Ufisadi NHIF

Tumesikia ya ATCL makubwa na yanayohatarisha maisha ya watu , hakuna hata mkuu mmoja wa serikali aliyesimama kidete na kuisafisha manejiment au kuikemea ...

Tumesikia ya Benki ya Posta juu ya ubadhirifu na JINAI ya kughushi laikini hakuna hata kiongozi si wa shirika lenyewe,wizara au kiongozi wa ngazi za juu hata za kati kuwasafisha watendaji au kuwauliza ili watoe majibu...Imeongezeka tena ya kuwa Benki ya Posta imetumia zaidi ya DOLA za kimarekani Thelathini na tano elfu (35,000.00) karibu shillingi millioni arobaini na tatu kumpeleka india kwa ajiri ya kuchunguzwa afya makamu mwenyekiti wa BODI ambaye si mtendaji wala si mwajiriwa wa benki ya posta... Akiongozana na MKEWE pamoja na Nurse wote wakilipiwa kwa wiki mbili...hata kujiuliza kazi ya nurse kutoka Tanzania itakuwa ni ipi na kazi ya mke itakuwa ni ipi... KIMYA KIMYA serikali kama haipo...
na mengine mengi mengi... wako kimya kabisa kama hawaoni wala kusikia

Haya ya Bima ya afya yameibuka...nafikiri tuanze kupima IQ za wanaoomba uongozi Tanzania,si dhani kama viongozi wetu wengi wanao uwezo mzuri wa kufikiri bila kuwategemea washauri
 
Karibu Afisa Usalama katika Jf,

Usishangaa sana sababu hata Maafisa wa Usalama wanajua hili,Ndiyo Hata Mwanakijiji alishawahi kuhoji je kuna ulazima wa TISS kuendelea kuwapo kama kuna mambo kama haya yanaendelea na wao bado wanaangalia.Tatizo ni Mkurugenzi au?
 
Nimesoma hii story nikasema Mungu ibariki Tanzania. Hapa nimechoka mwenyewe. Kwanza NHIF staff asante sana kwa kuleta hii habari hapa JF, tutajaribu kadi tuwezavyo kuisimamia katika koo.

Invinsible naomba hili swala kama inawezekana liwe sticky on top. Nadhani hili swala linausu familia nyingi Tanzania, hili swala linawagusa walimu wa msingi na sekondari ambao wanalisha knowledge kwa vijana wetu.

Kwanza kabisa nadhani Mkurugenzi wa huo mfuko(portfolio) hafahamu kabisa swala zima la kuendesha insurance. Kwanza ningeomba maelezo ya swala zima la PREMIA, jee ni the same as premium? na kama ni sawa na premium jee kabla hawaja adopt hii system wamefanya research ya aina gani kujua ni watu gani wanachongai mfuko? Jee wana health condition za aina gani? Jee wana umri unao range vipi? Lengo zima la kufanya hii ni sababu premium payment haziwezi kufanana, kwani ni less likey kijana wa miaka 25 kulipa sawa na mzee wa miaka 50 sababu wote wana demand tofauti katika swala zima la afya.

Katika maelezo imeonyesha mkurugenzi anajifanya yupo immuni na system ambayo wote mlikubaliana. Invyoonekana mfumo ulitengenezwa kama HMO yaani Health Maintentenance Organization, mfumo unamtaka mshiriki katika mfuko kuwa na access ya baadhi ya hospital ambazo zimekubaliwa na mfuko. Basi kama hiyo ni agreement ya kwanza, hakuna anayetakiwa kuwa above the law, yaani mfuko hauwezi kudhamini mtu yoyote kutibiwa nje au kutibiwa kwenye hospital zisizo katika makubaliano na mfuko.

Ili tupate ufahamu zaidi jee unaweza tuambia huu mfumo wa premia ni nini hasa? Maana sielewi kwa nini kununuliwe mfumo? Insurance kazi yake ni kukusanya pesa na kuziwekeza kwenye liquidity asset ambazo ni rahisi kuzigeuza kuwa cash. Swala ambalo linatakiwa liangaliwe na watu wenye mueleo wa juu wa maswala ya usimamizi wa fedha. Sasa nisicho elewa ni kwanini kuwe na mfumo wa kununuliwa kutoka India?

Hii inatokana na kuwa na viongozi mbumbu wasio kubali kwamba hawawezi kuongoza. Kuchukua mwalim kutoka IFM does not mean kwamba ana knowledge ya kufanya investments kwenye sector ya insurance.

Kuonyesha ni jinsi gani viongozi wa huo mfuko hawana strategic plan ni kwa kuwakubalia wananchi kutumia pesa zao kisha kufanya claim at the end of the day. Jee ni kwa nini hawakuweza kuasign hospital na kisha kunegosiate na hizo hospital kwenye costs.

