Buyaka
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 1,643
- 1,786
Utoto wa Nyerere umeuleta wewe hapa, jamaa hajasema lolote kuhusu utoto wa Nyerere wala kwamba yeye ni kiongozi wa CCM kwa vile eti ni mtoto wa Nyerere , acha kubabaikia pedigree ya mleta hoja, nobody is talking about utoto wa Nyerere hapa, get a grip!CCM sio chama cha kifalme kuwa mtoto Nyerere haimaniishi wewe ni kiongozi wa CCM
Mtu akitoa nasaha zake kwamba Kikwete apumzike hapo zimevunjwa taratibu gani za chama?
Kikwete ameshindwa kuongoza chama, kila siku ni minyukano ya wenyewe kwa wenyewe kwenye press conferences zisizoisha. Mwenyekiti anaambiwa chama kinaelekea pabaya anajibu kwa mipasho, "kwa wale wanaosema chama kinakufa watakufa wao itabaki CCM..." anajibu mipasho utadhani sio Rais. Kwani Nyerere alivyokua anaasa kuhusu mustakabali wa CCM alimaanisha hatakufa kabla hayo anayoasa hayajatokea? Kuna mtu hafi maisha haya? JK please! Shameful irresponsible leader, worst chairman CCM has seen since its founding in 1929.