Ugumu wa kupata scholarships

Ugumu wa kupata scholarships

ESPRESSO COFFEE

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2014
Posts
6,146
Reaction score
7,683
Wakuu Habari

Leo nimeona nije na ushauri kidogo kuhusu Watanzania wanaotafuta scholarship za kwenda kusoma nje ya nchi au ndani ya nchi.

Nianze kwa kusema tu kupata scholarship ni bahati kama Ilivyo bahati ya kubet. Sio kwamba unajua hapana ila ni Mungu anakuwa amekupangia.

Hivyo hivyo kwenye kupata scholarship. Kwa sasa Tanzania kumekuwa na wimbi kubwa la vijana wanaotafuta scholarship wakihisi ni kitu rahisi rahisi tuu. Wengine wamejikuta wanatumia pesa nyingi sana kutafuta scholarship bila mafanikio, Wengine wamediriki hadi kuingia mkenge kwa kufanya tendo la ndoa na wale wanaojiita msaada wa kutafuta scholarship mwisho wa siku wanatoswa.

Watanzania tuwe wa kweli usimwambie mtu kuwa kupata scholarship ni kitu rahisi rahisi tu hapana.

Wakati unamshauri mtu kuomba scholarship mwambie na ugumu wa kupata Scholarship. Wakati upo Form 4 watakwambia Scholarship za Diploma/Degree nje ya Tanzania ni easy tu kupata,

Unamaliza Form 4 unahangaika unatumia pesa nyingi mwisho wa siku unakosa, unaenda Form 6, Degree/Diploma, baadae Masters mwisho wa siku unajikuta umetumia zaidi ya 10M katika kutafuta kwako Scholarship bila mafanikio.

Kuwa Makini na hizi Scholarship za kwenye mitandao. Saa hizi utaambiwa umepata scholarship 50%, 50% unajitegemea kumbe ni uongo unakuta hiyo 50% ni karibia Million 30/20 wizi umekuwa mkubwa sana.

Na hasa wajinga ndio waliwao! Kuwa makini na Scholarship unazopata nusu nusu, kuwa makini wakati wa kuomba scholarship.

Scholarship kuomba huhitaji hata kulipia senti ili upate Scholarship kuwa makini. Ni bora ukaamini zile zinazotangazwa na Serikali ila ukipata ni vizuri ukaauliza kwa waliopita ukajua maana Serikali nayo imekuwa ikiwaingiza mkeng watoto wa kitanzania unaambiwa umepata Scholarship ukienda huko mambo yanakuwa magumu sana.

Kupata kwenyewee ni kwa kindugu. Hakuna kitu kinacho nikera kama matangazo ya GLOBAL EDUCATION LINK na mengine ya aina hiyo, yamejaaa wizi sana kwa Watanzania na huwa ninashangaa kuona Serikali bado inawaachia waendelee kuwepo.

Kikubwa tuwe makini na hizi Scholarship uchwara. Dunia imebadilika sana utoaji wa Scholarship miaka hii sio sawa na zamani. Wazungu wamesthuka na wamebadilika sana.

Maisha sio kama zamani kwa sababu uongo umekuwa mwingi. Zamani asilimia kubwa ya vituo vya watoto yatima wazungu walikuwa wanafadhi ila kwa sasa wamebadilika kwa sababu ya uongo hii ipo hadi kwenye Scholarship za shule.

Hasa huko China na nchi zingine kuweni makini msije mkaingia mkenge mkajuta baadae. Amini usiamini elimu ya Tanzania sio mbaya kama unavyofikiria wala usidanganywe kuwa kusoma nje ndio kupata ajira. Tukomae hapa hapa bongo tutatoboa.

Yapo mengi sana kuhusu Scholarship mengine tutapata kupitia comment za watu.

Tupendane kwa kuambiana ukweli. Maisha sio rahisi kama tunavyofikiria.
 
Ngoja niwahi kiti, nahitaji nipate elimu ya ziada juu ya hizi scholarships
 
danya,

Scholarship unaambiwa utoe dola 2200 ili wakutafutie chuo. Mmmh hawa ni mawakala kabisa alafu chuo unachotafutiwa wala boom hupewi yaani unaenda kujilipia tena sasa hiyo ni scholarship gani watanzania walio wengi ni zaidi ya wajinga.
 
Nakazia: kusoma nje China, India, Malaysia kwa ada kubwa alafu unarudi bongo kulipwa mshahara laki 5 kwa mwezi au kufungua duka/salon ni uzwazwa.
 
Ngoja nifuatilie wengine huwa wanapataje.
 
danya,

Scholarship unaambiwa utoe dola 2200 ili wakutafutie chuo. Mmmh hawa ni mawakala kabisa alafu chuo unachotafutiwa wala boom hupewi yaani unaenda kujilipia tena sasa hiyo ni scholarship gani watanzania walio wengi ni zaidi ya wajinga.

