Uhusiano wa kanisa na bendera hasa ya Marekani

Uhusiano wa kanisa na bendera hasa ya Marekani

romaki

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2013
Posts
477
Reaction score
218
Habari wanajamii,

Nimekuwa nikijiuliza na pia kufanya research na kusoma mada mbalimbali kuhusu uwepo wa bendera hasa ya Marekani katika makanisa ya kilokole hasa yanayomilikiwa na watu binafsi Lkn bado sijapata jibu sahihi nini maana yake, yawezekana uwepo wa bendera ya taifa flani mahali flani ni kwamba unakubaliana na sera zote za hilo taifa?

Naomba mwenye kujua siri au maana yake halisi atufahamishe na sisi tafadhali.

Nawasilisha.
 
Mkuu hiyo ya msikitini ndo naiona Leo, hiyo ni ya kwao wenyewe ama ya taifa flani?
 
Mkuu hiyo ya msikitini ndo naiona Leo, hiyo ni ya kwao wenyewe ama ya taifa flani?
Kwahiyo hapa hofu ni kuwa na bend era ya taifa Fulani!!??, il a bend era yenye siraha kwenye nyumba ya ibada ni sahihi!?
 
Habari wanajamii

Nimekuwa nikijiuliza na pia kufanya research na kusoma mada mbalimbali kuhusu uwepo wa bendera hasa ya marekani katika makanisa ya kilokole hasa yanayomilikiwa na watu binafsi Lkn bado sijapata jibu sahihi nini maana yake, yawezekana uwepo wa bendera ya taifa flani mahali flani ni kwamba unakubaliana na sera zote za hilo taifa? naomba mwenye kujua siri au maana yake halisi atufahamishe na sisi tafadhali.

Nawakilisha.

Unaposema bendera ya marekani badala ya bendera za mataifa mbalimbali unakosea na unajaribu kujenga mada ya kwako mwenyewe.Uwepo wa bendera zamataifa kanisani huonyesha kwamba injili ni kwa watu wa mataifa yote ikumbukwe pia haiwezi kuwepo bendera ya marekani bila uwepo wa bendera ya israel ambayo wakristo huamini ni taifa teule la Mungu.
 
mbona katoliki wanabendera ya vatican au hujui vatican ni nchi
 
Unaposema bendera ya marekani badala ya bendera za mataifa mbalimbali unakosea na unajaribu kujenga mada ya kwako mwenyewe.Uwepo wa bendera zamataifa kanisani huonyesha kwamba injili ni kwa watu wa mataifa yote ikumbukwe pia haiwezi kuwepo bendera ya marekani bila uwepo wa bendera ya israel ambayo wakristo huamini ni taifa teule la Mungu.
kwanini marekani na sio burundi?.

Au ule ubabe wa kivita na mandege ya hatari unawapa heshima maalumu?
 
Usipoteze muda wako mkuu na hawa walaghai. tumia mda wako kutafuta pesa, kuendeleza ujuzi na maarifa yako na pia kuendeleza jamii yako. hao ni wezi tu hawana hata falsafa ya kumkomboa mwanadam hasa mtu wa Africa zaidi ya kujitajirisha wenyewe

Habari wanajamii

Nimekuwa nikijiuliza na pia kufanya research na kusoma mada mbalimbali kuhusu uwepo wa bendera hasa ya marekani katika makanisa ya kilokole hasa yanayomilikiwa na watu binafsi Lkn bado sijapata jibu sahihi nini maana yake, yawezekana uwepo wa bendera ya taifa flani mahali flani ni kwamba unakubaliana na sera zote za hilo taifa? naomba mwenye kujua siri au maana yake halisi atufahamishe na sisi tafadhali.

Nawakilisha.
 
kwanini marekani na sio burundi?.

Au ule ubabe wa kivita na mandege ya hatari unawapa heshima maalumu?

Hujanielewa nini? Nimesema bendera za mataifa iwe taifa kubwa au dogo mbona hamuhoji uwepo wa bendera ya tanzania, kenya israel china huwezi weka bendera za mataifa yote inategemea muwekaji amependelea ipi.Kumbuka injili ni kwa watu wote matajiri na maskini na mataifa yote matajiri na maskini na marekani inawakilisha matajiri na taifa lenye nguvu so wanahaki ya kupata injili but siyo lazma kuweka bendera za hiyo ni pendekezo la muhusika kuwaonyesha watu kuwa injili si ya watu fulani tu bali wote wana haki ya kupokea.asante
 
vitu vingine ni kweli vinaleta maswali kichwani, ila nafurahi nimefunguliwa maana ya zile flags maana hata pale kwa pastor lusekelo naziona nikimcheki kwa tv.
 
kwanini marekani na sio burundi?.

Au ule ubabe wa kivita na mandege ya hatari unawapa heshima maalumu?

Kiongozi sio bendera za Marekani tu!? Kuna bendera za mataifa mengi tu, hata yetu pia huwa inakuwepo. Lakini mwisho wa siku dini inahitaji vitu vingi ili iendelee na Marekani ni moja ya mataifa yaliyochangia sana katika uendelezaji wa dini ya Kikristo kwa hiyo sio vibaya kuwatambua.
 
Makanisa mengi ya kipentecoste yameanzia USA so yamekuwa kama nationalistic churches!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Habari wanajamii

Nimekuwa nikijiuliza na pia kufanya research na kusoma mada mbalimbali kuhusu uwepo wa bendera hasa ya marekani katika makanisa ya kilokole hasa yanayomilikiwa na watu binafsi Lkn bado sijapata jibu sahihi nini maana yake, yawezekana uwepo wa bendera ya taifa flani mahali flani ni kwamba unakubaliana na sera zote za hilo taifa? naomba mwenye kujua siri au maana yake halisi atufahamishe na sisi tafadhali.

Nawakilisha.

Kwa kifupi USA ndiye mfadhili mkuu wa makanisa ya Kilokole.
 
Habari wanajamii

Nimekuwa nikijiuliza na pia kufanya research na kusoma mada mbalimbali kuhusu uwepo wa bendera hasa ya marekani katika makanisa ya kilokole hasa yanayomilikiwa na watu binafsi Lkn bado sijapata jibu sahihi nini maana yake, yawezekana uwepo wa bendera ya taifa flani mahali flani ni kwamba unakubaliana na sera zote za hilo taifa? naomba mwenye kujua siri au maana yake halisi atufahamishe na sisi tafadhali.

Nawakilisha.
Hakuna siri.
Mara nyingi ni multination aka international churches.
Hata kama siyo kuna tatizo lolote kuwa na bendera ya nchi fulani kanisa, nyumbani or wherever?
 
Back
Top Bottom