Ufafanuzi kuhusiana na maji ya mochwari ya kuoshea miili ya marehemu na matumizi yake kwenye kitoweo cha samaki wa kanda ya ziwa

Ufafanuzi kuhusiana na maji ya mochwari ya kuoshea miili ya marehemu na matumizi yake kwenye kitoweo cha samaki wa kanda ya ziwa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,869
Reaction score
828,403
Naandika kwa ufahamu na uzoefu wangu kutokana na kuwa mhudumu wa chumba cha maiti(mochwari) hapo kabla.. Nimewahudumia marehemu wengi kwa nyakati tofauti na wa jinsia na rika tofauti

Tangu tuhuma zilipotolewa siku mbili zilizopita na makamu wa rais jijini Mwanza akituhumu maji ya kuoshea maiti kama kisababishi cha ugonjwa wa saratani (sijui ni ipi mojawapo maana ziko nyingi) kutokana na kutumiwa kwenye kitoweo cha samaki na wafanyabiashara wa hiyo mboga.. Nilisita sana kuweka hii mada lakini kwenye kila uzi uliohusu hiyo tuhuma nilijitajidi kutoa ufafanuzi lakini nimegundua bado mkanganyiko ni mkubwa

Sasa iko hivi je maji ya mochwari ya kuoshea maiti ninini?
Haya ni maji ya kawaida kabisa yale ya kuuzwa dukani ama ya kisima ama ya DAWASA
Ni maji ya kumsafisha marehemu marehemu ama kumuogesha kwa ajili ya kumuandaa kwa safari yake ya mwisho na kumvisha nguo nzuri.. Hakuna la zaidi kama kumuogesha tu mtu yoyote anayetaka kuoga mwenye uchafu wa kawaida mwilini usoni sehemu za siri nk

Tunawaogesha ama kuwaosha marehemu kama maandalizi ya safari yao ya mwisho kwakuwa mara nyingi kwenye kitanda cha ugonjwa hawaogi/ogeshwi vizuri, ama kama ni mwili wa ajali kuwa na damu, vumbi tope nk..
Naendelea
Kimsingi si kumuogesha bali ni kumsafisha kwa taulo na maji ya sabuni, kumfutafuta na kumuosha sehemu mbali mbali za mwili

Kifuatacho ni kumpaka mafuta na kumremba, kumpulizia marashi fulani makali yanayodhibiti harufu yoyote kwa haraka kisha kumpulizia chemicali ya fomalin inayozuia mchakato wa mwili kuoza haraka.. Maana baada ya pumzi tu kuacha mwili kuoza na kuharibika ni haraka mno

Kwahiyo maji ya kuoshea maiti maarufu kama maji ya mochwari hayana tofauti na yale maji unayooga wewe.. Labda tu ni kwamba yale yanaosha mfu
Haya maji hayamwagwi hovyo na si maji ya kuyaweka muda mrefu maana yana uchafu wa mfu unaooza na kunuka sana

Maji ya mochwari kwenye ulimwengu wa roho ni maji mfu yasiyofaa chochote kwenye kutengeneza ngekewa mvuto nk iwe wa kimapenzi au kibiashara.. Ni maji yanayotumika kishirikina kuharibu kufisha, kuua, kutengenisha nknk.. Kamwe huwezi kuyatumia kuweka kwenye kitoweo cha samaki waliokufa.. Wataoza chini ya masaa 6

Sasa basi ninnini kilichoitwa maji ya mochwari? Hicho kitu ni ile chemikali ya fomalini inayozuia uharaka wa kitu chenye nyama kuoza haraka
Wavuvi wengi hawana majokofu ama vyombo vya kuhifadhi muda mrefu samaki wao kabla ya kumfikia mlaji wa mwisho.. Hivyo hupata fomalin kwa njia za magendo na kuitumia kuhifadhia mawindo yao.. Na hii sio kwenye samaki tu bali hata kwenye mabucha mbali mbali nchini ya nyama nyinginezo

Matumizi ya fomalin kwa ajili ya kuhifadhia vitoweo vya nyama tuhuma zake ni za muda mrefu sana tangia enzi za mzee ruksa, lakini kwa vile madhara yake si ya papo kwa papo.. Wafanyabiashara wasio wazalendo na watumishi wasio waaminifu wameendelea kutuumiza. Na si fomalin zote zinatoka mochwari nyingine hazifiki kabisa

Makamu wa rais anapaswa kurudi kwenye media na kutoa ufafanuzi kuepusha mkanganyiko kwenye jamii
 
.... Kumbe, mie najuaga ni usafi uliozidi.

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
Ile nyama ni mfu iliyoko kwenye mchakato wa kuoza, hata bucha iwe safi vipi harufu haiwezi kukosekana na kinachowavuta inzi ni harufu
Zaidi fuatilia haya mabucha ya kisasa yenye vioo full jokofu na sometimes AC unapoingia unakutana na kaharufu kasiko ka kawaida kama ka mochwari hivi na si harufu ya nyama yenye damu
 
Mheshimiwa yeye yawezekana alisema ukweli, tatizo ni namna alivyoufikisha ujumbe kwa jamii.

Mtani, niliwahi kusikia maji hayo eti yana ngekewa, mmmh.

Swali langu unalolikimbia kila siku sijui nikuulize tena.
karibu mtani niulize tuu.. Lakini yale ni maji mfu hayana jema ndio maana hayamwagi hata mtaroni wala hayafukiwi ardhini isipokuwa kwa sababu maalum
 
Ishu hizi tangu kitambo Sana,

Marehemu anko wangu Alikua dokta wa mifugo Anakuja dar anasomba mapipa kibao ya formaldehyde (fomalin) na Toyota Hilux anapeleka kuuza mwanza kwa wavuvi.

Mwanzon akaniambia ile Ni dizeli anawapelekea wavuvi kuendeshea injini zao ziwani. Nami Nikaamini

Ila Nikiwa advance najisomea organic chemistry, katika kunifafanulia ndo akanambia kua formaldehyde ndo ile huwa anabeba kwenye mapipa kwenda kuhifadhia samaki uko visiwani Maana kule hamna umeme wala mafriji.

Enzi hizo
Ndo zile meli na boti za uvuvi za mweshimiwa kishimba ndo zimepamba Moto, samaki wanauzwa Hadi ulaya Sato Yuko fresh na kavuliwa miez 2 ilopita visiwani ndani ndani uko hamna umeme wala friji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom