Ugonjwa wa Pumu (Bronchial Asthma): Chanzo, dalili na tiba

Yupo dr anatibu pumu kama kumsukuma mlevi nina ushahidi wa watu kibao waliopona mfano mwl wangu amepona kabisa mwingine ni meja jeneral samuel kitundu.
 
Nini maana ya Pumu?

Pumu ni hali ambayo huathiri njia za hewa, njia hizi za hewa pia huitwa mirija ya kupumulia. Mirija hii huanzia kwenye njia ya hewa(trachea) hadi kwenye mapafu.

Mchakato wa kupumua kwa watoto walio wengi ni rahisi : Watoto huingiza hewa kupitia puani au mdomoni na hewa huingia kwenye njia ya hewa(trachea) na kuelekea kwenye mapafu. Lakini Kwa watoto wenye pumu, hupumua Kwa shida Kwa sababu njia ya hewa hushindwa kupitisha hewa kwa sababu ya njia yao kuwa imehathiriwa na hali ya pumu.

Shambulio la pumu (Asthma attack) ni nini?


Hii ni hali ambayo hutokea wakati njia ya hewa inapo vimba na kuwa nyembamba na inakuwa vigumu kwa hewa kuingia na kutoka kwenye mapafu. Wakati mwingine njia za hewa zinapokuwa zimevimba hutoa majimaji mfano wa makamasi, hali ambayo husababisha mchakato mzima wa mabadlishano ya hewa katika mapafu kuwa mgumu na hii hali ndo inapelekea tatizo zima la mtotoanapo patwa na pumu kushindwa kupumua vizuri.

Wakati ugonjwa huu unaanza, upumuaji kwa mtoto unaweza kuwa wa kawaida na kuonekana kama vile hakuna tatizo, Lakini kipindi ugonjwa unapoanza, unaweza kuhisi kwamba mtu anapumua kupitia kwenye mrija. Mtoto mwenye pumu anaweza kutoa mlio kama wa filimbi (anapopumua), kukohoa, na kusikia kifua kubana.

Wakati shambulio la ugonjwa wa pumu(asthma attack), hali inaweza kuwa mbaya zaidi kama mtoto hatatumia dawa sahii za pumu. Baada ya kutumia dawa na kupata matibau sahii wakati wa shambulio la ugonjwa wa pumu, njia ya hewa mara nyingi hurudia hali yake ya kawaida, ingawa inaweza kuchukua muda mrefu kidogo wakati mwingine.

Pumu huwapata watu gani?

Pumu ni ugonjwa ambao huwapata watu wengi zaidi ya unavyo weza kufikiri.Karibia watoto milioni sita nchini marekani wanaumwa ugonjwa wa pumu(Hatujui hapa kwetu Tanzania ni idadi gani?).Ugonjwa wa pumu humpata mtoto mmoja hadi wawili katika kila watoto 10 kwa marekani. Hii ina maana kwamba kama una watoto 20 darasani, watoto 2-4 kati yao wanaweza kuwa na ugonjwa wa pumu. Ugonjwa wa pumu unaweza kumshika mtu katika umri wowote- kuanzia mtoto mchanga hadi mtu mzima-lakini huwashika zaidi watoto wenye umri wa kwenda shule(kuanzia miaka sita na kuendelea)

Hakuna anayejua kwa uhakika kwa nini ugonjwa huu unampata mtu mmoja na kuacha mwingine, lakini tunajua kwamba ugonjwa wa pumu unatokea ndani ya familia zetu. Hii ina maana kwamba kama mtoto ana pumu, yeye pia anaweza kuwa na mzazi, ndugu, mjomba au jamaa mwingine mwenye pumu au alikuwa na ugonjwa huu wakati bado mtoto.

Ugonjwa wa pumu unapoanza,huonyesha kama vile ni mafua,ambayo huambatana na kikohozi chenye kutoa mlio wa filimbi,lakini ugonjwa wa pumu siyo wa kuambukizwa. Huwezi kuambukizwa Kama unavyopata mafua

Ni sababbu zipi zinazopelekea Kupata shambulio la ugonjwa wa pumu (Asthma attack)?