Nashindwa kufahamu huu mfuko ni Insurance portfolio au ni some kind of mfuko ulianzishwa ili watu wapate kuwaibia masikini? sababu characteristics zake ni za insurance lakini matendo yake ni ya kifisadi. Jee ni kwa nini wachangie ujenzi wa dhahanati ya Amana? Jee wana mfuko wanafaidika nini baada ya swala hilo? Jee premium zao zitashuka au?

Mkuu wa NHIF ulioleta hizi habari naomba uridi tena hapa jamvini kwa more clerification. Sababu naona huu ni wizi wa wananchi, ni unyanyasaji wa Watanzania, ni ubabe usio na kikomo.

JK hapo mwanzo alisema Hari mpya na kasi mpya, maisha bora kwa kila Mtanzania. Sasa swala langu ni moja kwa washauri wa JK. January Makamba naomba umuulize JK ya kwamba jee kuna maisha bora kwa kila Mtanzania kwenye swala hili. Kama serikali inashindwa kuwatetea walimu wa Shule za msingi kule Maweni, Muheza, Shelui, Kibaoni, Kibondo au kule Mkange jee serikali hii itamtetea nani? Jee haki iko wapi?

Mama Kikwete yeye alishakuwa mwalimu, jee unalionaje swala zima kama hili? Wakati wewe na wenzio kina mama Lowassa mnatumia Class A government Health Insurance hebu fikiria hawa wavuja jasho wanaongoza uchumi wa Tanzania, wavuja jasho wanafundisha majority ya Watanzania kusoma na kuandika.

Najua JK and associate wanapita hapo every day, naomba hili swala liwe challange kwa wote, najua January Makamba unatazama hapa, nakupa hili swala kama challange kwako, nafahamu kuna wawakilishi wa wizara ya afya wanachungulia hapa, nao nawapa hili swala kama challange kwao. Waziri Pinda saidia watanzania hawa. Tumeshindwa kuwakamata EPA, BUZWAGI, RICHMOND and Kiwira, Jee tutashindwa kuzuia swala linalo wagusa Watanzania wengi wa vijijini kama hili? Wapi moral wa Watanzania kwa ajiri ya Watanzania? Wapi watatezi wa wanyonge? Wapi Haki kwa wote?

Mungu ibariki Tanzania
 
Dalili ya mvua ni Mawingu, na mti wenye matunda hutupiwa mawe!!!!









Tunaandika tukitambua kwa kufanya hivi tunahatarisha ajira zetu, lakini tunasukuma tukiamini kuwa ustawi wa taifa unatangulia mbele ya ajiri zetu. Sisi ni wafanyakazi wa Mfuko wa Bima ya Afya(National Health Insurance Fund-NHIF) tunachukua hatua hii baada ya kuwa tumepoteza imani na watendaji wakuu wa wizara ya Afya, Bodi inayosimamia Mfuko, Uongozi wa Juu Mfuko chini ya Mkurugenzi Bwana Emmanuel Dotto Bundala Humba ambao ndie kiini na mhimili wa ufisadi katika mfuko.

Baada ya kuwa tumejitahidi kuwasalisha hoja zetu kwa kufuata mikondo inayoeleweka pasipo hatua zozote kuchukuliwa tunalazimika leo kuwasilisha kwenu tukitambua juhudi zenu adhimu na za kizalendo katika kulisafisha taifa dhidi ya makucha yetu. Kwa msukumo huo tunawasilisha rasmi hoja zetu kwa viongozi wa CHADEMA kama taasisi pekee yenye dhamira sahihi katika kulisafisha taifa(hapa tunatambua kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA ndio mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya kusimamia mahesabu ya Mashirika ya umma) pamoja na magezeti ya Mwanahalisi na Tanzania Daima ambayo kwa mtazamo wetu ndio magazeti pekee yenye ujasiri wa kutosha katika kuanika uozo katika jamii na taasisi za umma. Pia Tovoti ya Jambo Forum ambayo inaendelea kutoa mchango mkubwa kwa taifa katika vita dhidi ya ufisadi na ujenzi wa demokrasia nchini. Tunatanguliza shukran zetu kwa hatua mtakazo zichukua katika hili.

1. Mgongano wa Kimaslahi na “Hongo” kwa viongozi wa Bodi na Wizara ya Afya
Bwana Humba ni mjanja na mwepesi katika kuweka mitego kwa viongozi wanaopaswa kusimamia utendaji wake. Uongozi wa Bodi uliopita uliwahi kupokea malalamiko ya wafanyakazi juu ya “ukatili” na Minenendo mibaya ya bwana Humba. Bodi iliamua kuunda tume ya uchunguzi chini ya mwenyekiti wa bodi wakati huo Professa Msimbichaka na Makamu wake ndugu Rutazamba.

Kamati hii iliibua matumaini kwa wagfanyakazi wakijua hatimae kilio chao kitasikika. Ghafla bwana Humba aliamua kuambatana na Mwenyekiti wa Bodi kwenda china kuhudhuria mkutano. Waliporudi kamati ya uchunguzi ilikufa na Bwana Humba akanza kutoa vitisho kwa wafanyakazi kwamba alipokuwa China alielezwa na mwenyekiti wa Bodi(Professa Msimbichaka) kuwa kuna baadhi ya wafanyakazi akiwaondoa “atafanikiwa” sana katika shughuli zake.

