King junior
Member
- Apr 8, 2011
- 63
- 12
Wanafunzi wanaosomea ualimu kitivo cha elimu Udom wapo mbioni kugoma.
Tukio limeanza jana baada ya kubandika matangazo ya mkasanyiko wa wanafunzi wote katika moja ya mabwalo ya wanafunzi (BLOCK F). Mnamo saa tatu usiku, wanafunzi zaidi ya elfu moja walikusanyika na kuanza kujadili hoja zenye mashiko na za msingi kuhusiana na kero mbali mbali zinazowakera wanafunzi hao, lakini moja lililopewa kipaumbele zaidi ni kucheleweshewa pesa za kujikimu (BOOM).
Kimsingi utaratibu huu mpya wa utoaji mkopo hadi wanafunzi wasaini umeonekana kuwa kero kwa kuwa uongozi wa chuo unatumia fursa hiyo kuchelewesha pesa hizo kwa wanafunzi.
Kwa taarifa za uhakika cheki ya malipo kutoka bodi ya mkopo ilifika tarehe 17/12/2011, ambapo malipo yalitakiwa kuanza tarehe 20/12/2011 lakini imekuwa tofauti.
Hadi leo nawasilisha mada, pesa haijaingia, huku kukiwa hakuna matumaini kuwa watawaingizia lini ingawa kwa taarifa ya waziri wa mkopo, ni kwamba kuanzia ijumaa ya tarehe 6/01/2012 ndio malipo yanaanza kufanyika.
Tukio limeanza jana baada ya kubandika matangazo ya mkasanyiko wa wanafunzi wote katika moja ya mabwalo ya wanafunzi (BLOCK F). Mnamo saa tatu usiku, wanafunzi zaidi ya elfu moja walikusanyika na kuanza kujadili hoja zenye mashiko na za msingi kuhusiana na kero mbali mbali zinazowakera wanafunzi hao, lakini moja lililopewa kipaumbele zaidi ni kucheleweshewa pesa za kujikimu (BOOM).
Kimsingi utaratibu huu mpya wa utoaji mkopo hadi wanafunzi wasaini umeonekana kuwa kero kwa kuwa uongozi wa chuo unatumia fursa hiyo kuchelewesha pesa hizo kwa wanafunzi.
Kwa taarifa za uhakika cheki ya malipo kutoka bodi ya mkopo ilifika tarehe 17/12/2011, ambapo malipo yalitakiwa kuanza tarehe 20/12/2011 lakini imekuwa tofauti.
Hadi leo nawasilisha mada, pesa haijaingia, huku kukiwa hakuna matumaini kuwa watawaingizia lini ingawa kwa taarifa ya waziri wa mkopo, ni kwamba kuanzia ijumaa ya tarehe 6/01/2012 ndio malipo yanaanza kufanyika.