Visababishi hutofautiana kutoka mtoto mmoja hadi mwingine. Sababu zipo nyingi.Baadhi ya watoto huwa na mzio(allergy), kwa vile vitu ambavyo huathiri njia ya hewa. Mara nyingi vitu vinavyoleta mzio kwa watoto wenye pumu ni vijidudu vidogo jamii ya mchwa vinavyopatikana kwenye vumbi, harufu mbaya (kama ulikuwa karibu na dimbwi na kuvuta harufu hiyo), mbelewele(pollen) kutoka mitini, majani na kwenye magugu.

Watoto wengi hupata shambulio la pumu wanapokuwa karibu na wanyama wenye manyoya kama Paka na mbwa,baadhi watoto wanapovuta hewa iliyochanganyika na chembechembe za manyoya hawa wanaweza pata shambulio la pumu.

Visababishi vingine ni pamoja na marashi(perfumes), vumbi la chaki, na uvutaji wa sigara. Uvutaji wa sigara sio mzuri hasa kwa mtu mwenye pumu.

Wakati mwingine maambukizi mbalimbali yanaweza kusababisha kulipuka kwa ugonjwa wa pumu,maradhi kama mafua, Kwa baadhi ya watoto, hali ya hewa yenye baridi inaweza kusababisha kulipuka kwa ugonjwa huo,baadhi ya watoto hupatwa na matatizo ya pumu wanapokuwa wanafanya mazoezi,hii ni aina ya pumu inayosababishwa na mazoezi.

Jinsi gani unaweza kutibu ugonjwa wa pumu kwa watoto?


Watoto wenye ugonjwa wa pumu wanatakiwa kujaribu kuepuka visababishi vyote vinavyoweza kuwasababishia shambulio la hewa.Ingawa kuna baadhi ya visababishi kama vumbi la chaki ni vigumu kuviepuka katika mzaizngira yetu hasa shuleni,lakini mtoto,wazazi na walimu wajaribu kuwasaidia watoto wenye matatizo haya.

Sura ya ugonjwa wa pumu hutofautiana kutoka kwa mtoto mmoja hadi mwingine, hivyo kuna dawa mbalimbali za kutibu ugonjwa wa pumu,na matibabu haya hutofautiana kati ya mtoto mmoja na mwingine hii ni baada yake daktari kujaribu kufuatilia sababu zilizopelekea ugonjwa huo, ni kwa kasi gani ugonjwa umetokea, na kiwango cha madhara ya ugonjwa huo. Hapo ndipo ataamua tiba ipi itakuwa sahii na bora kwa mtoto.

Baadhi ya watoto wanatakiwa wameze dawa za pumu mara kwa mara punde wanapopata ugonjwa huu. Hii huitwa dawa ya dharura kwa sababu hufanya kazi ya kufungua njia ya hewa ili mtu aweze kupumua. Watoto wengine wanatakiwa kutumia dawa za kudhibiti ugonjwa wa pumu kila siku,Dawa hizi huzuia shambulio la ugonjwa(asthma attack) kutokea.Kwa hiyo matibabu ya Pumu yanatofautina kutoka mtoto mmoja na mwingine.

Kwa watoto walio wengi ugonjwa wa pumu hupona au hupata nafuu wanapokua wakubwa. Baadhi ya madaktari wanadai kwamba hii hutokea kwa sababu, njia ya hewa hupanuka kadri mtoto anavyokua mkubwa. Njia ya hewa inapopanuka, hewa huingia na kutoka kiurahisi

Baadhi ya watu wazima hupata ugonjwa wa pumu, lakini hii haiwasumbui.Wanariadha wengi katika mbio za olimpiki na magwiji wengine wa michezo wanaweza kuendelea na michezo hata wanapokuwa na ugonjwa wa pumu.

UJUMBE WA KUPELEKA NYUMBANI:


Mzazi au mlezi anayeona mtoto mwenye dalili za ugonjwa wa pumu kama nilivyouelezea hapo juu kitu cha kwanza cha kufanya ni kumwaisha Katika kituo chochote cha Afya au Hospitali iliyo karibu nae.

Na kwa wale watoto walikwisha gundulika tayari na ugonjwa huu wa Pumu ni kuhakikisha wanafuta masharti yote ya Matibabu ili kuzuia shambulio la ugonjwa huu.