Pia aliendeleza tabia ya kutoa upendeleo kwa mwenyekiti wa bodi katka kuhakikisha yote anayopanga yanapitishwa na bodi. Kuna kipindi alilazimisha mfuko kulipa gharama za matibabu ya ndugu wa mwenyekiti wa bodi iliyomaliza mda wake(Professa Msimbichaka) aliekuwa ametibiwa katika hospitali ya St. Bernard iliyopo Kariakoo ihali tayari mkataba ulikuwa umevunjwa baina ya mfuko na hospitali hiyo. “Upendeleo” wa aina hii hudhoofisha sana uwezo wa kiutendaji wa bodi.

Bwana Humba amendeleza utamaduni mbaya wa “kununua” viongozi wa Bodi na tayari mwenyekiti mpya wa bodi amaenasa katika mtego kwani binti yake ameajiriwa katika mfuko huu jambo ambalo linadhibiti uwezo wake wa kusimamia utendaji wa mkurugenzi na wa shirika kwa maana anajaribu kulinda fadhila aliyopewa kwa mtoto wake kupewa ajira.

Kama vile haitoshi mtoto wa kaka yake na katibu wa wizara ya afya nae ameajiriwa katika mfuko huu. Itakumbukwa kuwa katibu mkuu wa afya kwa wadhifa wake alikuwa ni mjumbe mwenye ushwawishi mkubwa katika bodi ya mfuko wa bima ya afya. Kwa sasa mjumbe wa bodi toka wizara ya afya ni mkurugenzi wa mipnago wa wizara hiyo ambae kimlaka yupo chini ya katibu mkuu wa widhara na baadhi ya mikutano katibu huudhuria, hali hii inamuhakikishiwa “ulinzi” bwana Humba katika wizara ya afya.

2.Kupindisha taratibu maksudi kwa maslahi Binafsi​

Mara nyingi bwana Humba amekuwa akikataa kuudhinisha malipo kwa wafanyakazi pale wanapokuwa wamepata matibabu katika vituo vya afya ua hopsitali ambazo hazijasaliwa na mfuko kwa maelezo kuwa ni nje ya utaratibu. Jambo la kushangaza ni kuwa mara mke wa wa Mkurugenzi alipopata matitizo ya mguu, alilazwa MOI(kitengo cha mifupa Muhimbili) wakati ambapo MOI hajaingia mkataba na Mfuko. Mfuko ulilipa kiasi kikubwa cha fedha kugharamia matibabu ya mke wa mkurugenzi.

Cha ajabu zaidi ni kuwa hivi majuzi mke wa mkurugenzi alipelekwa India kwa ajili ya matibabu na kugharamiwa na Mfuko. Safari hii iligharimu Mfuko kiasi cha shilingi 25,764,000. Itakumbukwa kuwa Mfuko haujaanza kugharamia matibabu nje ya nchi, mkurugenzi kwa kujitetea alisema kwamba ampewa kibali na wizara ya afya!

Cha kujiuliza ni wanachama wangapi wa mfuko wanapata fadhila hizi? Ikubukwe kuwa sehemu kubwa ya wanachama wa mfuko na wanchangiaji wakubwa ni walimu je wao wanaweza kupelekwa nje kwa matibabu? Cha kusikitisha ni kuwa haya yanatokea wakati ambapo raisi wa chama cha walimu ni mjumbe wa bodi.

Pia katika maonyesho ya sabasaba jumla ya shilingi 23,033,000 zilitoweka, yani haizkutolea maelezo yoyote katika ripoti. “Uwizi” huu ulifanyika chini ya usimamizi wa Mwenyekiti wa Sabasaba Bwana Raphael Mwamoto. Rafiki mkubwa wa Mkurugenzi. Uwizi huu ulibainishwa na mkaguzi wa ndani lakini habari zilipofikishwa kwa mkurugenzi hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.
Utendaji wa bwana Mwamoto ni wa kutilia shaka tangu alipoajiriwa katika mazingira ya kutatanisha. Hakuweza kufaulu katika kipindi cha majaribio(Propabation) lakini katika hali ya kustaabisha mkurugenzi aliaamua kumbadilisha idara. Bwana Mwamoto alikuwa mwalimu katika chuo cha usimamizi wa Fedha(IFM) kabla ya kuletwa na mkurugenzi katika mfuko wa bima ya afya, inasemekana hajaacha rekodi nzuri IFM. Mara nyingi wafanyakazi wanapojaribu kumchunguza na kumuwajibishwa hutishiwa kwa maelezo kuwa yeye ni afisa wa usalama wa taifa!

