Udini umeharibu mambo

Udini umeharibu mambo

BIN BOR

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2010
Posts
1,013
Reaction score
407
Anitha ni mkatoliki lakini alipata mchumba mlokole aitwae Marko. Wazazi wa Anitha wakasema hawatakubali Marko amwoe Anitha hadi kwanza abadili dhehebu. Anitha akaanza kumbembeleza Marko kwa taabu maana walokole nao wakakataa kijana wao kuwa mkatoliki. Lakini penzi likakolea na baada ya miezi 3 akakubali kuwa mkatoliki. Marko akaanza mafundisho na siku ya komunio wazazi wa Anitha wakamzawadia gari kama matayarisho ya mume wa binti yao.

Siku moja kama baada ya miezi 2 hivi, Anitha alirudi nyumbani na machozi tele akaanza kugala gala chini.

Wazazi : Anitha vipi tena, umepatwa na masaibu gani?

Anitha : Marko hatanioa tena!

Wazazi : Kwa nini asikuoe wakati anaendelea vizuri na ukatoliki? Amepata komunio na kipaimara kama tulivyotaka! Amekuwa mkatoliki kweli kweli siku hizi.

Anitha : Hilo sasa ndio tatizo wazazi wangu!

Wazazi : Tatizo kivipi wakati amebadili dhehebu ili akuoe wewe?

Anitha : Ameamua kuwa padre........
 
Duuuu..u! Hii ya ukwel ila kosa co la marko ni lawazaz wake anitha duu!
 
mh kwa katoliki huwi padre kienyeji namna hiyo ndugu yangu
 
Nilifikiri ni mambo ya uongozi wa awamu ya 4 na udini kumbe ni utani?
 
ni kweli upadri si mchezo kwa komunio na kipaimara tu

Watu wa bongo kama wewe una lack sense of humor.........if it isn't a joke for you, just leave the forum silent to let the ones who understands it continue with their laughter. Hamuweki jokes! Watu wakiweka jokes mnaanza kujadili philosophy from joke words.....mtakua lini?
 
Watu wa bongo kama wewe una lack sense of humor.........if it isn't a joke for you, just leave the forum silent to let the ones who understands it continue with their laughter. Hamuweki jokes! Watu wakiweka jokes mnaanza kujadili philosophy from joke words.....mtakua lini?
Punguza jazba!
 
Watu wa bongo kama wewe una lack sense of humor.........if it isn't a joke for you, just leave the forum silent to let the ones who understands it continue with their laughter. Hamuweki jokes! Watu wakiweka jokes mnaanza kujadili philosophy from joke words.....mtakua lini?
kijana umeninukuu vibaya mbona sijatukana thread yako nimeikubali fresh tu soory if nimekuudhi but haikua lengo langu kukukatisha tamaa
 
Tumsifu YESU KRISTO baba paroko PADRE MARKO....teh teh teh teh teh teh
 
Ni joke nzuri, nimeifurahia! Lakini nasikitika title yake haiendani na hadithi yenyewe. Labda kama sielewi vizuri tafsiri ya udini.

Everything done purposely, you are falling in a trap....
 
Hili ni fundisho kwa vijana hasa wa kike wasidanganyike kwa mvulana kubadili dini au dhehebu amuoe huo ni utapeli tu wanangu semeni hatudanganyikiiiiiiiii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom