Wao naamini wametoa mchango wao zaidi ya inavyohitajika. Lisu amemwaga damu yake, mpaka leo ni mlemavu kwaajili ya kupigania haki.

Mbowe amekaa jela si mara moja au mara mbili kwaajili ya kupigania katiba, Heche amepoteza mpaka mdogo wake kwaajili ya kuoiganua haki.

Ben Sanane amepotea uhai wake kwaajili ya kupigania haki. Sugu amekaa jela, Msigwa amejaa jela, n.k. Ulitaka wafanye nini zaidi na wajitoe kwa kiasi gani zaidi ya hapo?
 
Mleta mada,usifikili watu woote waliomo humu ni wajinga na mazuzu kama wewe,kila mlichopanga dhidi ya jpm watanzania wanajua,na kila mkakati ulionyuma ya migongo yenu mnsoufanya kwa sasa,watanzania wansjua.pia chuki zenu juu ya jpm watanzania wsnajua zilitokana na nini.

JamiiForums-1308820841.jpg
 
Hapo Chadema hapajajaa majizi?

Mbona Mbowe analalamika mabilioni yake mliyokula?
Pesa ya Mbowe haikuliwa na mtu bali iliporwa na Serikali na nyingine ni matumizi halali kuisaidia CHADEMA na katika kampeni za kupigania haki. Serikali iliamua kumpunguzia nguvu Mbowe kwa kumfilisi ili asiwe na mchango kwenye safari ya kuitafuta haki na uhuru wa watu.
 
Mleta mada,usifikili watu woote waliomo humu ni wajinga na mazuzu kama wewe,kila mlichopanga dhidi ya jpm watanzania wanajua,na kila mkakati ulionyuma ya migongo yenu mnsoufanya kwa sasa,watanzania wansjua.pia chuki zenu juu ya jpm watanzania wsnajua zilitokana na nn,,View attachment 2509019
Hii ni hoja kwaajili ya walio wazima wa akili. Haikuhusu wewe.
 
Pesa ya Mbowe haikuliwa na mtu bali iliporwa na Serikali na nyingine ni matumizi halali kuisaidia CHADEMA na katika kampeni za kupigania haki. Serikali iliamua kumpunguzia nguvu Mbowe kwa kumfilisi ili asiwe na mchango kwenye safari ya kuitafuta haki na uhuru wa watu.
Itachukua machawa kama haya karne tano kujua kinachoongelewa na kinachoendelea wakati huu🤔
 
Hivyo vyama vya upinzani ni nani? Ni Mbowe, Lisu, Mnyika, Zito, n.k.? Au ni wananchi ndio wanaotengeneza vyama vya upinzani? Wao kama viongozi...
Wewe unaamini hao uliowataja wanapigania Haki kweli?

Kupigania haki kuna mshahara?
 
Pesa ya Mbowe haikuliwa na mtu bali iliporwa na Serikali na nyingine ni matumizi halali kuisaidia CHADEMA na katika kampeni za kupigania haki. Serikali iliamua kumpunguzia nguvu Mbowe kwa kumfilisi ili asiwe na mchango kwenye safari ya kuitafuta haki na uhuru wa watu.
Mbowe alifilisiwa nini na Serikali?
 
Umepiga kwenye mshono
Ila niongezee tu, hii tabia ya kufurahia wizi na kukubali dhulma wanayo wengi sana.
Wengi wanatetea wizi na serikali ndio ya kwenza kutetea wizi na tabia ya kuwachekea majizi

Watu wanaiba kutwa ila unasikia tu PM au waziri akisema Takukuru mchukueni huyo

Mwisho wa siku anapelekwa sehemu nyingine ya ulaji zaidi
Hatusikia mtu kala mvua 30 kwa kuiba hela za mradi mzima

Ila tunasikia mama aliekamatwa na mnofu wa mnyama pori na kufungwa miaka 30

Kweli kabisa hao vijana wa UV wanafundishwa na kuhubiriwa kuwa wakatili na waongo badala ya kulelewa wawe waadilifu

Kila wakati naandika humu kama mnataka Taifa la waadilifu anzeni na watoto wenu kuwafundisha uadilifu
Ila tatizo mnalipa Ada zao kwa hela za wizi mnafikiri hao watoto watakuwa na karama kweli

Heko sana kwa kulitambua hilo vijana badilikeni msiingie chamani au kazi zao na kubadilika kuwa watu wachafu mnaliangamiza Taifa
 
Mbowe alifilisiwa nini na Serikali?
Kumbambikia kodi isiyo stahilil kwenye hotel ya familia, ni kuiua biashsra. Kuvunja na kuharibu miundombinu ya shamba lake ilikuwa ni sehemu za kuua vyanzo vyake vya mapato.

Kumpora jengo la bilcanas, ilikuwa ni sehemu ya dhamira hizo hizo chafu. Kufungia accounts zake za benki ilikuwa ni sehemu ya uchafu huo huo.

Hata kumweka ndani kwa mipindi kirefu na kumnyima dhamana, nia mojawapo ni kumfanya ashindwe kusimamia miradi yake ya kiuchumi.
 
Kumbambikia kodi isiyo stahilil kwenye hotel ya familia, ni kuiua biashsra. Kuvunja na kuharibu miundombinu ya shamba lake ilikuwa ni sehemu za kuua vyanzo vyake vya mapato. Kumpora jengo la bilcanas, ilikuwa ni sehemu ya dhamira hizo hizo chafu. Kufungia accounts zake za benki ilikuwa ni sehemu ya uchafu huo huo. Hata kumweka ndani kwa mipindi kirefu na kumnyima dhamana, nia mojawapo ni kumfanya ashindwe kusimamia miradi yake ya kiuchumi.
Lakin yeye amedai waliomfilisi ni Chadema siyo Serikali!
 
Mleta mada,usifikili watu woote waliomo humu ni wajinga na mazuzu kama wewe,kila mlichopanga dhidi ya jpm watanzania wanajua,na kila mkakati ulionyuma ya migongo yenu mnsoufanya kwa sasa,watanzania wansjua.pia chuki zenu juu ya jpm watanzania wsnajua zilitokana na nini.

View attachment 2509019
Ni kweli sio wote tuliomo humu JF ni wajinga na mazuzu, ila wewe ni zaidi ya wajinga na mazuzu wote.
 
Back
Top Bottom