3.Ufujaji wa fedha​

Kiasi kikubwa cha fedha huwa kinapotea katika miradi mbalimbali ya shirika. Uwizi mkubwa upo katika kununua mfumo wa PREMIA ambao ulipaswa kubuniwa katika kusaidia uharakishaji wa malipo ya madai. Mfumo huu ulinunuliwa India. katika mkataba ulionekana utagharimu dola za kimerekani laki nne(400,000), hii ilikuwa mwaka 2005. Lakini cha kushangaza zimetumika zaidi ya shilingi milioni 700 katika manunuzi na mpaka leo mfumo huu(sytem) bado haujaanza kufanya kazi mpaka sasa. Ukipita katika ofisi za kanda utakuta wanatumia mfumo wa kawaida kulipa mahospitali.

Gharama za jumla za kuleta mfumo huu hewa zinazidi Bilioni moja ukujumlisha gharama za maandalizi, kuzunguka mikoani kutoa elimu kwa watoa huduma, matangazo katika vyombo vya habari na uzinduzi uliofanywa kwa kishindo kwa kuwakaribisha viongozi kutoka wizara ya Afya.

Cha kujiulizwa ni kwanini bodi inashindwa kuwawajibisha viongozi wa shirika kwa hasara kubwa kama hii? Uwizi huu unatokea ihali kuna malamiko makubwa toka kwa wanachama juu ya huduma mbaya za Mfuko. Hii ni sehemu ndogo tu ya ufisadi katika Mfuko wa bima ya Afya. Uchunguzi toka taasisi huru unaeweza kuibua mengi sana katika maeneo ya fedha, ukiukwaji wa taratibu na ajira holela zizizofuata taratibu za ajira.

4. Huduma Mbovu za Mfuko​

Uongozi wa sasa wa Mfuko umeshindwa kabisa kubuni mikakati ya kuimarisha huduma kwa wateja wake. Mfano sehemu kubwa ya wanachama wa mfuko huu ni walimu, wanapokwenda katika mahospitali au vituo vya afya katika maeneo yao na kukosa dawa, hulazimika kutumia fedha zao kununua dawa na Mfuko hukataa kuwafidia ghrama za mananuzi ya dawa ihali kila mwezi hukatwa katika mishahara yao kwa ajili ya mfuko. Haya yanatokea wakati Mfuko umekuwa mwepesi katika kutoa michango mikubwa katika shughulizi za hisani kama michezo!

Pia Kuna usumbufu mkubwa sana katika kutengeneza vitambulisho vya wanachama. Uongozi wa Humba hujitetea kuwa wao bado ni wachanga, yaani ni miaka saba ya uchanga! Itachukua miaka mingapi kwa Mfuko huu kukua chini ya uongozi wa Mfuko huu?

Katika hali ya kukosa mwelekeo ya kiongozi Mkurugenzi amaahaidi kujenga Hospitali Dodoma na Dar es salaam kwa kile anachokiita “centre of execelence”. Pia Mfuko umetoa shilingi milioni 225 kwa ajili ya ukarabati wa hospitali ya amana na mwananyamala! Hizi “centre of execelence” wanamjengea nani wakati wanachama wa Mfuko wako vijijini? Haya yanatokea wakati Raisi wa chama cha Walimu(CWT) bwana Mukoba na mwakilishi wa wafanyakazi wa serekali (TUGHE) bwana kiwenge ni wakumbe wa bodi! Ni kwanini wanashindwa kutetea maslahi ya wale wanaowawakilisha? Wanapumbambazwa na nini?

Kuna hitaji la lazima kuchukua hatua za haraka katika kuunusuru mfuku muhimu katika ustwi wa wafanyakazi. Tutaendelea kuwataarifu zaidi juu ya ufisadi unaoendelea katika taasisi hii muhimu katika ustawi wa wananchi hasa wenye kioato kidigo.

5.Dharau na Mienendo isiyokubalika katika jamii​

Mkurugenzi mkuu wa bima ya Afya moja ya Taasisi nyeti sana nchini ni mtu mwenye tabia ya majigambo, vitisho na dharahau. Mwenendo wake huu amewahi kuudhihirisha nje ya ofisi na kuupa fursa umma kutambua tabia halisi ya kiongozi mkuu wa shirika muhimu katika taifa. Itakumbukwa amewahi kumtukana na kumnyanyapaa nesi mmoja wa hospitali ya Hindu mandal(sasa marehemu) aliekuwa muathirika wa ugonjwa wa UKIMWI. Alifanya hivyo baada ya kuwa amekataliwa kupewa huduma kupitia mfuko wa bima ya afya kwa kuwa hakwenda na kitambulisho chake. Huu ni utaratibu wa kawaida katika uendeshaji wa mfuko.

