Udhaifu wa viongozi wa Kiafrika

The Bliss

JF-Expert Member
Oct 16, 2021
213
435
Yawezekana viongozi wetu wa kisiasa wanashindwa kutatua matatizo yanayowahusu wananchi kwa sababu mbili: Moja, hawana uwezo mzuri wa kufikiri na kutatua matatizo (Upeo wa akili zao ni mdogo).

Mbili, hawataki kutatua matatizo kwasababu matatizo ya wananchi ni fursa ya wao kuendelea kupata nafasi za uongozi ( Ulafi wa madaraka).

Kwa kuanza na sababu ya kwanza. Ni ukweli usiopingika kwamba viongozi wengi wa kiafrika hawako smart in problem solving. Wengi wao hawana uwezo mzuri wa kubuni mbinu za kuondoa tatizo badala yake huwa wanaondoa tatizo dogo kwa kuleta tatizo kubwa. Rejea ongezeko la tozo na mfumko wa bei Tanzania. Viongozi wengi hawana sifa za uongozi bali wanabebwa na historia za wazazi, ndugu , jamaa na marafiki ambao kipindi cha nyuma walibahatika kushika nafasi za uongozi katika nchi lakini kiuhalisia hawana sifa za uongozi na utendaji ambao unaweza kulitoa taifa hili sehemu ya chini na kwenda juu. Pia elimu za viongozi wengi wa kisiasa zimekuwa za kutiliwa mashaka na jamii kutokana na jinsi zilivyopatikana au kwasababu wanashindwa kutafsiri elimu zao katika mazingira halisi. Rejea baadhi ya PhD za viongozi wengi wa Tanzania.

Viongozi wengi hawana muda wa kujua matatizo halisi ya wananchi wao kwasababu ya historia za makuzi yao kwasababu wengi wamekulia kwenye maisha safi yasiyokuwa na shida kabisa. Kwahiyo kuonja maisha ya mtu anayekunywa maji katika bwawa moja na Ng'ombe inakuwa ngumu sana, kuonja maisha ya mtu anaesoma katika shule yenye walimu wawili au wanne haimuingii akilini, kuonja maisha ya watu wanaokosa huduma za afya hawezi kuelewa kwa uhalisia, kuonja maisha ya vitu kupanda bei hawezi kuonja uhalisia kwasababu hata vocha za mawasiliano wanapewa na serikali, gari za kutembelea pamoja na posho za kusinzia na kupiga makofi bado wanazipata. Hivyo basi inakuwa ngumu kukua kiakili na kupata mbinu na muamko wa kutatua matatizo ya wananchi. Rehejea maamuzi ya mawaziri na baadhi ya watendaji wa serikali.

Najaribu kufikiria pia katika mlengo wa nadharia ya pili kwamba endapo viongozi wetu hasa wa kisiasa wakitatua matatizo ya uhaba wa maji safi na salama, umeme wa uhakika, huduma za afya, miundombinu za barabara, elimu na usalama wa raia na mali zao, ajira hivi watajinadi kufanya nini wakati wa kampeni za kuomba nafasi za uongozi? Jibu ni kwamba hawatakuwa na chakuongea. Kwasababu wananchi watakuwa hawahitaji tena kutatuliwa shida za ugumu wa maisha bali wanahitaji kuambiwa kuhusu advanced economy, technology and world domination kitu ambacho viongozi wengi wa kiafrika hawawezi kukifanya. Rejea issue za PayPal, crypto currency, price za internet bundles.

Viongozi wetu wa kiafrika wamewekeza kwenye matatizo ya wananchi wao kama mitaji yao ya kisiasa hivyo basi kuondoa changamoto za wananchi katika jamii zao ni kujikosesha nafasi za uongozi kwasababu hawana cha kutoa katika jamii zaidi ya kuahidi kutatua matatizo yaleyale kila mwaka.

Hitimisho: Ukitaka kumtawala kwa urahisi binadamu basi mnyime elimu bora. Ukitaka binadamu akutii basi mfanye awe mnyonge kupitia njaa kisha mpe chakula kidogo kidogo.
 
Umaskini na ujinga wa WaTz, ndio mtaji wa CCM, na sio adui kama ikivyobainishwa miaka iliyopita.
 
Lakin pia tukisema wagombea wawe na degree, bado mtaanza kulalamika kwamba elimu sio kigezo cha kuwa uongozi.

Waafrika, tushazoea kulalamika
 
Matatizo wanayajua vizuri sana tena wengine wamefanyia tafiti ngazi ya master, PhD na katika mashirika ya ndani na nje kama UNICEF, twaweza, UNIDA Universities nk.

Uwezo wa kutatua matatizo unategemea uwezo wa uzalishaji mali.

Uzalishaji wa Africa soko lipo ulaya ambao wazungu wachina,wahindi hupanga bei ya kununua bei wanayoitaka wao kisha kutuuzia vifaa vya kutatua matatizo kwa bei kubwa sana.

Jiulize gari mpya ya halmashauri inanunuliwa shilingi ngapi, je ili ulinunue hilo gari inakubidi uuze tani ngapi za pamba au kahawa au gesi.

Viongizi wa Africa wamezidiwa akili/ujanja na wazungu katika fair/win win bussiness, hivyo wanakosa pesa za kuweza kutatua matatizo sio kwamba hawana akili au uwezo au hawatatambui matatizo bali wazungu ni wajanja kuwazidi.

Jambo lingine ni kuendeleza rushwa ndogo ndogo kwa manufaa yao binafsi na kujali vyama kuliko wananchi. Jambo lolote nje ya chama kinachotawala Africa halipokelewi.

Hata hivyo mimi naona kuna mabadiriko kiasi kwa viongozi wetu kuanza kutatua matatizo sugu japo kasi ni ndogo. Mfano sasa hivi vijiji vingi vina umeme, maji, zahanati mitandao ya simu.

Tukumbuke Africa ina natatizo mengi na sugu,wananchi nao wamelala kwani husubiri mpaka serikali ije itatue matatizo wanayoweza kuyatatua mfano kujenga zahanati, darasa,vyoo ipo katika uwezo wa wananchi ila kuajiri watumishi hawawezi. Hivyo LAWAMA ziende kote kote.
 
Matatizo wanayajua vizuri sana tena wengine wamefanyia tafiti ngazi ya master, PhD na katika mashirika ya ndani na nje kama UNICEF,twaweza, UNIDA Universities nk.

Uwezo wa kutatua matatizo unategemea uwezo wa uzalishaji mali.

Uzalishaji wa Africa soko lipo ulaya ambao wazungu wachina,wahindi hupanga bei ya kununua bei wanayoitaka wao kisha kutuuzia vifaa vya kutatua matatizo kwa bei kubwa sana.

Jiulize gari mpya ya halmashauri inanunuliwa shilingi ngapi, je ili ulinunue hilo gari inakubidi uuze tani ngapi za pamba au kahawa au gesi.

Viongizi wa Africa wamezidiwa akili/ujanja na wazungu katika fair/win win bussiness, hivyo wanakosa pesa za kuweza kutatua matatizo sio kwamba hawana akili au uwezo au hawatatambui matatizo bali wazungu ni wajanja kuwazidi.

Jambo lingine ni kuendeleza rushwa ndogo ndogo kwa manufaa yao binafsi na kujali vyama kuliko wananchi.Jambo lolote nje ya chama kinachotawala Africa halipokelewi.

Hata hivyo mimi naona kuna mabadiriko kiasi kwa viongozi wetu kuanza kutatua matatizo sugu japo kasi ni ndogo. Mfano sasa hivi vijiji vingi vina umeme, maji, zahanati mitandao ya simu.

