Akihojiwa na BBC, Waziri wa Afrika Mashariki wa Uganda amesema wataendelea na mipango yao ya kiuchumi licha ya kushutumiwa na baadhi ya watu kuhusu ushirika wao wa siri.
Aidha ameshutumu wote wanaolaumu kutengwa kwa Tanzania na Burundi katika mipango hiyo licha ya nchi hizo kuwa sehemu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki!
Hata hivyo mbuge mmoja wa bunge la Afrika Mashariki kutoka Burundi amesema kuwa si busara kuzitenga Tanzania na Burundi hata kama miradi hiyo haitajengwa katika nchi zao kwa kuwa nazo ni sehemu ya Afrika Mashariki na kwamba wananchi wao wana maslahi kwa namna moja au nyingine!
Nilimsikiliza yule Mbunge wa EAC-Burundi, ni bi Hafsah Mossi, mtangazaji wa zamani wa BBC, anachangia na kutoa maelezo kwa umakini na ueledi wa hali ya juu. Anatumia kugha za hekima sana huyu!