Marehemu kwa kutambua muongozo na taratibu za mfuko alimkatalia mkurugenzi kwa kuwa alikuwa amekiuka utaratibu, mkurugenzi alijaribu kumtisha kwa kutumia wadhifa wake na kwamba atahakikisha anafukuzwa kazi, baada ya marehemu kuwa na msimamo pamoja na vitisho vya mkurugezi ndipo bwana Humba alipoanza kutukana matusi na kumskashifu marehemu kutokana na hali yale ya kiafya hali iliyopelekea marehemu kupata shinikizo liliochukua maisha yake masaa machache badae. Habari hii iliripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari lakini ghafla ikapotea katika namna ya kushangaza. Upo uwezekano alihonga ndungu wa marehemu na baadhi ya vyombo vya habari ili kudhibiti taarifa zaidi kutoka na pengine kuchukuliwa hatua za kisheria. Kadhia kama hizi sehemu ya kazi kwa wafanyakazi wa NHIF. Hatuamini kama hizi ni tabia stahili kwa mtu mwenye dhamana ya kuongoza shirika la bima ya Afya nchini.
 
Usishangaa sana sababu hata Maafisa wa Usalama wanajua hili,Ndiyo Hata Mwanakijiji alishawahi kuhoji je kuna ulazima wa TISS kuendelea kuwapo kama kuna mambo kama haya yanaendelea na wao bado wanaangalia.Tatizo ni Mkurugenzi au?

Mkuu Gembe,

Heshima mbele, hivi karibuni tulikuwa kwenye kufuatilia ile topic ya kumtaka mkurugenzi wa sasa ajiuzulu kama tulivyokuwa tumeahidi, mkuu tuliyoyagundua according to the dataz ni aibu tupu, ni kwamba yule mstaafu kumbe alichofanya ni kumuachia mkuu wa sasa cheo cha jina tu, kumbe yule mstaafu mpaka leo bado anai-run ile idara kwa manufaa yake binafsi na kikundi chake flani,

Matokeo yake ni kwamba huko ndani sasa kuna division kubwa, kati ya wenye nguvu na wasiokuwa nazo, ukweli tulioupata ni kwamba huyu wa sasa hana uwezo wa kufanya kitu chochote, na kwa mara ya kwanza tunaendelea kupata picha kamili ya ushiriki wa mstaafu wa idara kwenye kuwapa mtandao madaraka, kumbe ni wao wawili yeye na mkapa ndio waliohusika hasa, na huyu mstaafu ndiye hasa aliyekuwa a link kwa kuwa nduma kuwili kwa sababu kumbe kuna watu waliokuwa wakirekodi vikao vyake vingi vya siri kati yake na ra na el, kule Dodoma,

The bottom line ni kwamba ameiacha idara kwenye hali ngumu sana kikazi kwa sababu kuna wanaoendelea kumpelekea kila kitu kama vile bado ni bosi, na yeye ndiye anyeendelea kutoa maamuzi yote mazito, kwa hiyo ndugu zangu tunayo kazi kubwa sana as a nation, lakini hatutachoka hata siku moja, tutaendela kuzitafuta dataz na kuzifikisha panapotakiwa ili zifanyiwe kazi,

According to the more dataz... ni kwamba wabunge wengi wanasubiri kikao kijacho cha bajeti, moto utawaka sana!

Mungu Aibariki Bongo Yetu!
 
Wana JF wenzangu, mimi nawapongeza sana kwa kuanika uoza unaofanyika kutoka kila eneo hapa Tz.Nasikitika kwamba majority ya raia wanaishi katika maisha duni na watu wachache wanatumia hela ya walipa kodi kijitajirisha.Kibaya zaidi mafisadi hawa hawachukuliwi hatua kali na jamii yetu inazidi kuwa maskini.

Hatua ya kuwa expose ni moja ya hatua poa kabisa lakini kinachotakiwa hapa ni kuwafikisha katika vyombo vya sheria ili wahukumiwe kwa uhalifu waliotenda dhidi ya jamii.

Sijaona concrete action towards mafisadi kutoka kwa vyombo vyetu vinavyosimamia sheria.Mafisadi yanawadharau watendaji wa serikali.Mafisadi yana uwezo mkubwa wa kifedha na yanakandamiza juhudi za wanajamii kutafuta haki.

Tunaipigia kelele serikali ichukue hatua thabiti lakini naona serikali imekuwa kibogoyo,haina meno.

Tutafika? Nani wa kutufikisha kwenye haki yetu?

Wale wenye dhamana ya kutulinda na maovu wako pamoja na timu ya mafisadi.Kama hawako na mafisadi basi wachukue hatua ya dhati ya kufanya "operation fagia ufisadi" na kuleta heshima kwa taifa.

Kama hizi ni ndoto za kufikirika basi na tukae na kuishi kama tulivyo.Tukubali kunyanyaswa na wenye fedha zilizopatikana kwa njia za uhalifu.

Sasa sijui hata naandika nini...nachanganyikiwa....mwisho wake hata sijui.Ewe Mungu iondoe nchi hii kwenye ufisadi uliokubuhu ili watoto wa Tanzania waishi kwa amani na salama.Amin.
 
