Ufugaji nyuki wa kisasa

kinsakina
Sasa, kabla ya kuweka makilia mpya kwenye mzinga mpia bila kundi la nyuki, si lazima mzinga huo uwe tayari una masega au?
Na kwa Tanzania, hiyo teknolojia ya kuzalisha malikia au makundi ya nyuki iko wapi 'In practice'?
 
Kumbe kazi ngumu aisee. Katika mifugo mingine tunasema kuzalisha kumbe kwenye nyuki ni kudhalisha? Inabidi kujifunza lugha kwanza aisee.
 
Kumbe kazi ngumu aisee. Katika mifugo mingine tunasema kuzalisha kumbe kwenye nyuki ni kudhalisha? Inabidi kujifunza lugha kwanza aisee.

kudhalisha.........hii ni changamoto namba moja kwenye hii ishu..
 
Sidhani kama ni hii mkuu, hawa hornet nadhani wanapatikana huko ulaya na Asia
Halafu wanapovamia wanaua karibia mzinga wote na kuoba asali..hiki ndio kinachotokea kwako?
Dah! mkuu, hii inaweza kuwa jibu labda inahitaji utafiti Zaidi. Hawa nao hutembea kama kundi au mmoja mmoja, na wanakuwa wanatokea wapi? na ni kwa vipi unaweza kuwatambua na kuwadhibiti?
 
Hii ndio inaweza kuwa sababu, labda atuambia kama kuna midawa sana kwenye mazingira
 



 
Tumewai fanya hii ya kuzalisha makundi ya nyuki na pia uzalishaji wa malkia wa nyuki...Ni raisi Tena Sana Kama una vifaa.
Nyuki wanamtengeneza malkia wenyewe na wanaweza tengeneza ata malkia 100 kwenye mzinga mmoja! Kuna vifaa maalumu kwa kazi hii,sisi tuliagiza China kupitia alibaba.kuna Queen cells (za plastic) ambazo unaweka katika mzinga na unachukua mayai alaiyotaga malikia wa nyuki na kuyaweka katika hizi Queen cells.

Nyuki watazitunza hizi Queen cell zenye mayai kwa kulisha chakula special Cha malkia wa nyuki kinachoitwa queen jerry.nyuki wakiona queen cells wao wanalisha chakula Cha kuzalisha malkia aijalishi idadi ya queen cells katika mzinga.unaweza zalisha ata queens 300 au zaidi kwa Mara moja toka mzinga mmoja...ila queen 2 awawezi kaa katika mzinga mmoja...nyuki upiganisha malkia mpaka mmoja afe mmoja abakie....

so kabla malkia awatotolewa inabidi uhamishe hizo queen cells...iwapo Kama unataka kufanya hili zoezi tuwasiliane..na few queen cells za plastics so unaweza jaribu...mwakani 2020 nna mpango wa kuanzisha project ya mizinga 10.000 Morogoro tunajenga queen realing lab ndani ya viwanja vya nane nane...wameshatupatia eneo pale na tulishalipa fees zao.
Cell ya kuzalisha malikia huwa inaangalia chini tufauti na za kuzalisha nyuki wa kawaida..nimeweka picha hapa ili uweze tambua queen cellz
 

Attachments

  • images (6).jpeg
    36 KB · Views: 24
  • images (7).jpeg
    20.2 KB · Views: 20
  • images (8).jpeg
    29.8 KB · Views: 24
  • images (9).jpeg
    12.2 KB · Views: 21
  • images (10).jpeg
    9.8 KB · Views: 22
  • queencellframe.jpg
    12.9 KB · Views: 18
Shukuran sana Mkuu. Tutawasiliana
 
kinsakina
Sasa, kabla ya kuweka makilia mpya kwenye mzinga mpia bila kundi la nyuki, si lazima mzinga huo uwe tayari una masega au?
Na kwa Tanzania, hiyo teknolojia ya kuzalisha malikia au makundi ya nyuki iko wapi 'In practice'?
malikia akishazalishwa anapelekwa kwenye mzinga wenye nyuki wadogo,wakubwa huwa tifu kumkubali malkia ,na kuna utaratibu wa kumuweka mpaka akubalike vinginevyo atauwawa na nyuki ,unapomuweka kwenye mzinga lazima usome saikologia ya nyuki ,unamuweka kwenye cage maalumu yenye wavu,

kisha unaitia ndani ya mzinga,ukiona nyuki wamekuwa na vurugu na wanamzonga kwenye cage ujue kimenuka mtoe hawajamkubali,utaendelea na zoezi hili mpaka nyuki wa react passive,itakupasa kumpakaa malkia asali kutoka kwenye mzinga unaotaka kumuweka ili akubalike kirahisi pale nyuki wanapomkataa,mizinga inapaswa iwekaribu na unapoishi
 
Je naweza kufuga Nyuki kwenye shamba la mikorosho?
Note; Kwenye mikorosho huwa tunapulizia dawa ya salfa, Je haidhuru nyuki? ama kupunguza ubora wa Asali?


Sent using Jamii Forums mobile app
Samahsni sana kwa kchelewa kujibu ujumbe wako. Ningependa kukuambia kua unaweza kufuga nyuki katika mashamba ya mikorosho bila wasiwasi na pia nyuki watasaidia kuchavusha mikorosho yako. Nigependa kujua izo kemikali za salfa huwa mnatumia muda gan na sehemu gan ya mti wa mkorosho.
 
Hapo kwenye nta hapo!! Naweza kushirikiana nanyi na hatimaye kuliongezea zao la asali thamani!! Ningependa nipate mawasiliano na wahitaji wa nta na asali mbichi.. karibuni sana namba yangu ni 0762044550
Karibu sana wasiliana nasi
 
Kwa nini msianzishe soko la asali la ndani na nje ya nchi, na muwe mnanunua kutoka kwa Wafugaji?

Mkatengeneza mfumo mzuri wa kuhakiki ubora wa asali na mkawahakikishia Wanunuaji kwamba wakinunua asali kwenu zina ubora wa asilimia 100%.
Tunashukuru sana kwa ushauri wao tunakaribisha watu wenye mawazo kama yako waweze kutushauri, tutafanyia kazi swala lako.
 
Salama wakuu,

Nimekuwa nikikabiliwa na changamoto ya nyuki kufa kwenye mizinga kwa sababu ambazo sijazielewa mpaka sasa.

Kwa wazoefu wa nyuki, ni mambo gani hasa yanaweza kupelekea nyuki kufa?
View attachment 1286616
Kuna sababu nyingi ambazo huweza kusababisha vifo vya nyuki katika mzinga, moja wako ni uwepo wa matumizi makubwa ya kemikali katika kilimo karibu na mizinga. Lakini pia sababu ni nyingi ambazo lazima uone kwa undanj zaidi. Tungependa kuona picha zaidi. Au wasiliana nasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…