Kwa kisayansi inaitwaje hiyo pilipili manga
Malila tunaomba msaada wako huku.
Bull Dog kanichomekea mchana kweupe !!!!!!
Kuna wakati nilitaka kwenda Morogoro kuona kilimo cha pilipili Mtama kule milimani, nikakosa usafiri. Asante kwa homework, ngoja niingie chaka nikaone kilichoko, nami nikipata nitarusha hadharani.
Si uongo Bulldog kachapia kumbe? UKipata chochote tutupie hapa. Natanguliza shukrani.
Tiba
Mkuu Malila anajua sana hii kitu.
Inaitwa Black pepper kwa lugha za watu wa Uk, kwa wingi inalimwa India, na hapa Tz inalimwa Unguja na Pemba. Kwa leo niishie hapa. Ingia kwa google, andika black pepper farming, kitu kinakuja kiulaini.
Wadau,
Nimetonywa na mtu kwamba zao la pilipili manga lina soko na kwa bei nzuri kwenye nchi za kiarabu. Nilitaka kujaribu kulima ili zao. Je kuna anayejua kilimo hiki kinaendeshwaje? Nataka kujua kama unapanda mbegu kwenye matuta au ni plain land, je ni zao linalostahimili ukame au mvua nyingi ni lazima? Na kwa hapa Tanzania hili zao linalimwa wapi?
Msaada tafadhali. Ili zao linaweza kunitoa kwenye umasikini.
Tiba
![]()
Pilipili manga zinastawi na kulimwa sana maeneo ya Amani Muheza Tanga (Usambara Mashariki). Pilipili manga zinapandwa kama vile unavyopanda matunda ya mipensheni. Shamba lako ni lazima liwe na idadi kubwa ya miti, miche ya pipili manga huoteshwa chini ya mti na kutambaa na mti hadi kileleni (tazama picha hapo juu). Kama shamba lako lina vyanzo vizuri vya maji na ukawa unamwagilia kila wakati ndiyo pilipili manga inavyochanua maua na kupata vikonyo vingi vya mbegu kama vinavyoonekana hapa chini.
Pilipili manga haina msimu jinsi inavyopata maji ndiyo huchanua mwaka mzima na inadumu zaidi ya miaka mitano, mazao yakianza kuwa hafifu unang'oa na kupanda pilipili mpya.
![]()
Asante mkuu kwa ushauri wa kitaalamu. Kwa ujuzi wako wa ili zao, linaweza kutoa mazao mazuri upande huu wa Bagamoyo?
Tiba
Black pepper tolerates temperature between 10°C and 40°C.
Gharama za kilimo zikoje kwa heka moja??
Kama utahitaji mbegu na ushauri, funga safari hadi Muheza Tanga, kutoka Muheza panda daladala zinazoenda Amani, muombe kondakita akushushe kiwanda cha pilipili au Jumuiya ya Wakulima wa Kilimo Hai Usambara Mashariki (JUWAKIHUMA) ni safari ya nusu saa kutoka muheza mjini.
Wanavyo vitalu na mbegu za kutosha.
![]()
Mkuu kama bado hujapata majibu tembelea www.kilimo.go.tz kuna pdf ya kilimo cha pilipili mtama.Wadau,
Nimetonywa na mtu kwamba zao la pilipili manga lina soko na kwa bei nzuri kwenye nchi za kiarabu. Nilitaka kujaribu kulima ili zao. Je kuna anayejua kilimo hiki kinaendeshwaje? Nataka kujua kama unapanda mbegu kwenye matuta au ni plain land, je ni zao linalostahimili ukame au mvua nyingi ni lazima? Na kwa hapa Tanzania hili zao linalimwa wapi?
Msaada tafadhali. Ili zao linaweza kunitoa kwenye umasikini.
Tiba