Lazima tukubali kuwa ile idara sasa hivi haipo kwani mambo yanayofanyika yanawadhalilisha sana, na kama hipo basi wafanyakazi wake ni wazembe sana au kama wanafanya kazi sawasawa wanamdhalilisha mkuu wa kaya kwani inawezekana wanamshauri lakini yeye hawezi kuchukua hatua madhubuti kwa wakati mpaka SFO waingilie kati.
 
Kwa kweli issue imefika mahali pake...wanajamii tuipigie debe huyu anayejiita mkubwa aadabishwe. Issue za mfuko wa Bima ya Afya imekuwa ni wimbo kwa walimu na walala hoi. Vimshahara vyenyewe vya kubeep halafu vinakatwa kila mwezi kwa geresha kuwa watapata huduma bora za afya. Kila siku wakienda hospitali wanaishia kupewa viasprini na kuambiwa dawa hakuna wakati bwana mkubwa anapeleka wife nje ya nchi na hospitali za maana kwa kutumia hela hizo hizo za michango ya walala hoi........ Hii nchi Jamani, ukifikiria sana unaweza ukatoa mtu roho...................
 
Kwa kweli issue imefika mahali pake...wanajamii tuipigie debe huyu anayejiita mkubwa aadabishwe. Issue za mfuko wa Bima ya Afya imekuwa ni wimbo kwa walimu na walala hoi. Vimshahara vyenyewe vya kubeep halafu vinakatwa kila mwezi kwa geresha kuwa watapata huduma bora za afya. Kila siku wakienda hospitali wanaishia kupewa viasprini na kuambiwa dawa hakuna wakati bwana mkubwa anapeleka wife nje ya nchi na hospitali za maana kwa kutumia hela hizo hizo za michango ya walala hoi........ Hii nchi Jamani, ukifikiria sana unaweza ukatoa mtu roho...................

Hili nalo inabidi liwekwe miguuni pa Kikwete.

Kikwete chonde chonde usiniangushe hata kwenye hili. Au unasubiria makachero wa nje waje kutusadia hapa pia?
 
Kinchosikitisha zaidi ni huyo mwanausalama wa taifa aliyegeuka kuwa fisadi anavyoshirikiana na mkurugenzi kuufilisi huo mfuko wa walimu walalahoi.
Inasikitisha na kukatisha tamaa kwa kweli.
 
kwani mafisadi wakitaka kula lazima watalazimisha mambo ili mradi wapate mahali pa kutafunia. Kwani ATCL imekuwaje watu wamelazimisha kukodi dege bovu ili wapate pa kula.
Utakapozungumzia matengenezo unatengeneza mpaka matumbo ya watu hata hili la Bima la afya ndio wale wale huenda hata huyo Humba anapata kiburi kuna mafisadi wakubwa wanamlinda....Iko siku yake naye tutamuweka sawa tu aeleze ukweli wa unachojua.....

Hivi Dr.Mwakyusa anayajua haya kama waziri mwenye dhamana au ndio wale wale funika kombe mwanaharamu apite???
 
Mkuu wa NHIF ulioleta hizi habari naomba uridi tena hapa jamvini kwa more clerification. Sababu naona huu ni wizi wa wananchi, ni unyanyasaji wa Watanzania, ni ubabe usio na kikomo.

Mtanganyika,

Tunashukuru. Tunasikitika kwamba Mkuu wa NHIF ameshindwa kurudi kwa wakati muafaka kuelezezea kwa upana yale ambayo ulikuwa umeyauliza ni kutokana na sababu zilizo juu ya uwezo wake.

Kwa siku tatu (3) zilizopita, NHIF Staff ameshindwa kabisa kuacess hii forum na amekuwa akijaribu mara kwa mara na kuishia kuambiwa kwamba User name na password ni incorrect. Sasa sijui kama huu ni ufisadi ndani ya Jamii Forum ama ni hali ya kawaida ambay oinawatokea watu wote.

Hata hivyo kuna usemi huwa napenda kuutumia kwamba, "Hata Punda Akifa Mzigo lazima Ufike!" kwa hiyo hili jukumu nalichukua mimi na kuhakikisha ya kwamba yale ambayo NHIF alitaka kuyaweka bayanayanawafikia.

Hatima ya Ufisadi huu lazima itafahamika na yale ambayo wanataka yafichike yatawekwa wazi!

Mpaka Kieleweke!
 
Mtanganyika,

Tunashukuru. Tunasikitika kwamba Mkuu wa NHIF ameshindwa kurudi kwa wakati muafaka kuelezezea kwa upana yale ambayo ulikuwa umeyauliza ni kutokana na sababu zilizo juu ya uwezo wake.

Kwa siku tatu (3) zilizopita, NHIF Staff ameshindwa kabisa kuacess hii forum na amekuwa akijaribu mara kwa mara na kuishia kuambiwa kwamba User name na password ni incorrect. Sasa sijui kama huu ni ufisadi ndani ya Jamii Forum ama ni hali ya kawaida ambay oinawatokea watu wote.

