Ufisadi wa elimu: Comredi Kainerugaba Msemakweli tunakuhitaji leo kuliko kipindi kile

mitale na midimu

JF-Expert Member
Aug 26, 2015
10,420
17,701
Katika mapambano ya Ufisadi nchini Ufisadi wa Elimu ulikuwa haujulikani kama nao ni ufisadi hadi alipoibuka mpambanaji huyu na kutanua maana ya ufisadi katika kimo, urefu na upana wake.


Kama bado upo,
Natamani utuletee Kitabu kipya kinachochambua elimu za wabunge,mawaziri na watu mashuhuri nchini ili kuwa kichocheo cha zoezi la uhakiki kwa wahakiki. Faida yake, Utakuwa umetusaidia wananchi kupambana na watuhumiwa, wajeruhiwa wa maamuzi ya serikali, watu wenye ugomvi binafsi, watu wasio na nia nzuri na taifa letu, wanamitandao maarufu ambao wenda wameweka akiba ufisadi huu wa elimu ili wautumie wakati wao watakapohitajika kueleza mienendo yao yenye mashaka.
Mfano sasa mada moto ni uhalali wa elimu au vyeti vya mkuu wa mkoa. Waanzilishi ni walewale ambao nao wanahitajika kusaidia dola katika majanga ya madawa. Vita vyako vile vingeanza mwanzoni mwa utawala huu wenda leo tusingekuwa tunajadili elimu za watu bali vitu vikubwa zaidi vyenye kulisaida taifa zaidi.

Ifikie hatua wale vijana waliowahi kuongoza taifa zima (TANZANIA ONES) kielimu iwe chuo au sekondari ndio wawe kwenye sehemu kubwa za wafanya maamuzi ya sisi wananchi tulio wengi huku vijijini.

Kutoka maktaba za JF
Kijitabu Cha Orodha ya mafisadi wa Elimu TANZANIA CHAGOMBEWA SOKONI
 
Katika mapambano ya Ufisadi nchini Ufisadi wa Elimu ulikuwa haujulikani kama nao ni ufisadi hadi alipoibuka mpambanaji huyu na kutanua maana ya ufisadi katika kimo, urefu na upana wake.


Kama bado upo,
Natamani utuletee Kitabu kipya kinachochambua elimu za wabunge,mawaziri na watu mashuhuri nchini ili kuwa kichocheo cha zoezi la uhakiki kwa wahakiki. Faida yake, Utakuwa umetusaidia wananchi kupambana na watuhumiwa, wajeruhiwa wa maamuzi ya serikali, watu wenye ugomvi binafsi, watu wasio na nia nzuri na taifa letu, wanamitandao maarufu ambao wenda wameweka akiba ufisadi huu wa elimu ili wautumie wakati wao watakapohitajika kueleza mienendo yao yenye mashaka.
Mfano sasa mada moto ni uhalali wa elimu au vyeti vya mkuu wa mkoa. Waanzilishi ni walewale ambao nao wanahitajika kusaidia dola katika majanga ya madawa. Vita vyako vile vingeanza mwanzoni mwa utawala huu wenda leo tusingekuwa tunajadili elimu za watu bali vitu vikubwa zaidi vyenye kulisaida taifa zaidi.

Ifikie hatua wale vijana waliowahi kuongoza taifa zima (TANZANIA ONES) kielimu iwe chuo au sekondari ndio wawe kwenye sehemu kubwa za wafanya maamuzi ya sisi wananchi tulio wengi huku vijijini.

Kutoka maktaba za JF
Kijitabu Cha Orodha ya mafisadi wa Elimu TANZANIA CHAGOMBEWA SOKONI
Msema kweli aongeze orodha mpya, mafisadi wa elimu wameongezeka.
Uhakiki wa vyeti na elimu ufanywe kwa viongozi kusiwe na dubble standard.
Wasihakikiwe wengine na wengine wanaachwa!!
NECTA na Waziri Mhs Ndarichako tusaidie!!
 
Kinacho nsikitisha katika suala hili la ufisadi wa elimu Ni kwamba Mafisadi wenyewe wamepewa ring la kuhakiki vyeti Feki kwa hiyo zoezi hili kufanikiwa had kuona safari ndefu.
 
Back
Top Bottom