Tukumbuke Africa ina natatizo mengi na sugu,wananchi nao wamelala kwani husubiri mpaka serikali ije itatue matatizo wanayoweza kuyatatua mfano kujenga zahanati, darasa,vyoo ipo katika uwezo wa wananchi ila kuajiri watumishi hawawezi. Hivyo LAWAMA ziende kote kote.
Asante sana umeeleza vizuri
 
16402654753460.jpg
 
Napenda sana mada positivr kama hizi aisee.

Na mimi naomba nichangie kwa kusema kwamba suala la changamoto kutokutatuliwa kunachangiwa na mambo mengi sana na mawili ndio umetaja ila nyuma ya pazia yapo mengi.

Kuna upande wa serikali ama vipngozi kuna mapungufu yao miongoni mwayo umeyataja hayo.

Alafu kuna upande wa wananchi ambako nako hali ni mbaya,hawajaamka na kuchukua majukumu yao kisawasawa,wanashabikia vyama badala ya maendeleo,wanasubiri kila kitu kitoke serikalini n.k

Wananchi wanao wajibu wa kuandaa mipango mbalimbali ya kujinasuua katika matatizo yanayowakumba, wananchi waandae mipango mikakati waandae programs ambazo zinaelezea plan zao juu ya kutatua changamoto za maji,waandae program zenye plan za kutatua changamoto za umeme, sio wanakuja watu wanafanya mambo bila kuwashirikisha wananchi wa eneo husika mwishowe mipango inakuwa sio endelevu kabisa.

Wananchi wanakosa maji je wananchi wameandaa mpango gani kuhakikisha wanaliendea suala hili na kutatua changamoto ?

Wananchi na sisi tunao wajibu pia wa kuhakikisha tunapiga hatua fulani kutatua changamoto kisha serikali inaaendelea na hatua kadhaa kumaliza changamoto hizo.

Mabadiliko yanahitajika kwetu sisi na viongozi,kila mmoja anao wajibu
 
Napenda sana mada positivr kama hizi aisee.

Na mimi naomba nichangie kwa kusema kwamba suala la changamoto kutokutatuliwa kunachangiwa na mambo mengi sana na mawili ndio umetaja ila nyuma ya pazia yapo mengi.

Kuna upande wa serikali ama vipngozi kuna mapungufu yao miongoni mwayo umeyataja hayo.

Alafu kuna upande wa wananchi ambako nako hali ni mbaya,hawajaamka na kuchukua majukumu yao kisawasawa,wanashabikia vyama badala ya maendeleo,wanasubiri kila kitu kitoke serikalini n.k

Wananchi wanao wajibu wa kuandaa mipango mbalimbali ya kujinasuua katika matatizo yanayowakumba,wananchi waandae mipango mikakati waandae programs ambazo zinaelezea plan zao juu ya kutatua changamoto za maji,waandae program zenye plan za kutatua changamoto za umeme,sio wanakuja watu wanafanya mambo bila kuwashirikisha wananchi wa eneo husika mwishowe mipango inakuwa sio endelevu kabisa.

Wananchi wanakosa maji je wananchi wameandaa mpango gani kuhakikisha wanaliendea suala hili na kutatua changamoto ?

Wananchi na sisi tunao wajibu pia wa kuhakikisha tunapiga hatua fulani kutatua changamoto kisha serikali inaaendelea na hatua kadhaa kumaliza changamoto hizo.

Mabadiliko yanahitajika kwetu sisi na viongozi,kila mmoja anao wajibu
Changamoto ni kwamba serikali inakusanya kodi nyingi, vitu vinapanda bei sana kiasi kwamba hata wananchi wanakuwa busy kutafuta mahitaji muhimu tu pia wakitaka kufanya project kwa mfano kuna baadhi ya maeneo wananchi huamua kujenga barabara lakini mwisho wa siku serikali hai support wakati inawakamua kodi kila kukicha.
 
MaCCM yakiomba yapewa pasi ya kuongoza nchi mwaka 1961, lakini ona nini kimetokea baada ya kupata pasi hiyo kwa bahati mbaya😁😁😁
 
Back
Top Bottom