Hata hivyo kuna usemi huwa napenda kuutumia kwamba, "Hata Punda Akifa Mzigo lazima Ufike!" kwa hiyo hili jukumu nalichukua mimi na kuhakikisha ya kwamba yale ambayo NHIF alitaka kuyaweka bayanayanawafikia.

Hatima ya Ufisadi huu lazima itafahamika na yale ambayo wanataka yafichike yatawekwa wazi!

Mpaka Kieleweke!


Pengine amesahau signature yake mwambie awasiliane na Admin au Invisible.

Thanks
 
Nawashukuru wote kwamba nimefanikiwa kurudi katika Forum. Naomba niongezee haya yafuatayo katika mjadala mzima wa Ufisadi unaoendelea hapa NHIF.


"Awali ya yote napenda kuwashukuru wana JF wote kwa mchango wenu katika mjadala huu. Mmetupa moyo sana na hamasa kubwa na hivyo kudhihirisha kuwa wapo watanzania wenzetu katika maeneo mbalimbali ya dunia wenye uchungu na nchi yao. Asanteni sana. Pia kwa namna ya Kipekee na namshukuru ndugu Field Marshal ES kwa kufikisha kilio chetu katika mamlaka ya juu zaidi.

Mtusamehe kwa kuwa hatujaonekana tena tangu tuwalishe malezo yetu juu ya ufisadi wa NHIF unaongozwa na Humba! Tangu tumeandika JF juu ya ufisadi wa NHIF bwana Humba ameitisha kikao cha ‘management' na moja ya mambo waliojadili ni juu ya kuanikwa kwa udhaifu wake wa kioungozi. Alianza kwa kukurupuka kusaka vielelezo vya "Baraka" za wizara kumruhusu mkewe kutibiwa nje ya nchi kwa gharama ya Mfuko! Itakumbukwa,kama nilivyoeleza awali ushawishi mkubwa wa Humba kwa uongozi wa wizara ya Afya hususani Katibu mkuu wa wizara ambae nae ni mmojawapo wa watu wanaofaidika na "Hisani " Za Humba. Pia cha ziada ikiwa ni utaratibu wa kawaida kwa mtu kupewa Baraka na wizara ili atibiwe nje na kwa gharama za Mfuko, kwanini utaratibu huu usiwe wazi kwa wanachama wote? Kwanini usiwekwe? Yeye na wapambe wake wanamsaka kwa udi na uvumba mtu alie leta taarifa hapa. Uzuri ni kwamba wapo baadhi ya washauri wake waliomhakikishia kuwa JF haisomwi na watu wengi kwa hiyo hatapata madhara makubwa!


Upo ufisadi mwingine katika ujenzi wa jengo la NHIF liliopo Kursani ambao kwa sasa ndio makoa makuu ya NHIF. Gharama za awali za jengo zilisemwa kuwa ni Bilioni Mbili, cha kusikitisha ni kwamba gharama za ujenzi zimezidi mno kiasi cha awali kilichokubaliwa. Nasaka Nyaraka za kiasi halisi cha fedha kilichotumika kama ziada ya Bilioni mbili halafu nitawaletea hapa!!! Sasa kuna hali ya kutoamniniana baada ya habari hii kutoka, ila tutajitahidi kupata taarifa kamili.


Yupo aliuliza kuhusu mfumo wa Premia. Mfumo wa PREMIA sio Premium bali ni ‘software' iliyotazamiwa kuharakisha malipo ya wateja(mahospitali). Mpaka sasa mfumo haujaanza kazi baada ya matumizi yanaozidi Bilioni moja katika mfumo huo.


Kwa yule anaeulizia mawasiliano kamili ya Mkurugenzi wa NHIF bwana Humba ni haya Hapa:
Simu ya Mkononi: 0784650090
0784852339
Simu ya Mezani: 2133972
Email: ehumba@nhif.or.tz
ebdhumba@yahoo .com

Zipo taarifa nyeti tukifanikiwa kuzipata zitakuwa zimeanika kwa ufasaha ufisadi wa NHIF. Tunajitahidi, tukipata tutauleta hapa.

Asanteni
 
Kikwete Ana Kazi Sana Na Nchi Hii....tumuulize Swali Moja Tu"ataifanyia Nini Nchi Hii"
 
Inaelekea ufisadi umejikita vilivyo kila mahali. Inabidi tuutafute mzizi wa ufisadi tuung'oe la sivyo itakuwa kama tuna-prune matawi tu wakati mti unaendelea kushamiri...
 
Nawashukuru wote kwamba nimefanikiwa kurudi katika Forum. Naomba niongezee haya yafuatayo katika mjadala mzima wa Ufisadi unaoendelea hapa NHIF.


“Awali ya yote napenda kuwashukuru wana JF wote kwa mchango wenu katika mjadala huu. Mmetupa moyo sana na hamasa kubwa na hivyo kudhihirisha kuwa wapo watanzania wenzetu katika maeneo mbalimbali ya dunia wenye uchungu na nchi yao. Asanteni sana. Pia kwa namna ya Kipekee na namshukuru ndugu Field Marshal ES kwa kufikisha kilio chetu katika mamlaka ya juu zaidi.

