lyambalyamfipa
New Member
- Jan 27, 2020
- 1
- 3
MHESHIMIWA RAIS MAGUFULI,
Wafanyakazi wa NSSF, tunaendelea kuwasilisha malalamiko yetu kwako kuhusu ufisadi na ubaguzi uliopo shirikani ili ufanye uchunguzi wako na uchukue hatua stahiki ili kuliokoa shirika letu.
1. Udanganyifu katika utendaji wa shirika.
Mkurugenzi Mkuu kwa makusudi kabisa aliopoingia shirikani alipunguza malengo yaliyokwisha wekwa na mtangulizi wake ili aonekane 'anaperfom" hivyo taarifa zikawa zinapelekwa wizarani zikionesha anavuka malengo kwa mwaka wa 2018/2019.
Mwaka 2019/2020 kwa ujanja kabisa hakukuwa na ongezeko lolote la malengo bali alichofanya ni kujumlisha michango na wanachama waiohamia NSSF kutoka mifuko mingine kwenye makusanyo ya mwaka uliopita, hivyo inaonekana ameongeza makusanyo kwa asilimia kubwa sana na amekuwa akipita na kujisifu kwa hilo.
2. Ubaguzi kwa wafanyakazi.
Mkurugenzi huyu amekuwa akifanya ubaguzi wa wazi baina ya staff aliotoka nao PPf na sisi wa NSSF, kwa mfano staff wote wa PPF wamewekwa makao makuu tu hawapelekwi mikoani.
Aidha kuna staff ambao PPF hawakuwa na cheo chochote lakini walilopokuja NSSF wamepewa umeneja.
3. Ubaguzi katika mishahara.
Inafahamika wazi kuwa mfanyakazi wa umma anapohamishiwa kwenye taasisi nyingine anahamia na mshahara wake iwapo ni mkubwa.
PPF mishahara yao ilikuwa ni mikubwa kuliko NSSF. Lakini kwa hila kabisa akatumia kipengele cha kodi ya nyumba na kuwqaongezea mishahara staff aloikuja nao kutoka PPF, kisha wakaingia mikataba na mabenk chap chap wakaikopea nyongeza ile yote hii mantiki yake ni kukwepa hoja za CAG iwapo wangekopeshana kupitia mikopo ya shirika na vile vile kujilipa in advance in case of anything. Jamaa ni mjanja sana yeye na watu wake.
4. Dhuluma kwenye makato ya wafanyakazi.
Ndani ya NSSF kuna mpango wa uchangiaji wa wanachama wa NSSF-Hiari kwa wafanyakazi ambapo mwajiri anachangia 10% na mfanyakazi anakatwa 10%.
Mpango huu haupo NSSF peke yake bali mashirika mengi yana mpango kama huu kwa namna tofauti hata PPF walikuwa nao na walilipana mafao mifuko ilipounganishwa.
Mwezi Desemba 2018 mkurugenzi mkuu alisitisha kuchangia 10% yake bila taarifa yoyote huku akiendelea kuwakata wafanyakazi mpaka hivi leo licha ya wafanyakazi wengi kuandika barua kuomba makato hayo yasitishwe.
Mwezi Desemba 2019 mkuu huyu aliitisha baraza la majadiliano na kuwafahamisha kuwa alisitisha makato kutokana na agizo lako ulilotoa ulipokutana na viongozi wa mifuko mwezi Desemba, 2018 hivyo amekuja na mpango mpya ambao itabidi michango yote iliyokokwisha changiwa NSSF kiasi cha bilioni 23 kitolewe na uanzishwe mfuko binafsi wa wafanyakazi utakao kuwa na bodi yake na uongozi wake utakaojumuisha na wafanyakazi waliohamia.
Wawakilishi wa wafanyakazi walijua huu ni mchezo mchafu aina ya DESI, hivyo wakaugomea mpango huo na ikakubaliwa kuwa makato kwa wafanyakazi yasitishwe kuanzia mwezi Desemba, 2019.
Na michango iliyopo iendelee kubaki NSSF, Cha kushangaza makato yanaendelea mpaka sasa na hatujui kimsingi mkuu anahitaji nini hasa.
Mheshiwa Rais, tunaomba uingilie kati, kwani tunakufahamu na wewe ni msema kweli na mtetezi wa wanyonge.
