Uhusiano wa usiku na kifo

Uhusiano wa usiku na kifo

''Allaah Anafisha nafsi wakati wa mauti yake; na zile zisizokufa katika usingizi wake, basi Huzizuia ambazo Amezikidhia mauti, na Huzituma nyingine mpaka muda wake maalumu uliopangwa. Hakika katika hayo bila shaka kuna Aayaat (dalili, ishara n.k) kwa watu wanaotafakari.'' .39:42
 
Wakuu, amani iwe kwenu.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza nimekuwa nikijiuliza ni kwanini watu wengi hasa wagonjwa waliolazwa mahospitalini hufariki usiku na sio mchana?

Karibuni tushirikishane mawazo.
Usiku ni muda wa mashetani kujivijali, mchana ni wa Mungu wa kweli na malaika wema.
 
Mkuu sababu ya wagonjwa kufariki usiku ipo kisayansi kabisa , kwa kuwa wagonjwa wengi wanaofariki muda wa usiku huwa wamedhoofu na mifumo yao ya upumuaji huwa imezidiwa katika kuchuja hewa chafu na safi (O2 na CO2). Hivyo basi kwa kuwa usiku huwa hakuna hewa ya Oxygen ya kutosha kama ilivyo kwa muda wa mchana kwani muda wa mchana (day time) mimea huvuta CO2 katika kujitengenezea chakula chake na hutoa Oxygen ambayo wanyama akiwemo binadamu huitumia. Wakati wa Usiku (no Sun light) mimea hutumia oxygen na kutoa CO2 hivyo kufanya hewa ya Oxygen kupungua na kusababisha wagonjwa hasa wale waliodhoofu kukosa hewa ya O2 kwa kiwango husika hivyo kufa.
Asante kwa kufikiri kisayansi mkuu. Sisi kila kitu ni uchawi tu. Tungekuwa tunajaribu kwanza kutafuta sababu za kisayansi tunapokabili jambo kama ulivyofanya hapa kabla ya kukimbilia uchawi naamini tungekuwa kwingine kimaendeleo.
 
Mbona mi maza alifariki mchana, acha uongo mtoa mada!
 
Kila nafsi itaonja mauti! ... umemaanisha hivyo kwa sababu gani?
Kwa kuwa umesema usiku ni wa mashetani kujivinjari na mchana ni wa Mungu wa kweli
 
Kifo kama nicha mapenzi ya mungu mtu hufa mda ule aliozaliwa kama ilivyo mtoto anavyo zaliwa mda mimba iliyotunga hivyo watu wengi hufa usiku kwakua pia watu wengi huzaliwa usiku kutokana naukweli kwamba mimba nyingi hutungwa usiku
 
Muda wote Mungu anatawala,,, usiku nguvu za Giza huwa zinafanya kazi Sana'a,,,,lkn kifo hakihusian unless kuna mazingira ya nguvu za Giza,,,,wagonjwa hufa usiku kwa sababu body system zimetulia,,,normal rate and routine of blood supply inakuwa dogo,,, if no blood supply no Life,,,,
 
Kifo kama nicha mapenzi ya mungu mtu hufa mda ule aliozaliwa kama ilivyo mtoto anavyo zaliwa mda mimba iliyotunga hivyo watu wengi hufa usiku kwakua pia watu wengi huzaliwa usiku kutokana naukweli kwamba mimba nyingi hutungwa usiku
hiii ni statement mpya katika maisha yangu,asante kwa kuw nmejifunza
 
Mbona hujiulizi kwa nini kidonda hupona usiku na Si mchana? Ukitaka kuangalia maendeleo ya kidonda asubuhi
 
Kwa sababu MWENYEZI MUNGU ameufanya usiku uwe na mahusiano thabiti na ROHO,ndo mana unapofika usiku watu weng tunafanya mazoezi ya KUFA kwa KULALA haimaanishi mchana watu hawalali ispokuwa ulalaji wa mchana ni tofauti na wa usiku,
[1]Mtu akirud anavua nguo alizokua nazo mchana ili aoge huenda akachukua taulo au asichukue kama anavovuliwa maiti nguo zake baada ya kufa ili aoshwe kwa waislamu nako kuna kipande cha sanda[taulo] kwa ajili ya kumfutia maji mait baada ya kuoshwa,
[2]Ukirud unaweza ukajipulzia manukato au asijipulizie kama ambavo maiti nazo zinapoandaliwa zinapuliziwa
[3]Baada ya kuoga utavaa nguo tofaut na ulizoshindia utavaa ya kulalia hata maiti nae huvalishwa nguo nyingn baada ya kuoshwa tofaut na ile aliyopatia umauti
[4]Ukimaliza utaingia ktandan kwa ajili ya kulala kama ambavyo maiti yeye hubebwa mpaka kitandani kwake[kaburini].
[6]Yawezekana ukasali kabla ya kulala kama ambavyo maiti inaswaliwa[fanyiwa maombi]kabla ya kuzikwa,
[7]Utataka giza kama giza la kaburini basi nawe utazima taa.
Hakuna sababu ya kisayansi hata moja. Ni mkururo wa usambamba (parallelism) usio na uhusiano wo wote wa cause and effect. Mwafrika na imani zake za mauzauza sijui mpaka lini. Muulize mzungu hili swali na more than 75% utapata jibu la kisayansi mf. ishu za mfumo wa damu, quality ya Oksijeni usiku, ubongo kuwa dormant kidogo usiku etc...
 
Back
Top Bottom