SoC03 Ujasiriamali shuleni

Stories of Change - 2023 Competition

Mama Alfan

New Member
Jul 4, 2023
1
2
Ujasiriamali ni stadi inayomuwezesha mtu kubuni na kuanzisha miradi mbalimbali ya uzalishaji mali kulingana na fursa zilizopo katika mazingira yake.Kuna aina nyingi za ujasiriamali kama vile kuuza mbogamboga,kutengeneza sabuni na nyinginezo nyingi.

Uzalishaji unaweza kuwa wa aina tofautitofauti pia husaidia vijana kujikwamua na shida mbalimbali pia hupelekea vijana kutokua tegemezi Kwa wengine.

ujasiriamali unapaswa kufundishwa shuleni kuanzia shule za msingi,sekondari na vyuoni ili kufanya vijana waweze kujitegemea na kupata ujuzi mbalimbali mara wanaposhindwa kuendelea na masomo yao.somo la ujasiriamali shuleni litamfanya kijana kuwa mkakamavu na hodari katika kujitafutia kipato halali.

Ujasiriamali huwaepusha vijana na makundi mbalimbali ya kiuhalifu yanayo zuka maeneo mengi,Somo hilo pia likifundishwa mashuleni linaweza kusaidia kuepukana na wingi wa watoto/vijana wasio na ajira kwasababu vijana wanaweza kujiajiri wenyewe. Wakihitimu masomo yao bila kusubiri ajira.

Somo la ujasiriamali ni Somo linaloweza kuinua uchumi wa nchi kwasababu ni Somo pana ambalo halichagui umri na halina ukomo na nisomo bunifu pia ni Somo lenye manufaa Kwa pande zote mbili na linafanya watu kujifunza zaidi kwani linaleta maendeleo yenye tija Kwa jamii husika, Mfano vijana wengi Sasa wanaweza kutengeneza bidhaa mbalimbali za viwandani,kama vile sabuni za maji,sabuni za miche na batiki.

Ujasiriamali ukifundishwa shuleni ni nguzo imara Kwa jamii na kizazi cha Sasa na kitasaidia vijana wengi kuepukana kutazama video mbalimbali za ngono kwenye mitandao ya kijamii na watatumia mitandao hiyo ya kijamii kutangaza fursa walizo nazo ili kujipatia wateja wa maeneo tofauti tofauti na aliyopo yeye.

Hivyo Somo la ujasiriamali ni muhimu shuleni na likifundishwa litalenga kuinua uchumi wa nchi na kuepukana na vitendo viovu vya unjaji wa amani.
 
ujasilia mali haliwezi kuwa somo labda topic ziwe nini mbona vyuoni linafundiswa sasna na bado graduets wanawaza ajira hakuna wanachoweza kubuni au kuanzisha zaidi ya kubeba bahasha na kuapply job on line wakati wale wajasi wa ukweli wanapiga mishe toka chekechea...
wazo langu
kuna vitu nimevijua baadae sana lakini nilijikuta nimo ndani ya ujasi kuna mavitabu kama ya kina obii okonko...zile story zinahamasihsa mtu asome apate kazi aanze ku chase girls..siji zawadi ya ushindi sijui nini vingi tu..vingeweka vitabu vinavyo hamasisha au kuibua uthubutu wa watu kufanya biashara au ujasi ila ambao somo lingewakolea lazima wangeachana na masomo(amini nakuambia) huwezi ukavifungamanisha ujasilia mali na hii elimu yetu ya sasa inalenga mtu asome aje aajiriwe wote taget ni hio kama taget sio hio watu wangeacha kusoma na kufuata taget zao..mzazi yupo radhi kulipa mamilioni kila mwaka lakini milioni hata moja ya mtaji mtoto akimaliza hawezi kumpa zaidi ya kumpa hongo ya kulipa kwenye interview na nauli....hapo ndio siwaelewi wazazi wa kibongo...hata we na rasilimali hakupi mpaka aanze kungoka meno..huku wakati akitafuta anasema ni ya watoto..kwa hio kila mwaka kila siku waafrika tutakua tunazalisha kizazi rat race...kuanza na kujirudia pale pale... wachache wajasila mali wanaweza kuwafundisha watoto kile wanahofanya wao ni kulipa ada na daftari akitegemea mwanae apate elimu bora labda atatoboa huko akiajiriwa ila elimu itakayomjenge mtoto awe mjasilia mali mzazi anaona ni kuteseka kwa mtoto au status mbaya ya mtoto....kwa hio tubadilike sisi wazazi somo la fedha linafundishwa nyumbani lakini majumba yetu yamekuwa sehemu ya kuwaspoli watoto wetu tukiona kuwa tuanishi maisha ya kifahari nao wafaharike...tukitegemea serikali ibadili mambo...change ni wewe change ni sisi...
 
Back
Top Bottom