Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,213
- 9,643
Ndugu zangu,
Rais mstaafu mh Jakaya Kikwete Ndiye Aliyenishawishi Kujiunga na CCM Mwaka 2005 Nikiwa mkoani Rukwa wilaya ya Sumbawanga vijijini, mji mdogo wa Laela Jimbo la Kwela lililokuwa linaongozwa na Marehemu Chrisant maji ya Tanga Mzindakaya. Nilikuwa huko kwa baba yangu mdogo ambako nilikuwa nasoma.
Kikwete alikuwa amekuja kuomba kura za Urais katika uchaguzi mkuu ulioacha historia ya kipekee kuwahi kutokea hapa nchini kwa mgombea wa CCM kupendwa na kukubalika na makundi yote na vyama vyote hadi vya upinzani.
Hakika kikwete alikubalika, alipendwa, alikuwa na mvuto wa kisiasa kuwahi kutokea hapa nchini. Kila mtu alitamani kumuona na kumsikiliza, kila mtu alitamani asiondoke na kufunga mkutano, kila mtu alitamani siku ya kupiga kura ifike haraka ili ampigie kura kikwete.
Watu waliona ni kama siku ya kupiga kura inachelelewa sana kufika maana kila mtu alitaka kuwa sehemu ya historia kumpigia kura Kikwete, hakika kampeni zake zilipendeza na kuvutia. Kila Kona na kila mahali ilikuwa ni CCM tu.
Picha zake zilipambwa na kupambika kila mahali, tisheti na vitenge vyenye picha yake vilivaliwa na kila mtu utafikiri sare ya taifa, hakika hata mimi niliitafuta tisheti ya CCM yenye picha yake kwa hali na mali.
Hatimaye Kikwete alikaribishwa jukwaani kutoka jukwaa kuu, lakini kitu alichokifanya Kikwete kilibaki ni historia na kuandika jina lake katika mioyo ya Wafipa na wana laela. Kikwete aliinua mkono wake juu na kufunua lile jukwaa dogo alipokuwa anatakiwa kusimama na kuhutubia kusudi na yeye awe juani maana jua lilikuwa limewaka.
Halafu akasalimia na kwa upole na tabasamu akasema, "NYOTA NJEMA HUONEKANA ASUBUHI", uwanja mzima uliokuwa umefurika mpaka pa kupita sisimizi palikosekana ulilipuka kwa shangwe, nderemo, vifijo, makofi, kelele za kuimba Rais..Rais..Rais zikitawala uwanja wote wa shule ya msingi Laela. Jamani ilikuwa ni furaha kubwa sanaaa kwetu.
Kitendo cha kutoa kitambaa kilichokuwa kimefunika jukwaa lake ili Naye akae juani Kama sisi kilitugusa na kugusa mioyo ya wote, watu wakasema hakika huyu Ni chaguo la Mungu,Hakika huyu atalia nasi katika shida na kufurahi nasi katika Raha, wakasema hakika huyu Ni Joshua anaye tupeleka Kanaan, wakasema hakika huyu atasimama nasi katika magumu,wakasema huyu Ni mwezetu alietoka na kukulia katika maisha yetu na anayejuwa maisha yetu na Hali zetu. Kila mtu aliongea mengi Sana ya kumpongeza mh kikwete.kama Ni point Basi alizoa point zote. Kama Ni Kura hakika alizoa Kura zoteee za Wana laela,
Kiukweli Ni kutokea hapo niliipenda Sana CCM, Nilitamani ningempigia Kura katika uchaguzi ule lakini nilikuwa sijafikia umri wa kupiga kura, hivyo nikaishia kuwaambia watu wampigie kura Rais kikwete aliyeonyesha moyo wa upendo kwetu wananchi Hadi kuamua kukaa na kusimama nasi juani licha ya kuwekewa kimvuli. Nikutokea hapo nimekuwa mtafuta Kura za CCM popote pale. Ni kutokea hapo sijawahi kujuta kuwa mwana CCM. Wala sijawahi kuacha kuisemea CCM mahali nilipo. Ni kikwete Ndiye Aliyenishawishi kuipenda CCM maana niliona Ni chama kinachowajali wananchi na kuguswa na shida zao na kuwa na Sera na ajenda zinazogusa maisha ya watanzania.
Asante Sana mh kikwete kwa kunifanya kuipenda siasa na CCM kwa ujumla,Asante kwa kutujengea shule za kata ambazo Mimi Ni mnufaika nazo na nimefaidika na kupata Elimu kupitia juhudi zako ,Asante kwa kunipatia mkopo wa Elimu ya juu ulionisaidia kutimiza Ndoto zangu za kupata Elimu ya juu licha ya kuwa nimetoka familia masikini,Asante kwa kulitumikia Taifa letu kwa uzalendo mkubwa na kwa demokrasia ya Hali ya juu sana,.