Mtoto anayejua mapema kwamba kuna vitu vinamletea madhara katika njia ya hewa au sababu nyingine anaweza kutumia dawa mapema zitakazosaidia kufanya njia ya hewa iendelee kuwa wazi.Mtoto ambaye hupata pumu anapofanya mazoezi anaweza kutumia dawa kabla ya kufanya mazoezi ili waweze kumaliza mbio au michezo vizuri.

Kwa watoto walio wengi ugonjwa wa pumu hupona au hupata nafuu wanapokua wakubwa. Baadhi ya madaktari wanadai kwamba hii hutokea kwa sababu, njia ya hewa hupanuka kadri mtoto anavyokua mkubwa. Njia ya hewa inapopanuka, hewa huingia na kutoka kiurahisi

Baadhi ya watu wazima hupata ugonjwa wa pumu, lakini hii haiwasumbui.Wanariadha wengi katika mbio za olimpiki na magwiji wengine wa michezo wanaweza kuendelea na michezo hata wanapokuwa na ugonjwa wa pumu.
 
MziziMkavu kwa kua pumu hutokana na ufinyu wa njia ya hewa kwa kiswahili rahisi basi mgojwa yyte wa pumu akizoezwa michezo from utotoni anaweza kupona kabisa. moja wapo ya aina za michezo ni ile inayoinvolve sprinting like football na kukimbia hasa marathon hii ni kwasababu mwanamichezo b4 anything atajenga uwezo wa kutanua kifua kisha kujaza hewa so with time utakuta alveoli zinatanuka na kumudu kuingia hewa nyingi.

athmatic patients hawatakiwi kufanya michezo au sanaa ambayo inawasubject kwenye chocking materials kam vile uana mitindo, pia kuogelea unless awe ana mtu pembeni wa kumuobserve vinginevyo huwa wanashauriwa wanaoppenda swimming basi wawe ni wale ambao ni sprinters yaani wakimbiaji vinginevyo watakufa ndani ya mji. michezo ya kwenye mabarafu kwao haitakiwi kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Wanajanvi,

mzee wangu, anasabuliwa na kukohoa kikohozi kikavu hasa wakati wa baridi.ninaomba ushauri wapi naweza kupata dawa ya tatizo hilo.dawa yenyewe ni ipi. Asanteni sana
 
Dawa ya Maradhi
PUMU (ASTHMA): Haya ni maradhi ambayo husibu mapafu na kumsababisha mgonjwa apate shida ya kupumua. SABABU: Yawezekana kusababishwa na vumbi, aina ya unga au vumbi litokanalo na maua, baadhi ya vyakula, mabadiliko ya hali ya hewa, wanyama kama paka na mbwa, aina ya bacteria, kuvuta sigara, pumu ya kurithi. n.k.

DALILI: (3) Mgonjwa hupata shida ya kupumua ndani


hewa safi ya oksijeni na kupumua nje hewa chafu ya kabondayoksaidi.

(4) Wakati mwingine utamsikia mgonjwa akipumua anatoa sauti isiyokua ya kawaida (wheezing sound) hii ni kwa sababu ya wingi wa makohozi (mafua) yaliyosongamana ndani ya mapafu na kuzuia nafasi ya hewa. Mgonjwa hupata shida anapokua ndani ya chumba ambacho ndani yake hakuna hewa ya kutosha kwa sababu ya udogo au upungufu wa madirisha. Mgonjwa hupata nafuu baada ya kutoa na kutema makohozi na kukaa sehemu yenye hewa safi.




(5) Kukohoa au kikohozi cha muda mrefu. TIBA: Kanuni ya kwanza: Chukua bakuli yenye maji ya moto kisha udondoshee ndani yake matone kadhaa ya mafuta ya habatsoda. Kaa juu ya kiti halafu ujifunike shuka na usogeze bakuli lenye maji ya moto na


habat soda ili upate mvuke wake. Tiba hii inaitwa Aromatherapy. Baada ya kufanya hivyo jipake mafuta ya habat soda mgongoni na kifuani halafu unywe mafuta ya habat soda matone matatu. Tumia kanuni hii kutwa mara mbili asubuhi na

jioni kwa muda wa wiki mbili. Kanuni ya pili: Chukua asali nusu lita, juisi ya kitunguu saumu mili lita 200, unga wa habat soda vijiko vinne vikubwa, unga wa tangawizi vijiko viwili vikubwa, unga wa mdalasini kijiko kimoja kikubwa. Vyote changanya pamoja. Kula vijiko viwili vikubwa kutwa mara tatu.
 
