Ujerumani yasema inatoa misaada kwa CCM kama inavyotoa kwa CUF, CDM etc

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,898
SHIRIKA la misaada ya Kijerumani la Konrad Adenauer Stiftung (KAS) limeiumbua serikali kwa kile ilichoita, “kuudanganya ulimwengu” kwamba baadhi ya nchi wafadhili zimekuwa zikisaidia vyama vya upinzani kuangusha serikali. Mwakilishi mkazi wa taasisi hiyo nchini, Stefan Reith, alisema shutuma za serikali kwamba wanavifadhili vyama vya siasa vya upinzani ni ya kusikitisha kwani nchi yao na taasisi za misaada hazijawahi kufadhili mambo kama hayo.

“Taasisi za Kijerumani zinafanya kazi na vyama vyote vya siasa nchini. Tunafanya kazi na CHADEMA, tunafanyakazi na CCM (Chama Cha Mapinduzi) na tunafanyakazi na CUF (Chama cha Wananchi). Kote huko hatutoi fedha moja kwa moja bali tunasaidia kuendesha semina, warsha, mikutano, mafunzo na ushauri. Basi,” alisema Reith.


Kauli ya mwakilishi huyo wa moja ya nchi zinazotoa misaada mikubwa kwa serikali ya Tanzania, imekuja baada ya kuwapo shutuma za muda mrefu kutoka kwa viongozi wa serikali na CCM, kwamba baadhi ya nchi wahisani zinasaidia CHADEMA kuangusha serikali. Alisema, “Kitendo cha serikali kusema CHADEMA inafadhiliwa na Ujerumani si sahihi na pengine ni jambo lisilo na maana kwa sababu kinachopata CHADEMA kutoka KAS ndicho hicho hicho kinachopata CCM na CUF kutoka FES,” alisisitiza.


Reith alitoa kauli hiyo jana katika hoteli ya New Afrika jijini Dar es Salaam, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa, aliyedai kuwa chama chake kimekuwa kikishambuliwa na serikali kwamba kinapokea fedha kutoka kwa wahisani ikiwamo Ujerumani kwa nia ya kuiangusha serikali ya Rais Jakaya Kikwete, wakati ambapo madai hayo hayana ukweli. Dk. Slaa alisema hawajawahi kupewa fedha kwa ajili ya maandamano ya kupindua nchi bali wamekuwa wakipata fedha kwa ajili ya kuendesha semina, makongamano na warsha.


“Nasema mbele ya wafadhili wetu Wajerumani waseme kama wametupa hata senti kufanya maandamano…hawa wanasaidia shughuli kama hizi za semina ya mabadiliko ya tabia ya nchi,” alieleza Dk. Slaa huku akimtolea macho mwakilishi huyo wa taasisi ya Kijerumani.
“Tusipumbazwe katika siasa zisizo na tija, mbona serikali inasaidiwa kwenye bajeti yake asilimia 34, wakisaidiwa wao sawa CHADEMA ikisaidiwa nongwa,” alieleza Dk. Slaa.
Katika mkutano wa Bunge la bajeti, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa

Tanzania, Benard Membe, alizituhumu nchi wahisani kuvisaidia baadhi ya vyama vya upinzani nchini kutaka kuiangusha serikali; madai ambayo yaliibua mjadala mkubwa bungeni. Akichangia kauli ya Membe, Mbunge wa Ubungo (CHADEMA), John Mnyika, alimtaka kiongozi huyo wa serikali kuthibitisha madai yake, kutaja nchi ambayo alisema inafadhili upinzani au kufuta kauli yake. Membe aligoma kufuta kauli hiyo, wala kutaja nchi aliyoituhumu, badala yake alisema, “Wahusika wanajijua.”

Source: Tanzania Daima
 
Uongo na unafiki unalimaliza Taifa!bila kubadilika na kuwa wakweli tutatangatanga bila mafanikio!
 
CCM wanataka wasaidiwe wao tu, wakisaidiwa vyama vingine ni nongwa na watalalamika kama vichaa vile.
 
hahaha napita tu, mtu mzima ukizodolewa aibu

Hivi akina Membe kabla ya kutoa matamko huwa wanarewind ukanda kwanza kuona cause and effect? Ni kuropoka kama yule niliyesoma kwenye kitabu cha Standard English hadithi ya Kalegesi. Serikali ya Kikwete na CCM wamejaa akina Kalegesi, ni kupayuka payuka tu.

