Ufugaji bora wa sungura kwa ajili ya kukuza kipato

BUSHMEN 88

Member
Sep 3, 2022
25
31
Habarini wanajukwaa natumai ni wazima wa afya tele na pia natanguliza shukrani zangu kwenu.

Nimeanzisha mradi wa ufugaji wa sungura ili niweze kukuza kipato na kupambana na changamoto za maisha baada ya kuona ugumu wa maisha kila kukicha kheri ya jana. Hivyo basi niliamua kuanza kufuga na sungura kumi lakini nilifanikiwa kuanza na sungura watano kulingana na mtaji nilikuwa nao wa shilingi laki moja yani nilinunua majike manne na dume moja.

Mradi huu yapata miezi miwili na nusu mpaka sasa hivi lakini sungura majike watatu wamefanikiwa kuzaa jumla ya watoto ishirini na moja yani uwiano wa kila mmoja kuzaa watoto saba.

Sasa naomba nielimishwe nifanyaje ili niweze kuwanusuru kutunza vizuri watoto wasipate na magonjwa, kufa ukizingatia mimi ndio mara ya kwanza naanza kufuga sungura naombeni mchango wenu na ushauri wadau na watalaamu wa ufugaji wasungura.

Ahsanteni.
 
Nafugia kwenye banda lilipo juu chakula nawapa majani makavu na mabichi, pumba yenye mchanganyiko wa mashudu, dagaa, uduvi na chokaa.
 
Pia usiwape majani ya kabeji(kabichi)hasa sungura wadogo,kwani hupelekea sungura kufa..hasa inapotokea kukawa na mabaki ya sumu kwenye hayo majani..japo sio mara nyingi.
 
IMG_20220902_182919_347.jpg

Naombeni kuona picha ya Banda la sungura,wakwangu nimewafuga kienyeji wanachimba chini ndio wanakoishi naona siwatendei haki
 
Watoto wa sungura mara nyingi huanza kufa pale wanapoacha kunyonya, hivyo kuwa makini, pia baridi huwa inawasumbua, kingine usiwachanganye sungura wadogo na wakubwa huwa wanatabia ya kukanyagana, mm mwezi huu nimepoteza watoto 15 wa sungura wenye umri wa mwezi mmoja,
 
Nje ya Mada kidogo:
Tatizo la Sungura kula watoto wake huwa linasbabishwa na nini na nini suluhisho lake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom