Sakata la Ugomvi baina ya RC Gambo na Mkurugenzi wa Jiji Arusha lashika kasi

buswelu moja

JF-Expert Member
Aug 24, 2014
226
147
Ugomvi, chuki na uhasama baina ya mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na mkurugenzi wa jiji la Arusha, Dkt Madeni unazidi kuchukua sura mpya baada ya Gambo kumwambia kwamba usemaji wake una mipaka na kumwonya awe makini.

Wawili Hawa wana Hali ya kutoelewana huku chanzo kikidaiwa ni kugombea mradi wa ujenzi wa kituo kikuu Cha mabasi ya mikoani jijini Arusha.

Wakati mkuu wa mkoa na timu yake wakipendekeza ujenzi huo ufanyike mahali pengine mkurugenzi naye ameibuka akitaka mradi huo ufanyike sehemu nyingine.

Lakini pia inadaiwa mkurugenzi amekuwa akipingana na maagizo ya Rc Gambo kwa madai kwamba yeye anaripoti moja kwa moja kwa mkuu wa nchi hususani kufuatia nafasi yake akitajwa kwamba ni ofisa mwandamizi wa idara ya usalama wa taifa (TISS).

Katika madai hayo Rc Gambo anahisi Mkurugenzi amekuwa akipenyeza taarifa mbalimbali kwa mkuu wa nchi ili kumharibia kitumbua chake.

Lakini ugomvi huu unazidi kuchukua sura mpya baada ya DC wa Arusha, Gabriel Daqaro kumtabiria Mkurugenzi wa jiji kwamba huenda siku moja akawa mkuu wa mkoa wa Arusha na alitabiri hivi Karibuni alipokuwa akihutubia mkutano wa walimu wa shule za msingi na sekondari wilaya Arusha.

Itakumbukwa ya kwamba Daqaro ni afisa usalama wa taifa na aliwahi kuwa mlinzi wa Rais Magufuli kabla ya kupewa cheo cha ukuu wa wilaya.

Sinema ni ndefu macho na masikio ni yetu tutaendelea kuwajuza.

 
Hii habari imeletwa kiushabiki tu, hakuna bifu yoyote, nimeisikiliza hiyo clip, hakuna bifu bali kuna kukumbushana tu the chain of command.

RC ndie rais wa mkoa!, kila kitu kiko chini yake, hivyo RC yuko right, yeye ndiye mwenye kauli ya mwisho kuhusu jambo lolote la mkoa wake.
P
 
Mh RC amekuwa na tendency ya kugombana na wasaidizi wake na wala sio Dkt Madeni tu itakumbukwa pia aliwahi (bifu bado linaendelea)kuingia kwenye msuguano na DC Daqaro lakini pia na mkurugenzi wa sasa wa tume ya uchaguzi. Naona amemwambukiza na Jerry Muro lakini kiukweli hawajielewi,mkoa wa Arusha Mh Rais anauona kwa jicho la tatu
 
Mkubwa huwa hakosei, kauli ya mwisho ni ya mwisho, the boss is always right. Na ikitokea the boss asiwe sahihi ziko taratibu za kumrekebisha na sio kwa kutofautiana in public.
P

This is almost saying mkubwa ni Mungu kitu ambacho sidhani kama ni sahihi sana. Moja ya matatizo makubwa tuliyonayo kama nchi kwa sasa ni kwa sababu kuna watu wana-amini kwamba wao hawakosei. Wao always wako sahihi which is completely wrong na kwamba wanachosema wao kinapaswa kuwa hivyo hata kama kuna njia nyingine mbadala ambayo huenda ni bora zaidi.

Mambo yamebadilika sana kwa sasa, mfano upatikanaji wa taarifa umebadilika sana na umerahisishwa mno, kuaccess information ni rahisi mno so hata namna ya uongozi inapaswa kubadilika sana. Na kwa uongozi hapa ninamaanisha mpaka ngazi ya familia. Baba kwa mfano, ukitaka kui-bulldose familia kwa kizazi hiki eti kwa sababu tu wewe ni baba ni lazima uchemshe.
 
