Ngisibara
JF-Expert Member
- Jan 2, 2009
- 3,298
- 2,074
Hadi watu flani wafe labda ndiyo serikali iamke. Suala kama hili lilizuka mwishoni mwa miaka ya 1990 pale ambapo ndugu watatu wa jamii ya Kihindi (waliokuwa wakimiliki kampuni moja ya Clearing and Forwarding -- Dewlo Brothers) walipowaua wafanyakazi wao wawili wa Kiafrika (na baadaye kuwachoma moto) ili kuwaziba midomo wasije wakatoa kwa vyombo husika habari za ufisadi wao wa ukwepaji kodi -- kama huu huu wa hawa jamaa wa Kiarabu.
Ingawa Wahindi wao walikamatwa, na kufunguliwa kesi ya mauaji, walikuja shinda kesi baada ya kukaa takriban miaka 5 rumande. Kushinda kwao kesi bila shaka kulitokana na nguvu za pesa walizokuwa nazo walizotoa kwa waendesha mashitaka ambao waliivurunda kesi hadi yule Jaji aliyewaachia kutamka kwamba charge sheet na ushahidi uliowasilishwa na waendesha mashitaka ulikuwa ni aibu tupu!
Nadhani twaiona sasa historia ikijirudia, na nahofia huenda kuna watu watakufa.
Asante sana Zak kwani nilikuwa nahamu sana kujua kesi ile iliishaje, kumbe ni vilevile anyway mungu yu nasi..