Ugaidi - hivi polisi wameshatoa hata picha ya mtu mmoja anayeshukiwa kwa ugaidi huko pwani?

2kimo

JF-Expert Member
Jan 23, 2014
2,029
2,071
Dunia nzima kabla ya kupambana na magaidi watu huanza kwa kufanya utafiti kujua nguvu ya adui.
  1. Kwanza huanza kwa kutambua jina la kundi kama lipo maana hiyo pia yaweza kuwa Link muhimu kwenye kujua dhamira ya uharifu na msimamo wa kundi.
  2. Kujua dhamira Yao ili waweze kujua ni jambo la kunegotiate, kutolea ufafanuzi au ni typical uharifu wa kupiganwa from the word go
  3. Kujua kiongozi wa kundi na members wengine muhimu
  4. Kujua recruitment procesa ili uweze ku predict speed ya ukuaji wa kundi na uweze kujua pattern ya watu unaowashuku kama wanafaa kupoteza muda kuwafuatilia au uwakamate tu straight
  5. Kujua vyanzo vyao vya mapato na silaha ili uweze kudhibiti supply
  6. Kujua makao yao makuu na machimbo yao mengine ili kuweza kuwadhibiti
Sasa hadi leo hakuna taarifa rasmi juu ya kibiti.
Yawezekana hata waharifu tunapanda nao mbagala wakiwa wanaelekea kazini kibiti lkn sasa hatuwafahamu.
IGP mangu, hebu fanyeni kipindi maalum mtuelezee kuhusu hao majangili tujue angalau hayo tuliyoyasema hapo, naamini wananchi watasaidiana na jeshi lao kuwadhibiti hao waharifu.
Ni vema mkafanya mapema maana kama speed Yao ya kuongeza members ni kubwa itakuja kuwa alshabaab inaundwa nchini na tumeshindwa kuidhibiti
 
Back
Top Bottom