Uimara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo

Uimara wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo

super thinker

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2010
Posts
370
Reaction score
109
Hi ni kwao wote wenye tamaa ya kufa kwa hiki chama,

Sisi kama wafuatiliaji wa mambo yatokeayo kwa umakini na uweledi wa hali ya juu, tuna imani kuu na viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo katika wafanyayo, najua kama wewe ni kati ya watu wanaotamani chama hiki kife unatambua wazi kwamba safu ya uongozi kwenye hiki chama ni imara hakuna, kimoyo moyo unakubali na najua hata unatamani kingekamata nchi.

Ni watu wanaofanya mambo kwa umakini na uweledi uliotukuka katika kila nyanja ya kiuongozi wa kisiasa.

Histry tells a lot on the strength ya viongozi hawa na haina haja ya kuanza kuelezea hapa. Sio tu safu ya juu ya uongozi, hata wanachama wake "kwa asilimia kubwa" ni watu makini, wasioyumbishwa na wanaofanya maamuzi baada ya upembuzi yakinifu wa mambo, pole yao wanaohisi kuna kufa kwa hiki chama hata siku moja.

Lengo si kukiangusha "the green" but kuwa na ukombozi wa 2 wa mtanzania na ukombozi huo unaanza na kukiangusha hiki kilichopo sasa madarakani.

Ushauri
Kama watanzania, tuyafanye maisha yetu yawe na tendency ya kufanya maamuzi baada ya kuwaza kiundani kidogo, na si kukurupuka,kurubuniwa au kudanganywa. Kama ni msomi, usiidharau elimu yako kwa kutetea issues zibomoazo nchi, kuwa na msimamo katika kuchambua national events na kuwa stable katika kuconclude, kamwe usiupambe uongo ama kuufukia ukweli, kwa njia hiyo unaikalia elimu yako na utashi ulio nao unless hauithamini.

Nalink uimara wa kisomo, si kisomo tu, na utashi ulio nao na uimara wa viongozi wa chadema kwani wafanyayo ni wazi yanatakiwa kuwa supported, na mtu yoyote afanyaye visivyo waziwazi kama yatokeayo sasa achukuliwe hatua stahiki bila kujali uimara wake katika chama na nchi kwa ujumla. Thats the spirit ya mtu yoyote mwenye msimamo. Mke hawezi kukucheat kwenye ndoa mara kadhaa, ukapata tetesi, ukaconfirm then ukamvumilia tuuuuuuuu, unafuga chatu atakayekumeza any time.

Chadema songa mbele, tuchambuao mambo kwa umakini na uimara tuko nyuma yenu na tunajua mnatambua hilo na ndo maana mnatoa maamuzi yanayoweza kuonekana sio lakini mnajua watu wapo nyuma yenu na ni watu makini.

Peoples' power - Nguvu ya uma daima
 
Fanyieni kazi mkakati wa ushindi 2013 na mjibu hoja hizo hadharani. Cdm kwishney
 
Nakubaliana nawe mkuu. Tatizo la sisi Watanzania hatupendi kufikiri ila tunapenda kufuata mikumbo, wakati mwigine kwa kutofahamu au kwa kujaribu kupunguza shida zetu za kila siku za njaa au kwa kutafuta umaarufu. Ndiyo maana nchi inadidimia kimaendeleo kila siku kwa sababu hiyo. Chama tawala kinajua udhaifu huo wa watu kufuata ya mikumbo kwa sababu ya njaa yao kali waliyowasababishia kwa makusudi ili waweze kuwamudu, ndiyo maana jambo lisilo na kichwa wala miguu CCM wanaliavalia njuga wanajua tu kuna malimbukeni kibaao watawafuata.Lakini masuala nyeti yanayohusu maendeleo yetu sisi tunayapuuza na kuwakabidhi wafadhiri wayatatue. Kwa mwendo huu tutafika !!!? Hapa kufika katika safari ya maisha bora kwa kila mtanzania mpaka aondolewe msababishaji CCM madarakani.
 
Chadema Daima.
Watimuliwa wote sasa chali siku 14 Ni jibu tosha.
 
CHADEMA (a) na CHADEMA (b).
Kifo cha CHADEMA ni kibaya sana hakijawahi tokea duniani.
 
Inashangaza kuona vichwa mbalimbali vya habari vikishabikia sakata la akina Zitto Kabwe kama ndio anguko au mpasuko ndani ya CHADEMA. Binafsi sioni kama kuna mpasuko wala vipande ndani ya CHADEMA ila naona kinazidi kuimarika baada ya kugundua mbinu za usaliti na hujuma ambazo zingefanikiwa zingechangia kukivuruga chama.
 
wee tulia tu anafukuzwa waende naye huku kwa maCCM, kuna kijama cha temeke nacho jana kimetoa tamko, nakione huruma kinapotezwa sasa hivi
 
Unasukumwa na UKABILA na UKANDA,Karata zenu muzichange vizuri,mustafute mchawi baadae.
 
Ndo maana unaona wewe binafsi hakuna anguko,lakini wenye upeo mpana wameshaona tatizo la chadema.
Kama chama kinazidi kuimarika,kuna wanachama wangapi wameingia nakutoka baada ya ZZK kuvuliwa madara?
 
kama magamba, kwa mitindio ya bongo zao, wanadhani kwamba chadema itakufa au kudorora, watasubiri sana.
 
Back
Top Bottom