Mt. Benedict wa Nursia mwanzishini wa shirika la Wabenedictin duniani alisema kama ifuatavyo kwa washirika wake: "Mwenye hekima hujulikana kwa maneno machache."
 
Hahaha slaa kaenda kulalamika kwa wajerumani .... Dah sijui what will his next move huyu mzee ...
 
CCM=chama cha malalamiko,chama cha manungayembe, chama cha mababu waropokaji, aibu imewakuta.
 
ccm na serikali vitasababisha Watanzania tunapigwa na nchi za magharibi!,hivi hawakumbuki kuwa ktk orodha ya nchi duniani zilizokuwa zinahifadhi magaidi yanayoishambulia Marekani,na washirka wake,Tanzania nayo imo? Tena ilkuwa ya32.Watanzania tukae chonjo na ccm na sirikali yake!!!!
 
Hahaha slaa kaenda kulalamika kwa wajerumani .... Dah sijui what will his next move huyu mzee ...



Hivi huo udokta uliupata chuo cha kata nn? Siamini kama hii ni akili ya chuo cha MUHAS.
 

• NI BAADA YA DK. SLAA KUWACHONGEA

Na Ratifa Baranyikwa

SHIRIKA la misaada ya Kijerumani la Konrad Adenauer Stiftung (KAS) limeiumbua serikali kwa kile ilichoita, “kuudanganya ulimwengu” kwamba baadhi ya nchi wafadhili zimekuwa zikisaidia vyama vya upinzani kuangusha serikali.


Mwakilishi mkazi wa taasisi hiyo nchini, Stefan Reith, alisema shutuma za serikali kwamba wanavifadhili vyama vya siasa vya upinzani ni ya kusikitisha kwani nchi yao na taasisi za misaada hazijawahi kufadhili mambo kama hayo.


“Taasisi za Kijerumani zinafanya kazi na vyama vyote vya siasa nchini. Tunafanya kazi na CHADEMA, tunafanyakazi na CCM (Chama Cha Mapinduzi) na tunafanyakazi na CUF (Chama cha Wananchi). Kote huko hatutoi fedha moja kwa moja bali tunasaidia kuendesha semina, warsha, mikutano, mafunzo na ushauri. Basi,” alisema Reith.

Kauli ya mwakilishi huyo wa moja ya nchi zinazotoa misaada mikubwa kwa serikali ya Tanzania, imekuja baada ya kuwapo shutuma za muda mrefu kutoka kwa viongozi wa serikali na CCM, kwamba baadhi ya nchi wahisani zinasaidia CHADEMA kuangusha serikali.


Alisema, “Kitendo cha serikali kusema CHADEMA inafadhiliwa na Ujerumani si sahihi na pengine ni jambo lisilo na maana kwa sababu kinachopata CHADEMA kutoka KAS ndicho hicho hicho kinachopata CCM na CUF kutoka FES,” alisisitiza.


Reith alitoa kauli hiyo jana katika hoteli ya New Afrika jijini Dar es Salaam, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa, aliyedai kuwa chama chake kimekuwa kikishambuliwa na serikali kwamba kinapokea fedha kutoka kwa wahisani ikiwamo Ujerumani kwa nia ya kuiangusha serikali ya Rais Jakaya Kikwete, wakati ambapo madai hayo hayana ukweli.


Dk. Slaa alisema hawajawahi kupewa fedha kwa ajili ya maandamano ya kupindua nchi bali wamekuwa wakipata fedha kwa ajili ya kuendesha semina, makongamano na warsha.


“Nasema mbele ya wafadhili wetu Wajerumani waseme kama wametupa hata senti kufanya maandamano…hawa wanasaidia shughuli kama hizi za semina ya mabadiliko ya tabia ya nchi,” alieleza Dk. Slaa huku akimtolea macho mwakilishi huyo wa taasisi ya Kijerumani.


“Tusipumbazwe katika siasa zisizo na tija, mbona serikali inasaidiwa kwenye bajeti yake asilimia 34, wakisaidiwa wao sawa CHADEMA ikisaidiwa nongwa,” alieleza Dk. Slaa.


