Steven mushi mushi
JF-Expert Member
- Jul 25, 2016
- 533
- 741
Ni kijana ambaye ni jirani yetu, sasa huyu kijana huwa anatabia ya kutaniana sana na mama yake mzazi yaani wana ule utani tu wa kawaida wa mama na mtoto. Jana jioni baada ya kutoka shule maana yeye ni mwanafunzi anasoma kidato cha tatu akiwa nyumbani na mama yake wakawa wanataniana kama kawaida yao sasa ndiposa huyu dogo akamtania mama yake kuwa eti kwa jinsi alivyo handsome enzi zake huyu mama kama angekuwepo akamtokea angekataa. Sasa kumbe wakati wanataniana dingi alikuwa ndani na akasikia ile kauli ya dogo aliyemuambia mama akakasirika na akaona Kama ni dharau mtoto kumwambia mama maneno kama yale hata kama walikuwa wanataniana, Baba yake akatoka na kiti na kumpiga nacho mtoto wake lakini kwa bahati mbaya kile kiti kikampiga dogo mguuni na kumtengua mguu na baadaye wakampeleka hoapitali maana kilimuumiza kweli. Sasa huyu dogo leo ndo karuhusiwa kurudi home na analia sana huku akimlaumu sana Baba yake kwa kitendo alichomfanyia ilihali ule ulikuwa tu ni utani na dingi yake naye anasema hakujua Kama kile kiti alichompiga nacho kingemuumiza vile na anadai alikasirishwa na yale maneno ya dogo aliyomwambia mama yake kuwa kwa jinsi alivyo handsome enzi zake angekuwepo akamtokea Kama angekataa. Daah hata kama una utani na wazazi wako wakati mwingine inabidi uwe makini na kauli zako maana wakati mwingine sinawezaleta madhara hata Kama mlikuwa mnataniana