Mtusamehe kwa kuwa hatujaonekana tena tangu tuwalishe malezo yetu juu ya ufisadi wa NHIF unaongozwa na Humba! Tangu tumeandika JF juu ya ufisadi wa NHIF bwana Humba ameitisha kikao cha ‘management’ na moja ya mambo waliojadili ni juu ya kuanikwa kwa udhaifu wake wa kioungozi. Alianza kwa kukurupuka kusaka vielelezo vya “Baraka” za wizara kumruhusu mkewe kutibiwa nje ya nchi kwa gharama ya Mfuko! Itakumbukwa,kama nilivyoeleza awali ushawishi mkubwa wa Humba kwa uongozi wa wizara ya Afya hususani Katibu mkuu wa wizara ambae nae ni mmojawapo wa watu wanaofaidika na “Hisani ” Za Humba. Pia cha ziada ikiwa ni utaratibu wa kawaida kwa mtu kupewa Baraka na wizara ili atibiwe nje na kwa gharama za Mfuko, kwanini utaratibu huu usiwe wazi kwa wanachama wote? Kwanini usiwekwe? Yeye na wapambe wake wanamsaka kwa udi na uvumba mtu alie leta taarifa hapa. Uzuri ni kwamba wapo baadhi ya washauri wake waliomhakikishia kuwa JF haisomwi na watu wengi kwa hiyo hatapata madhara makubwa!


Upo ufisadi mwingine katika ujenzi wa jengo la NHIF liliopo Kursani ambao kwa sasa ndio makoa makuu ya NHIF. Gharama za awali za jengo zilisemwa kuwa ni Bilioni Mbili, cha kusikitisha ni kwamba gharama za ujenzi zimezidi mno kiasi cha awali kilichokubaliwa. Nasaka Nyaraka za kiasi halisi cha fedha kilichotumika kama ziada ya Bilioni mbili halafu nitawaletea hapa!!! Sasa kuna hali ya kutoamniniana baada ya habari hii kutoka, ila tutajitahidi kupata taarifa kamili.


Yupo aliuliza kuhusu mfumo wa Premia. Mfumo wa PREMIA sio Premium bali ni ‘software’ iliyotazamiwa kuharakisha malipo ya wateja(mahospitali). Mpaka sasa mfumo haujaanza kazi baada ya matumizi yanaozidi Bilioni moja katika mfumo huo.


Kwa yule anaeulizia mawasiliano kamili ya Mkurugenzi wa NHIF bwana Humba ni haya Hapa:
Simu ya Mkononi: 0784650090
0784852339
Simu ya Mezani: 2133972
Email: ehumba@nhif.or.tz
ebdhumba@yahoo .com

Zipo taarifa nyeti tukifanikiwa kuzipata zitakuwa zimeanika kwa ufasaha ufisadi wa NHIF. Tunajitahidi, tukipata tutauleta hapa.

Asanteni

Thanks kwa kuja hapa kutufanyia clarification sasa nimeelewa zaidi kabisa kuhusu hiyo software ya Premia. Swala la kwanza jee swala zima la kuadopt PREMIA lilikubadilika miongoni mwa wanachama? Jee hii software itakuwa implimented kwenye kila kituo cha afya ambacho wanachama watatibiwa?

Ni wazi kabisa hili swala la kuadopt software kwa ajili ya kufanya malipo ni danganya toto, kwani kwa asilimia kubwa sana hapo Tanzania tekinologia hiyo itakubwa na ukinzani mkubwa. Jee ni kwanini swala la PREMIA halikuwekwa kama long term project? Maana sioni umuhimu wa kuadopt software itakayo tumika only Dar au kwenye miji mikubwa pekee kwani ndiko kwenye computer.

Jee mlikubaliana kuhusu ujenzi wa jengo la NHIF? Na kama halikuwepo kwenye makubaliano jee ni nani alianzisha, na kwa faida gani?
 
Kikwete Ana Kazi Sana Na Nchi Hii....tumuulize Swali Moja Tu"ataifanyia Nini Nchi Hii"

Nadhani katika harakati zake za kuwania Uraisi wa Tanzania mwaka 2005 Kikwete hakuwahi kufikiria kwamba anatakiwa kuitumikia nchi yake Tanzania.

Pamoja na kashfa zote ambazo zimemzunguka hajawahi hata mara moja kupambana na hawa mafisadi bila ya kuwaogopa!!! amekuwa ni mwoga na anadiriki kuendelea kumbatiana na hawa waovu MAFISADI waliomzunguka! Kila nikifikiria sisi walalahoi na huu mfuko wa Bima ya Afya, nafikia kwamba kuna siku mafisadi watatoka kwa mtutu!!!

Ikiwa tu rais ataendelea kutabasamu kinafiki hadharani... Kudhihirisha kwamba mafisadi watakingiana vifua always!
 
Back
Top Bottom