Kazi Iendeleee , mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627
Rais mstaafu mh Jakaya Kikwete Ndiye Aliyenishawishi Kujiunga na CCM Mwaka 2005 Nikiwa mkoani Rukwa wilaya ya Sumbawanga vijijini, mji mdogo wa Laela Jimbo la Kwela lililokuwa linaongozwa na Marehemu Chrisant maji ya Tanga Mzindakaya. Nilikuwa huko kwa baba yangu mdogo ambako nilikuwa nasoma.
Kikwete alikuwa amekuja kuomba kura za Urais katika uchaguzi mkuu ulioacha historia ya kipekee kuwahi kutokea hapa nchini kwa mgombea wa CCM kupendwa na kukubalika na makundi yote na vyama vyote hadi vya upinzani.
Hakika kikwete alikubalika, alipendwa, alikuwa na mvuto wa kisiasa kuwahi kutokea hapa nchini. Kila mtu alitamani kumuona na kumsikiliza, kila mtu alitamani asiondoke na kufunga mkutano, kila mtu alitamani siku ya kupiga kura ifike haraka ili ampigie kura kikwete.
Watu waliona ni kama siku ya kupiga kura inachelelewa sana kufika maana kila mtu alitaka kuwa sehemu ya historia kumpigia kura Kikwete, hakika kampeni zake zilipendeza na kuvutia. Kila Kona na kila mahali ilikuwa ni CCM tu.
Picha zake zilipambwa na kupambika kila mahali, tisheti na vitenge vyenye picha yake vilivaliwa na kila mtu utafikiri sare ya taifa, hakika hata mimi niliitafuta tisheti ya CCM yenye picha yake kwa hali na mali.
Hatimaye Kikwete alikaribishwa jukwaani kutoka jukwaa kuu, lakini kitu alichokifanya Kikwete kilibaki ni historia na kuandika jina lake katika mioyo ya Wafipa na wana laela. Kikwete aliinua mkono wake juu na kufunua lile jukwaa dogo alipokuwa anatakiwa kusimama na kuhutubia kusudi na yeye awe juani maana jua lilikuwa limewaka.
Halafu akasalimia na kwa upole na tabasamu akasema, "NYOTA NJEMA HUONEKANA ASUBUHI", uwanja mzima uliokuwa umefurika mpaka pa kupita sisimizi palikosekana ulilipuka kwa shangwe, nderemo, vifijo, makofi, kelele za kuimba Rais..Rais..Rais zikitawala uwanja wote wa shule ya msingi Laela. Jamani ilikuwa ni furaha kubwa sanaaa kwetu.
Kitendo cha kutoa kitambaa kilichokuwa kimefunika jukwaa lake ili Naye akae juani Kama sisi kilitugusa na kugusa mioyo ya wote, watu wakasema hakika huyu Ni chaguo la Mungu,Hakika huyu atalia nasi katika shida na kufurahi nasi katika Raha, wakasema hakika huyu Ni Joshua anaye tupeleka Kanaan, wakasema hakika huyu atasimama nasi katika magumu,wakasema huyu Ni mwezetu alietoka na kukulia katika maisha yetu na anayejuwa maisha yetu na Hali zetu. Kila mtu aliongea mengi Sana ya kumpongeza mh kikwete.kama Ni point Basi alizoa point zote. Kama Ni Kura hakika alizoa Kura zoteee za Wana laela,
Kiukweli Ni kutokea hapo niliipenda Sana CCM, Nilitamani ningempigia Kura katika uchaguzi ule lakini nilikuwa sijafikia umri wa kupiga kura, hivyo nikaishia kuwaambia watu wampigie kura Rais kikwete aliyeonyesha moyo wa upendo kwetu wananchi Hadi kuamua kukaa na kusimama nasi juani licha ya kuwekewa kimvuli. Nikutokea hapo nimekuwa mtafuta Kura za CCM popote pale. Ni kutokea hapo sijawahi kujuta kuwa mwana CCM. Wala sijawahi kuacha kuisemea CCM mahali nilipo. Ni kikwete Ndiye Aliyenishawishi kuipenda CCM maana niliona Ni chama kinachowajali wananchi na kuguswa na shida zao na kuwa na Sera na ajenda zinazogusa maisha ya watanzania.
Asante Sana mh kikwete kwa kunifanya kuipenda siasa na CCM kwa ujumla,Asante kwa kutujengea shule za kata ambazo Mimi Ni mnufaika nazo na nimefaidika na kupata Elimu kupitia juhudi zako ,Asante kwa kunipatia mkopo wa Elimu ya juu ulionisaidia kutimiza Ndoto zangu za kupata Elimu ya juu licha ya kuwa nimetoka familia masikini,Asante kwa kulitumikia Taifa letu kwa uzalendo mkubwa na kwa demokrasia ya Hali ya juu sana,.
Kazi Iendeleee , mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627