Mungu akubariki!
Wafanyakazi wa NSSF, tunaendelea kuwasilisha malalamiko yetu kwako kuhusu ufisadi na ubaguzi uliopo shirikani ili ufanye uchunguzi wako na uchukue hatua stahiki ili kuliokoa shirika letu.
1. Udanganyifu katika utendaji wa shirika.
Mkurugenzi Mkuu kwa makusudi kabisa aliopoingia shirikani alipunguza malengo yaliyokwisha wekwa na mtangulizi wake ili aonekane 'anaperfom" hivyo taarifa zikawa zinapelekwa wizarani zikionesha anavuka malengo kwa mwaka wa 2018/2019.
Mwaka 2019/2020 kwa ujanja kabisa hakukuwa na ongezeko lolote la malengo bali alichofanya ni kujumlisha michango na wanachama waiohamia NSSF kutoka mifuko mingine kwenye makusanyo ya mwaka uliopita, hivyo inaonekana ameongeza makusanyo kwa asilimia kubwa sana na amekuwa akipita na kujisifu kwa hilo.
2. Ubaguzi kwa wafanyakazi.
Mkurugenzi huyu amekuwa akifanya ubaguzi wa wazi baina ya staff aliotoka nao PPf na sisi wa NSSF, kwa mfano staff wote wa PPF wamewekwa makao makuu tu hawapelekwi mikoani.
Aidha kuna staff ambao PPF hawakuwa na cheo chochote lakini walilopokuja NSSF wamepewa umeneja.
3. Ubaguzi katika mishahara.
Inafahamika wazi kuwa mfanyakazi wa umma anapohamishiwa kwenye taasisi nyingine anahamia na mshahara wake iwapo ni mkubwa.
PPF mishahara yao ilikuwa ni mikubwa kuliko NSSF. Lakini kwa hila kabisa akatumia kipengele cha kodi ya nyumba na kuwqaongezea mishahara staff aloikuja nao kutoka PPF, kisha wakaingia mikataba na mabenk chap chap wakaikopea nyongeza ile yote hii mantiki yake ni kukwepa hoja za CAG iwapo wangekopeshana kupitia mikopo ya shirika na vile vile kujilipa in advance in case of anything. Jamaa ni mjanja sana yeye na watu wake.
4. Dhuluma kwenye makato ya wafanyakazi.
Ndani ya NSSF kuna mpango wa uchangiaji wa wanachama wa NSSF-Hiari kwa wafanyakazi ambapo mwajiri anachangia 10% na mfanyakazi anakatwa 10%.
Mpango huu haupo NSSF peke yake bali mashirika mengi yana mpango kama huu kwa namna tofauti hata PPF walikuwa nao na walilipana mafao mifuko ilipounganishwa.
Mwezi Desemba 2018 mkurugenzi mkuu alisitisha kuchangia 10% yake bila taarifa yoyote huku akiendelea kuwakata wafanyakazi mpaka hivi leo licha ya wafanyakazi wengi kuandika barua kuomba makato hayo yasitishwe.
Mwezi Desemba 2019 mkuu huyu aliitisha baraza la majadiliano na kuwafahamisha kuwa alisitisha makato kutokana na agizo lako ulilotoa ulipokutana na viongozi wa mifuko mwezi Desemba, 2018 hivyo amekuja na mpango mpya ambao itabidi michango yote iliyokokwisha changiwa NSSF kiasi cha bilioni 23 kitolewe na uanzishwe mfuko binafsi wa wafanyakazi utakao kuwa na bodi yake na uongozi wake utakaojumuisha na wafanyakazi waliohamia.
Wawakilishi wa wafanyakazi walijua huu ni mchezo mchafu aina ya DESI, hivyo wakaugomea mpango huo na ikakubaliwa kuwa makato kwa wafanyakazi yasitishwe kuanzia mwezi Desemba, 2019.
Na michango iliyopo iendelee kubaki NSSF, Cha kushangaza makato yanaendelea mpaka sasa na hatujui kimsingi mkuu anahitaji nini hasa.
Mheshiwa Rais, tunaomba uingilie kati, kwani tunakufahamu na wewe ni msema kweli na mtetezi wa wanyonge.
Mungu akubariki!