Scholarship Nyingizi ni Wizi Mkubwaaaa,Hasa Kwa Wale wavivu Wa Kufikiri! Barua Nyingi za Scholarship Zinatengenezwa hapa Bongo! Dola 2200 ungesoma Bongoo Fresh Tuuu! Kuna Dada Namfahamu Aliliwa kiboga na hawa wanaojiita mawakala wa kupata scholarship China! Aliletewa barua Kuwa Amepata Scholarship ila atatakiwa kuongeza Kiasi cha Hela cha Ada na malazi na Ticket anajitegemea ukipiga hesabu kiasi anacho takiwa kulipa yeye ndio ada halisi ya hicho chuo! Kapigaa changa la macho eti umepata Scholarship asilimia 50% wakati hamna unafuu wowote ada ndio Ile Ile! Watanzania Tuwe makini.
 
Nakazia: kusoma nje China, India, Malaysia kwa ada kubwa alafu unarudi bongo kulipwa mshahara laki 5 kwa mwezi au kufungua duka/salon ni uzwazwa.

[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] Ni muhimu Sana Kama Ukibahatika Mzazi Akakupeleka Chuo chochote Nje ya Nchi Ni Vyema Ukaangalia Fursa Gani zinapatikana Huko ili ukimaliza Ubaki hukoo kwa muda wakati unajipanga kuja Kufanya Mashambulizi Bongo! China,India na Malaysia ni kati ya nchi ambazo zinawafanya Vibaya Wabongo kwenye Upande wa Elimu! Kuna Dada Daktari Kasoma Malaysia Kaja Bongo Analipwa Laki 8 na hana Ujuzi wowote!
 
Ni posti ya zamani, lakini si mbaya kuchangia!
Kubwa kwanza la kueleweka ni kuwa 'scholarships' si utapeli ama wizi kama tunavyotaka wengine wafahamu. Jambo lingine la kufahamu ni kuwa hakuna sehemu yeyote ambayo usipokuwa makini utajikuta unadondokea kwa 'wajuaji' na kulizwa. na hivyo ndivyo kwenye utafutaji wa 'scholarships'. Ukiona umelizwa kwenye kutafuta 'scholarships' ni heri ufute mawazo ya kusoma nje kwa 'scholarships', maana ni wazi unakuwa umedhihirisha kuwa utashi wako ni mdogo sana. 'Scholarships' zipo nyingi sana ambazo zinakuhitaji wewe mwenyewe kusoma maelezo na kutuma maombi. Unapotapeliwa maana yake hata kujishughulisha kuzisoma hutaki, unataka umuwachie mtu mwingine akufanyie kazi, hapo ndipo matepeli wanawatafuna.
Lakini jambo lingine, ni kweli 'scholarships' zinapatikana kwa ushindani sana, hasa miaka ya hivi sasa ukilinganisha na zamani. Hii lakini haimaniishi kuwa kuzipata ni bahati, si kweli, bali ni namna vile unavyoweza weka makarabrasha yako ama kutumia vyema usaili unaofanyiwa kuwashinda wengine. Na hapa pia ndipo Wabongo tunachemka, sisi mara nyingi mawazo ya kusoma nje kwa 'scholarships' yanatujia tunapokumbwa na kitu (mf. kazini hakuendi vyema, unasema nitafute tu shule nje niende; kuna rafiki yako umemtamania nawe unakuja tu na wazo la harakaharaka na mimi niende nje). Hii si rahisi kupata 'scholarships'. Upatikanaji wa 'scholarships' unahitaji 'commitment' hasa ya kutaka kusoma, kwa maana unaweza tuma maombi mara nyngi sana na kukosa. Kama ilivyo biashara, unavyokosa ndivyo unakuwa umeijua zaidi 'scholarships', mfano muda wa kufunguliwa, muda wa mwisho wa maombi, mahitaji yake, nk. Awamu ijayo unakuwa na maaandalizi mema zaidi ya mwanzo. Maana yake kama ulishawahi kuomba na kukosa 'scholarships' nyingi, unajikuta una "profiles' la kutosha kucheza nalo kwa awamu zinazofuata. Hii ndiyo sababu mwanzo nimesema inahitaji 'commitment', ukikurupuka tu unataka kusoma kisa ofisini umezinguana na bosi (unataka kumkimbia kwa muda), njia ya 'scholarships' haikufai.
Hitimisho: Tunapeana uzoefu tu, linapokuja suala la kuamini kila mmoja ana haki ya kuamini vile anavyoona ni sahihi.
 
Back
Top Bottom