Katika mkutano wa Bunge la bajeti, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Benard Membe, alizituhumu nchi wahisani kuvisaidia baadhi ya vyama vya upinzani nchini kutaka kuiangusha serikali; madai ambayo yaliibua mjadala mkubwa bungeni.


Akichangia kauli ya Membe, Mbunge wa Ubungo (CHADEMA), John Mnyika, alimtaka kiongozi huyo wa serikali kuthibitisha madai yake, kutaja nchi ambayo alisema inafadhili upinzani au kufuta kauli yake.


Membe aligoma kufuta kauli hiyo, wala kutaja nchi aliyoituhumu, badala yake alisema, “Wahusika wanajijua.”


Akizungumza kwenye semina hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya New Afrika, Reith alisema utafiti uliofanywa na Umoja wa Mataifa (UN) unaonyesha Tanzania na nchi zilizoko Afrika Mashariki zimeathirika vibaya kuliko nchi nyingine duniani kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi na matokeo hayo ni matukio yanayoshuhudiwa hivi sasa ya ukame, mafuriko ya msimu, tatizo la umeme na uhaba wa chakula.


Alisema katika siku zijazo fedha nyingi za wafadhili zitakuwa zikielekezwa kwenye mabadiliko ya tabia ya nchi, na kutokana na serikali ya Tanzania kushindwa kutekeleza mikakati yake, upande wa upinzani utafaidika kisiasa na kiuchumi.


Mbali na hilo, Reith aliishangaa serikali kushindwa kutumia teknolojia mpya katika kushughulikia tatizo la umeme ambalo nalo limetokana na tabia ya nchi, na kuhoji kwa nini tuisubiri TANESCO.


Katika hilo, Dk. Slaa aliipiga kijembe falsafa inayotumiwa na CCM akisema kuwa huwezi kuzungumzia maisha bora kabla hujatekeleza mikakati ya kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi, na kuongeza kuwa CHADEMA imeliona hilo na inafikiria nini cha kufanya ili kuleta maisha bora.


Alisema, “CHADEMA tumeona tushirikiane na Kamati Kuu kuweka sera endelevu ya kuhifadhi mazingira kwa kuanzia na chombo cha kisera kisha kwenda kwenye ngazi mbalimbali, ni kazi ambayo itaifanya Tanzania kuwa sehemu bora ya kuishi binadamu.”


Akionekana kuibeza falsafa hiyo ya CCM ya maisha bora kwa kila Mtanzania Dk. Slaa alisema, “CHADEMA inafikiria mikakati na mipango sahihi ya kuleta maisha bora…maisha bora hayaji kwenye majukwaa.


“Huwezi kuzungumzia kilimo kama maji hakuna, huwezi kuzungumzia ufugaji kama miti hakuna…hatutaogopa kusemwa tumeanzia hapa, tutakwenda kusaidia wananchi tutaweka pamba masikioni kupambana na propaganda; tutafanya kila linalowezekana kuipeleka nchi kwenye neema,” alieleza mwanasiasa huyo machachari nchini.


Dk. Slaa aliitaka serikali kutekeleza yale inayopaswa kutekeleza na kuitaka ipunguze safari za kuhudhuria mikutano ya nje ya nchi kama hakuna tija yoyote.

 
Tatizo la Upinzani wa Tanzania sio International; Kenya Upinzani wao unajulikana nje ya Mipaka ya Kenya

Tunahitaji Upinzani wetu Uwe International
 
acha kukariri mdogo angu! Sio kila docta ni wa medicine.



kuna wakati alijisifia mwenyewe kuwa ni medical docta dude ndio maana najaribu kulinganisha fani yake na upupu anaoumwaga hapa sioni uwiano
 
kuna wakati alijisifia mwenyewe kuwa ni medical docta dude ndio maana najaribu kulinganisha fani yake na upupu anaoumwaga hapa sioni uwiano

Acha upuuzi wewe bwana mdogo,kama hujui vitu si uulize kwanza ndo uchangie hoja
 
Tatizo la Upinzani wa Tanzania sio International; Kenya Upinzani wao unajulikana nje ya Mipaka ya Kenya

Tunahitaji Upinzani wetu Uwe International
Mkuu hakuna upinzani umejulikana kimataifa hapa Afrika bila kumwaga damu! Nafikiri muhimu ni elimu ya uraia kwa watz ili wafanye maamuzi sahihi
 
Back
Top Bottom