Hata yeye alimfanyia hivo hivo Ntibenda Kijiko hapo hapo Arudha wakati akiwa DC na kijiko Rc. Wakati Ntibenda akiwa na shughuli huku yeye aliwaita watendaji wote na kuwaambia yeye ndo rc na waende huko.hii nchi kwa sasa haifuati utaratibu inategemeana ukaribu wako na mkuu wa nchi hata mtendaji wa kata anaweza muamuru RC!

Siku si nyingi shule zilichomwa mfululizo Arusha na akatumia vijana wa ccm kusema Ntibenda ameshindwa kuimarisha usalama Arusha, hivi lini RC akalinda shule zidichomwe?

Watu tukiendelea na mshangao tukasikia Ntibenda sio Rc tena.... huyu mkuu tuliyenaye anachangia pakubwa kwenye migogoro ya viongozi
Hii habari imeletwa kiushabiki tuu, hakuna bifu yoyote, nimeisikiliza hiyo clip, hakuna bifu bali kuna kukumbashana tuu the chain of command.

RC ndie rais wa mmoja, kila kitu kiko chini yake, hivyo RC yuko right, yeye ndiye mwenye kauli ya mwisho kuhusu jambo lolote la mkoa wake.
P
 
Power does not make your smart but exposes your ignorance
This is almost saying mkubwa ni Mungu kitu ambacho sidhani kama ni sahihi sana. Moja ya matatizo makubwa tuliyonayo kama nchi kwa sasa ni kwa sababu kuna watu wana-amini kwamba wao hawakosei. Wao always wako sahihi which is completely wrong na kwamba wanachosema wao kinapaswa kuwa hivyo hata kama kuna njia nyingine mbadala ambayo huenda ni bora zaidi.

Mambo yamebadilika sana kwa sasa, mfano upatikanaji wa taarifa umebadilika sana na umerahisishwa mno, kuaccess information ni rahisi mno so hata namna ya uongozi inapaswa kubadilika sana. Na kwa kwa uongozi hapa ninamaanisha mpaka ngazi ya familia. Baba ukitaka kui-bulldose kwa kizazi hili ni lazima uchemshe.
 
Hata yeye alimfanyia hivo hivo Ntibenda Kijiko hapo hapo Arudha wakati akiwa DC na kijiko Rc. Wakati Ntibenda akiwa na shughuli huku yeye aliwaita watendaji wote na kuwaambia yeye ndo rc na waende huko.hii nchi kwa sasa haifuati utaratibu inategemeana ukaribu wako na mkuu wa nchi hata mtendaji wa kata anaweza muamuru RC! Siku si nyingi shule zilichomwa mfululizo Arusha na akatumia vijana wa ccm kusema Ntibenda ameshindwa kuimarisha usalama Arusha, hivi lini RC akalinda shule zidichomwe??? Watu tukiendelea na mshangao tukasikia Ntibenda sio Rc tena.... huyu mkuu tuliyenaye anachangia pakubwa kwenye migogoro ya viongozi

Aliwaambia watendaji wa kata wao ni wawakilishi wake katika maeneo yao, wasibabaishwe na Mkurugenzi wala Mkuu wa wilaya
 
Lakini pia kwa nini watu msiwe mnafanya shughuli zenu na mambo ya watu muyaache?hayo si ya kwao?wengine mnapoteza muda mwingi kuacha kufijiri maisha yenu kwa sababu ya maugomvi ya watu wengine
 
Hii habari imeletwa kiushabiki tuu, hakuna bifu yoyote, nimeisikiliza hiyo clip, hakuna bifu bali kuna kukumbashana tuu the chain of command.

RC ndie rais wa mmoja, kila kitu kiko chini yake, hivyo RC yuko right, yeye ndiye mwenye kauli ya mwisho kuhusu jambo lolote la mkoa wake.
P
We naye huna lolote, tulishakuweka Kapuni baada ya kumumuza Kabendera. Siku tizi unajipendekeza tu kwa watawala.
 
Back
Top Bottom