Dawa ya Maradhi
PUMU (ASTHMA): Haya ni maradhi ambayo husibu mapafu na kumsababisha mgonjwa apate shida ya kupumua. SABABU: Yawezekana kusababishwa na vumbi, aina ya unga au vumbi litokanalo na maua, baadhi ya vyakula, mabadiliko ya hali ya hewa, wanyama kama paka na mbwa, aina ya bacteria, kuvuta sigara, pumu ya kurithi. n.k.

DALILI: (3) Mgonjwa hupata shida ya kupumua ndani


hewa safi ya oksijeni na kupumua nje hewa chafu ya kabondayoksaidi.

(4) Wakati mwingine utamsikia mgonjwa akipumua anatoa sauti isiyokua ya kawaida (wheezing sound) hii ni kwa sababu ya wingi wa makohozi (mafua) yaliyosongamana ndani ya mapafu na kuzuia nafasi ya hewa. Mgonjwa hupata shida anapokua ndani ya chumba ambacho ndani yake hakuna hewa ya kutosha kwa sababu ya udogo au upungufu wa madirisha. Mgonjwa hupata nafuu baada ya kutoa na kutema makohozi na kukaa sehemu yenye hewa safi.




(5) Kukohoa au kikohozi cha muda mrefu. TIBA: Kanuni ya kwanza: Chukua bakuli yenye maji ya moto kisha udondoshee ndani yake matone kadhaa ya mafuta ya habatsoda. Kaa juu ya kiti halafu ujifunike shuka na usogeze bakuli lenye maji ya moto na


habat soda ili upate mvuke wake. Tiba hii inaitwa Aromatherapy. Baada ya kufanya hivyo jipake mafuta ya habat soda mgongoni na kifuani halafu unywe mafuta ya habat soda matone matatu. Tumia kanuni hii kutwa mara mbili asubuhi na

jioni kwa muda wa wiki mbili. Kanuni ya pili: Chukua asali nusu lita, juisi ya kitunguu saumu mili lita 200, unga wa habat soda vijiko vinne vikubwa, unga wa tangawizi vijiko viwili vikubwa, unga wa mdalasini kijiko kimoja kikubwa. Vyote changanya pamoja. Kula vijiko viwili vikubwa kutwa mara tatu.

Hiyo dawa unayosema ndio utapona moja kwa moja au utapata nafuu? Nimekwisha kutumia habatsoda, vitunguu maji, asali na still kipumu kinaniandama! I dont think kama kuna dawa ya kuponya haya maradhi bali ipo tu ya kukupa afueni.

Kama ipo ata namie naitaka! Ila situmii za kienyeji coz i dont trust them
 
Kama wewe Huamini Dawa za Kienyeji Nenda hospitali watakupatia Dawa ya Pumu usiulize hapa Dawa ya Pumu wakati hospitali zipo nenda ukatibiwe Hospitalini... chilubi

Mzizimkavu,
Vema,yeye kama haamini anategemea kupona kwa dawa zipi? kama ni za Hospitali si aende huko? Aache kabisa kutuchanganya wakati dawa za asili ndiyo zinatutibu.

Mimi binafsi nina matatizo ya seasonal Athma na ilikuwa ikinisumbua sana,LKN sasa ni miezi 8 hivi na hata Athma haijawahi kunisumbua sasa. Na dawa pekee ninayotumia ni ASALI. Ninatumia asali kwenye chai kila siku na pia kila siku usiku kabla ya kulala nakula kijiko 1 cha asali.Na kwasababu kwa kipindi chote hiki na hata dawa nilizopewa Aghakan sijatumia yapata miezi 8 sasa. Hivyo, naamini dawa za asili zinasaidia. Mimi naamini ASALI ndiyo imekuwa ikinisaidia kwa kipindi chote hiki. Na kuhusu ASALI nilipata humu humu JF, hivyo kama kuna mtu ambaye haamini atuache sisi wengine tunaoamini na tayari nimeona matunda ya dawa za asili na JF:

NB: Mzizimkavu na wengineo, kamwe msikatishwe tamaa na wale wasioamini, kwani tulio wengi tunaheshimu sana michango yenu na Mungu azidi kuwabiriki.
 
