Ufahamu Mmea aina ya Azolla

Mzikii

Member
Oct 14, 2016
17
18
Habari wana JF. Azolla ni mmea(magugu) ambao huelea kwenye maji, mmea huu una kiwango kizuri cha protini 25 -30% na huota sana kwenye mashamba ya mpunga na madimbwi.Kutokana na tafiti mbalimbali mmea huu umeonekana kuwa na matumizi mengi katika sekta tofauti tofauti kama kwenye viwanda (Hasa katika nchi zilizoendelea), kilimo na ufugaji.

Katika nchi zetu Azolla hutumika sana kama chakula cha mifugo( Mfano Ng'ombe, kuku na samaki) tafiti pia zimethibitisha kuwa chakula hiki husaidia mifugo kukuwa vizuri na kutoa products kama ( maziwa, mayai na nyama) zenye ubora wa hali ya juu. Pia Azolla ni chakula kizuri sana kwa samaki kwa sababu ni chakula pekee cha asili kinachoelea hivo husiadia kupunguza gharama za kusafisha mabwawa kila baada ya muda fulani kutokana na kulisha samaki vyakula vinavyozama majini na kutuama.

Kilimo cha Azolla ni rahisi na kina gharama ndogo. Ili uweze kulima Azolla unahitaji kuwa na mbegu( Zinapatikana kwenye madimbwi), mbolea(Za asili au Kemikali), udongo, maji, plastic sheet( kwa ajili ya kutunza maji) na eneo. Kwa kuanzia Azolla inaweza limwa kwa kuchimba chini bwawa dogo lenye urefu wa mita 3 kwa 2 na kina cha futi moja(cm 30).

Azolla hukuwa ndani ya siku kumi na tano tu na baada ya hapo utakuwa unavuna kila baada ya siku mbili kwa mwaka mzima.Hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za chakula kama pumba kwa mifugo.

Nawasilisha;



Source: Yashrag Agro Tech and Knowledge Tv.
 
Hapo katika kuwapa kuku inakuwaje inakasuhwa au wanapewa yakawa mabichi hivyo hivyo?
 
Hapo katika kuwapa kuku inakuwaje inakasuhwa au wanapewa yakawa mabichi hivyo hivyo?
Mkuu denoo49, Azolla inaweza kutumika kwa kuku na mifugo mingine kama ng'ombe, sungura n.k, ikiwa katika hali ya ubichi( fresh) au ukavu (dried).Lakini azolla mbichi huwai kuharibika kwahiyo kama ipo nyingi unashauriwa kuikausha kwanza kwa matumizi ya muda mrefu.
 
Mi nikitaka mbegu napataje,na kwa kipimo hicho cha mita 3 kwa 2 unaweza kulisha kuku wangapi au sungura wangapi kwa siku?
 
Mi nikitaka mbegu napataje,na kwa kipimo hicho cha mita 3 kwa 2 unaweza kulisha kuku wangapi au sungura wangapi kwa siku?
Mbegu Tunazo ila kama upo kati ya mikoa ya Mwanza, Mara na Mbeya huko mbegu hupatikana kwa wingi katika madimbwi na mashamba ya mpunga, kwa kipimo hicho unaweza vuna kilo tatu(3kg) hadi nne(4kg) kwa siku hivo kwa hio siku moja unaweza kulisha kuku wakubwa thelathini(30) mpaka arobaini(40) hii ni kutokana kuwa kwa wastani kuku mkubwa mmoja hula gram 100 za chakula kwa siku.
Azolla inaweza tumika pekeake kama chakula pia inaweza tumika kwa kuchanganywa na vyakula vingine vya mifugo kama pumba.
 
Mbegu Tunazo ila kama upo kati ya mikoa ya Mwanza, Mara na Mbeya huko mbegu hupatikana kwa wingi katika madimbwi na mashamba ya mpunga, kwa kipimo hicho unaweza vuna kilo tatu(3kg) hadi nne(4kg) kwa siku hivo kwa hio siku moja unaweza kulisha kuku wakubwa thelathini(30) mpaka arobaini(40) hii ni kutokana kuwa kwa wastani kuku mkubwa mmoja hula gram 100 za chakula kwa siku.
Azolla inaweza tumika pekeake kama chakula pia inaweza tumika kwa kuchanganywa na vyakula vingine vya mifugo kama pumba.
Nashukuru sana kwa ufafanuzi,mi niko Njombe ngoja nione kama naweza kutafuta huku nikikosa ntafanya jitihada za kukutafuta kiongozi,thanks.
 
nimewahi kuzama kwenye dimbwi la maji nikidhani hakuna maji hayo majani yalitanda kufunika maji kabisa

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Mkuu mzikii, asante kwa taarifa.. Je, hayo magugu mtu akiyastawisha kwa ajili ya biashara, kuna soko lake?
 
Kweli mkuu.. Nilichojifunza kule ni kuwa kwa sasa soko ni kama halipo maana hayajazoeleka. Kama mtu akilima ni kwa ajili ya kulishia mifugo anayofuga. Asante
 
Habari wana JF. Azolla ni mmea(magugu) ambao huelea kwenye maji, mmea huu una kiwango kizuri cha protini 25 -30% na huota sana kwenye mashamba ya mpunga na madimbwi.Kutokana na tafiti mbalimbali mmea huu umeonekana kuwa na matumizi mengi katika sekta tofauti tofauti kama kwenye viwanda (Hasa katika nchi zilizoendelea), kilimo na ufugaji.

Katika nchi zetu Azolla hutumika sana kama chakula cha mifugo( Mfano Ng'ombe, kuku na samaki) tafiti pia zimethibitisha kuwa chakula hiki husaidia mifugo kukuwa vizuri na kutoa products kama ( maziwa, mayai na nyama) zenye ubora wa hali ya juu. Pia Azolla ni chakula kizuri sana kwa samaki kwa sababu ni chakula pekee cha asili kinachoelea hivo husiadia kupunguza gharama za kusafisha mabwawa kila baada ya muda fulani kutokana na kulisha samaki vyakula vinavyozama majini na kutuama.

Kilimo cha Azolla ni rahisi na kina gharama ndogo. Ili uweze kulima Azolla unahitaji kuwa na mbegu( Zinapatikana kwenye madimbwi), mbolea(Za asili au Kemikali), udongo, maji, plastic sheet( kwa ajili ya kutunza maji) na eneo. Kwa kuanzia Azolla inaweza limwa kwa kuchimba chini bwawa dogo lenye urefu wa mita 3 kwa 2 na kina cha futi moja(cm 30).

Azolla hukuwa ndani ya siku kumi na tano tu na baada ya hapo utakuwa unavuna kila baada ya siku mbili kwa mwaka mzima.Hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za chakula kama pumba kwa mifugo.

Nawasilisha;



Source: Yashrag Agro Tech and Knowledge Tv.
Thanks for sharing..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom