Tutor B
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 9,025
- 6,617
UHALISIA WA MAISHA YA KILA SIKU
Ukiamka asubuhi na kuwasha taa, ujue shirika la Tanesco wamechukua hela toka kwako.
Ukienda bafuni kuoga ujue Idara ya maji wamechukua hela toka kwako, kiwanda cha sabuni pia wamechua za kwao.
Ukipiga mswaki kwa kutumia dawa – ujue kiwanda cha kutengeneza dawa wamechukua hela toka kwako.
Ukielekea kazini ujue waendesha bodaboda, daladala na makampuni ya mafuta wamechukua hela toka kwako.
Wakati ukiwa ofisini ukajisikia kupata kifungua kinywa ujue mwenye mghahawa / mama ntilie kachukua zake toka kwako … NA MENGINE MENGI.
Hivi hujiulizi ni kwa nini hakuna sehemu ambapo hata wewe unapaswa kuchukua hela pasipo uwepo wako? Njia rahisi ya kuchukua hela zako pasipo wewe kuwepo ni kujiingiza kwenye ujasiriamali. Jenga mazingira ya kupata hata Tshs. 5,000/= pasipo wewe kuwepo mahali pale.
Nikutakie Jumanne njema yenye mafanikio.
Ukiamka asubuhi na kuwasha taa, ujue shirika la Tanesco wamechukua hela toka kwako.
Ukienda bafuni kuoga ujue Idara ya maji wamechukua hela toka kwako, kiwanda cha sabuni pia wamechua za kwao.
Ukipiga mswaki kwa kutumia dawa – ujue kiwanda cha kutengeneza dawa wamechukua hela toka kwako.
Ukielekea kazini ujue waendesha bodaboda, daladala na makampuni ya mafuta wamechukua hela toka kwako.
Wakati ukiwa ofisini ukajisikia kupata kifungua kinywa ujue mwenye mghahawa / mama ntilie kachukua zake toka kwako … NA MENGINE MENGI.
Hivi hujiulizi ni kwa nini hakuna sehemu ambapo hata wewe unapaswa kuchukua hela pasipo uwepo wako? Njia rahisi ya kuchukua hela zako pasipo wewe kuwepo ni kujiingiza kwenye ujasiriamali. Jenga mazingira ya kupata hata Tshs. 5,000/= pasipo wewe kuwepo mahali pale.
Nikutakie Jumanne njema yenye mafanikio.