Mzizimkavu,
Vema,yeye kama haamini anategemea kupona kwa dawa zipi? kama ni za Hospitali si aende huko? Aache kabisa kutuchanganya wakati dawa za asili ndiyo zinatutibu.

Mimi binafsi nina matatizo ya seasonal Athma na ilikuwa ikinisumbua sana,LKN sasa ni miezi 8 hivi na hata Athma haijawahi kunisumbua sasa. Na dawa pekee ninayotumia ni ASALI. Ninatumia asali kwenye chai kila siku na pia kila siku usiku kabla ya kulala nakula kijiko 1 cha asali.Na kwasababu kwa kipindi chote hiki na hata dawa nilizopewa Aghakan sijatumia yapata miezi 8 sasa. Hivyo, naamini dawa za asili zinasaidia. Mimi naamini ASALI ndiyo imekuwa ikinisaidia kwa kipindi chote hiki. Na kuhusu ASALI nilipata humu humu JF, hivyo kama kuna mtu ambaye haamini atuache sisi wengine tunaoamini na tayari nimeona matunda ya dawa za asili na JF:

NB: Mzizimkavu na wengineo, kamwe msikatishwe tamaa na wale wasioamini, kwani tulio wengi tunaheshimu sana michango yenu na Mungu azidi kuwabiriki.
Mkuu. TELO wewe endelea tu kutumia hiyo Asali itazidi kukusaidia nakupa na faida ya hiyo Asali kila siku unapo amka kabla kula kitu chemchsamaji ya uvuguvugu glasi moja kisha tiya ndani yake kijiko kimoja kikubwa cha Asali kunywa kila siku asubuhi kabla hujala kitu itakusaidia kuondowa maradhi hayo ya Pumu tumia kila siku katika Maisha yako muache huyo chilubi na ujinga wake anazarau Dawa za mitishamba.
 
Last edited by a moderator:
Kuna majani yanaitwa Athma weeds, au Euphorbia hirta, au mziwaziwa, google utaona picha yake then utaumbua kwani ni very common weed!

Kausha pamoja na majani ya mpapai; sokota then smoke. Ukishindwa basi choma chumbani unapolala!

Inarelieve, sina uhakika inaponya kabisa!
 
Kuna majani yanaitwa Athma weeds, au Euphorbia hirta, au mziwaziwa, google utaona picha yake then utaumbua kwani ni very common weed!

Kausha pamoja na majani ya mpapai; sokota then smoke. Ukishindwa basi choma chumbani unapolala!

Inarelieve, sina uhakika inaponya kabisa!
astma huwa haiponi? cha muhimu ni kuepuka vitu vinavyoweza kuiprecipitate ikaanza kama vile vumbi na poleni(chavuo) dawa nyingi za asili kama kujifukiza au kunusa majani ya mkaratusi inasaidia. lakini kwa mtoa mada kukohoa haiconclude kwamba ni astma
 
ooh! nimesahau asthma ikiwa kali inaweza sababisha kifo dawa ni kuwahi hospitali kupata sindano za epinephrine
 
Pole sana Kimla.

Kitu kingine cha kuachana nacho (kama unatumia) ni alcohol, huwa ina side effect ya ku trigger asthma mara nyingi.Kutegemea na aina ya pombe.
 
aha aha aha kama haamini dawa za kienyeji sijui km za hospitali ndo zinatibu asthma hasa ile ya aleji au ya kurithi sana sana utapewa aminophyline,ventolyne, ephridine nk km hali mbaya utapewa vidone vikali au sindano zake na bado hautapona sana sana ni kusogeza siku....Asthma kuna watu wamepona kabisaa tena hizi za kurithi kwa madawa ya kienyeji cha msingi usikate tamaa kwan madawa ya kienyeji yapo selective huyu yanaponesha yule haponi so hujui wewe ni ipi itakuponesha..mie mwenyewe nikienda BUKOBA tu shughuli yani siku mbili tu kifua kinaanza yani silali kabisa kinabana na pia nakohoa na hiyo ni coz BK ni baridi sana na hali ya kule ni ya wingu zito lakini nikiondoka BK hua sijui km na asthma kwani nakua mzima kabisa
 
Asanteni kwa michango.Je hawa Arusha herbalist wanasema wanadawa ya kutapisha na unapona kabisa.Je kunamtu aliisha wahi kuzitumia atusaidie kujua efficiency yake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom