ufafanuzi wa haya maandiko

nyabhingi

JF-Expert Member
Oct 12, 2010
15,515
20,005
MODS KUWENI NA UVUMILIVU,HII NI MIJADALA MUHIMU KATIKA KUWEKANA SAWA KUHUSU HAYA MAPOKEO KWA MTU MWEUSI KUTOKA UGHAIBUNI..

Kumbukumbu la Torati 28:53

53 Nawe utakula uzao wa tumbo lako mwenyewe, nyama ya wana wako na binti zako aliokupa Bwana, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako.


Malaki 2:1-3

2 Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema Bwana wa majeshi, basi nitawapelekeeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni.

3 Angalieni, nitaikemea mbegu kwa ajili yenu, nami nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya vyakula vyenu; nanyi mtaondolewa pamoja nayo


Luka 22:36

Akawaambia, Lakini sasa mwenye mfuko na auchukue, na mkoba vivyo hivyo; naye asiye na upanga, na auze joho yake akanunue.


Mwanzo 3:22

Kisha Mwenyezi-Mungu akasema, “Sasa, binadamu amekuwa kama mmoja wetu, anajua mema na mabaya. Lazima kumzuia kula lile tunda la mti wa uhai, kwani akilila ataishi milele!”



HESABU 31:15-17

15 Kwa hiyo Musa akawaambia: “Je, mmemhifadhi hai kila mwanamke?+ 16 Tazama! Hao ndio, kupitia kwa neno la Balaamu, waliowashawishi wana wa Israeli kukosa uaminifu+ kwa Yehova juu ya lile jambo la Peori,+ hivi kwamba tauni ikaja juu ya kusanyiko la Yehova.+ 17 Na sasa ueni kila mtoto wa kiume, na kumuua kila mwanamke ambaye amefanya ngono na mtu kwa kulala na mwanamume


Warumi 13

13 Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu. 2 Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu.


1 timotheo 2:11-12

11 Mwanamke na ajifunze akiwa kimya na kwa kujitiisha kikamili.+ 12 Simruhusu mwanamke kufundisha,+ wala kuwa na mamlaka juu ya mwanamume,+ bali kuwa kimya.


Mwanzo 9:25-27

25 Basi akasema:“Alaaniwe Kanaani.

Na awe mtumwa wa hali ya chini kabisa kwa ndugu zake.”26 Naye akasema tena:“Abarikiwe Yehova, Mungu wa Shemu,Kanaani na awe mtumwa wake. 27 Mungu na ampe Yafethi nafasi ya kutosha,Akae katika mahema ya Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake pia.”


Ezekieli 23:20

Aliwatamani sana wanaume wenye uume kama wa punda na manii kama farasi dume.”


Kumbukumbu la torati 28:28-35

28 Yehova atakupiga kwa wazimu+ na kupoteza uwezo wa kuona+ na kuchanganyikiwa kwa moyo.+ 29 Nawe kwa kweli utakuwa mtu anayepapasa-papasa katikati ya mchana, kama vile kipofu anavyopapasa-papasa gizani,+ nawe hutafanya njia zako zifanikiwe; nawe utakuwa mtu tu ambaye sikuzote hupunjwa na kunyang’anywa, pasipo mtu wa kukuokoa.+ 30 Utamchumbia mwanamke, lakini mwanamume mwingine atamlala kinguvu.+ Utajenga nyumba, lakini hutakaa ndani yake.+ Utapanda shamba la mizabibu, lakini hutaanza kutumia matunda yake.+ 31 Ng’ombe-dume wako atachinjwa hapo mbele ya macho yako—lakini hutakula sehemu yoyote yake. Utanyang’anywa punda wako mbele ya uso wako—lakini hatarudi kwako. Kondoo wako watapewa adui zako—lakini hutakuwa na mwokozi yeyote.+ 32 Wana wako na binti zako watapewa watu wengine+ na macho yako yakitazama na kuwatamani sikuzote—lakini mikono yako itakuwa haina nguvu.+ 33 Mazao ya udongo wako na mazao yako yote yataliwa na watu ambao hukuwajua;+ nawe utakuwa mtu aliyepunjwa na kupondwa sikuzote.+ 34 Nawe utatiwa wazimu kwa kuona kwa macho yako mambo ambayo utaona.+ 35 “Yehova atakupiga kwa jipu hatari kwenye magoti yote mawili na miguu yote miwili, ambalo hutaweza kupona, kutoka wayo wa mguu wako mpaka utosi wa kichwa chako


Kumbukumbu la torati 25:11

11 “Ikiwa wanaume wawili watapambana pamoja, na mke wa mmoja awe amekuja karibu ili kumkomboa mume wake kutoka mkononi mwa yule anayempiga, naye ameunyoosha mkono wake na kumkamata sehemu zake za siri,+ 12 basi ukate mkono wa mwanamke huyo.



2 wafalme 2:23-25

3 Naye akapanda kutoka hapo mpaka Betheli.+ Alipokuwa akipanda njiani, tazama, palikuwa na wavulana+ wadogo waliotoka katika jiji, nao wakaanza kumdhihaki,+ wakazidi kumwambia: “Nenda juu, wewe kipara!+ Nenda juu, wewe kipara!” 24 Mwishowe akageuka nyuma, akawaona, naye akawalaani+ katika jina la Yehova. Ndipo dubu-jike+ wawili wakatoka katika vichaka, wakaanza kuwararua vipande-vipande watoto 42 kati yao.+ 25 Naye akaendelea kutoka hapo mpaka Mlima Karmeli,+ na kutoka hapo akarudi Samaria.


Kumbukumbu la torati 21:18-21

“Ikiwa mtu atakuwa na mwana ambaye ni mkaidi na mwasi,+ awe hasikilizi sauti ya baba yake au sauti ya mama yake,+ nao wamemrekebisha bali yeye hawasikilizi,+ 19 baba yake na mama yake watamshika na kumtoa nje mpaka kwa wanaume wazee wa jiji lake na kwenye lango la mahali pake,+ 20 nao watawaambia wanaume wazee wa jiji lake, ‘Huyu mwana wetu ni mkaidi na mwasi; hasikilizi sauti yetu,+ ni mlafi+ na mlevi.’+ 21 Ndipo watu wote wa jiji watampiga kwa mawe, naye lazima afe.



Mambo ya walawi 21:17-23

17 “Sema na Haruni, na kumwambia, ‘Mtu yeyote wa uzao wako katika vizazi vyao vyote ambaye ana kasoro+ asije karibu ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 18 Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye kasoro, asikaribie: mtu aliye kipofu au kilema au mwenye pua pana au mwenye kiungo kimoja kilicho kirefu mno,+ 19 au mtu aliyevunjika mguu au aliyevunjika mkono, 20 au mwenye kijongo au aliyekonda au mwenye ugonjwa wa macho au mwenye vigaga au mwenye mba au aliyevunjwa mapumbu yake.+ 21 Mtu yeyote wa uzao wa Haruni kuhani ambaye ana kasoro hatakaribia ili kutoa matoleo ya Yehova kwa njia ya moto.+ Kuna kasoro ndani yake. Hatakaribia ili kuutoa mkate wa Mungu wake.+ 22 Anaweza kula mkate wa Mungu wake kutoka kati ya vitu vitakatifu zaidi+ na kutoka kati ya vitu vitakatifu.+ 23 Hata hivyo, hatakaribia pazia,+ wala hatakaribia madhabahu,+ kwa sababu kuna kasoro ndani yake;+ naye hatapatia unajisi patakatifu pangu,+ kwa kuwa mimi ni Yehova ninayewatakasa wao.


1 samweli 15:3

3 Sasa nenda, umpige Amaleki,+ umwangamize+ pamoja na vitu vyote alivyo navyo, usimhurumie, nawe uwaue,+ mwanamume na mwanamke, mtoto na mtoto anayenyonya,+ ng’ombe pamoja na kondoo, ngamia pamoja na punda.’


Mwanzo 22:2

Mungu akamwambia, “Mchukue mwanao, Isaka, mwanao wa pekee umpendaye, uende mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuonesha.”



1 Petro 2:18

18 Ninyi watumwa, watiini mabwana wenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wapole na wema peke yao, bali hata wale walio wakali.
 
Hapo pa Ezekiel 23:20 umetoa kwenye biblia ya aina gani?
Maana niliyosoma mimi haina neno uume?
Screenshot_20181003-160951.jpeg
 
hoja yako kubwa ni nini mkuu?
bibilia imejaa mashahiri, maonyo na kupewa matokeo halisi ya kutotii, mifano, nyimbo, mithali,maombi, maonyo maelekezo, makosa ya watakatifu, operation za Mungu wakati watu wakiwa na ujinga wa elimu ya ukombozi wa Mungu.
sasa ukiingia ukakokota vifungu lazima upoteze mwelekeo.
binafsi sijaona tatizo hapo, labda kama kuna moja ambalo umelipa kipaumbele.
 
Mathayo 11:25 Ndipo Yesu akasema: “Ninakusifu hadharani, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu nawe umeyafunua kwa watoto wadogo.


lazima uwe mnyenyekevu kama mtoto mdogo ili uelewe Biblia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom