Udhaifu Wa JK: Tafsiri Yangu

Udhaifu Wa JK: Tafsiri Yangu

I wish tungekuwa tunajadiliana hivi kila mara.

Nimepata mawili matatu kutoka kwako lakini nami nakupa assignment,nina miaka 50+ na vita ya Uganda nilikuwa Musoma na kuziona ndege mbili za kwetu zikitunguliwa na mizinga yetu na ilikuwa graduation ya Musoma alliance School.

Uhujumu uchumi ndo tuliohusika kulinda mawaziri na ofisi za serikali na vile vile kupakua behewa la vinywaji vikali hapo Railway ambapo wengine walikunywa mpaka kulazwa hospitali,je mimi ni wa lini?Ilikuwa ndo mara yangu ya kwanza kuona TV na ilkuwa imetupwa karibu Oysterbay Police.

Nimefurahishwa sana na uungwana wako katika kuchangia tuendelee hivi.
 
Wanadamu tunapaswa kuhukumu dhamira ya mtu na si matokeo. Bado namwona JK kama kiongozi mwenye dhamira njema kwa nchi yetu

Waandishi kama wewe ni hatari kwa ustawi wa jamii na maendeleo yake.Natumai haya maneno unayoyapamba hayatoki rohoni na si kwa nia njema isipokuwa njaa na ili watoto wapate kula!
Ni vigumu kumshawishi mtu anayefikiri sawa sawa kukubali Jk aliwasamehe wezi wa Pesa za umma kwa nia njema!


By Sn2139

Mkuu Mig hapo umedadavua vyema kabisa na umenifurahisha sana ndugu yangu.. lakini ulichosema hapo chini ...


Nakupongeza kwa kuafikiana na Mjengwa. Mimi sikuafikiana naye. Mimi na wewe tunatofautiana. Sisi ni watu wawili wenye mawazo huru lakini akili zetu zinahifadhi models tofauti inapofika wakati wa ku-analyse mambo mbalimbali.

Hoja uliyoichomeka juu ya udhaifu wa mfumo ni mjadala tofauti na mrefu. Kinachonishangaza mara kwa mara ni namna mijadala inayomhusu Mh Dr Kikwete kupindishwa na kuelekezwa kwa vitu au watu mbadala ili kumnusuru na kumsaidia kuepa lawama na laana za watu. Naona anawatumia vizuri sana watetezi wake. Kumbuka kuwa, tumekuwa tukisikia mara nyingi :
(1) Rais Kikwete ni kiongozi msikivu lakini wasaidizi wake ndio wanaomwangusha! Hapo amesafishwa kwa hoja dhaifu kabisa!
(2) Rais Kikwete sio dhaifu ila mfumo uliopo ni dhaifu na ameurithi toka awamu ya kwanza! Hapo tena ametakaswa!
(3) Rais Kikwete ndiyo kiongozi pekee aliyeweza kuchukuwa maamuzi magumu kuwafikisha katika vyombo vya sheria mafisadi! Hapo tena amekuwa hero na shupavu! Huu ni usanii tu...watu wanataka kuhadaa watoto waende kulala usingizi.

Mfumo huu anaotumia Mh Kikwete, ndio aliotumia Mkapa, ndio aliotumia Al~Hajj AH Mwinyi, ndio aliotumia Mwenyeheri JK Nyerere, je unadhani hawa nao walionesha udhaifu wa kiuongozi kama tunaouona kwa Col Kikwete? Fafanua ukizingatia matukio yafuatayo:
(i) Ndege ya kijeshi kutua nchini na kuondoka na wanyama hai bila kipingamizi chochote
(ii)Wezi wa pesa ya EPA kuombwa kurudisha pesa kwa hiari na bila kufikishwa mahakamani
(iii)Orodha ya wafanya biasha ya madawa ya kulevya kufikishwa kwa rais na yeye kukaa nayo miaka 7 bila hatua yoyote
(iv)Richmond: Kikwete.. "simjuwi mmiliki"...Lowasa: "Unakumbuka nilikupigia simu ...ili nisitishe mkataba lakini ukanizuwia.."
(v) Luhanjo, Jairo, etc
Mkuu asante kwa hoja naona nikikupa like haitatosha
 
I wish tungekuwa tunajadiliana hivi kila mara.

Nimepata mawili matatu kutoka kwako lakini nami nakupa assignment,nina miaka 50+ na vita ya Uganda nilikuwa Musoma na kuziona ndege mbili za kwetu zikitunguliwa na mizinga yetu na ilikuwa graduation ya Musoma alliance School.

Uhujumu uchumi ndo tuliohusika kulinda mawaziri na ofisi za serikali na vile vile kupakua behewa la vinywaji vikali hapo Railway ambapo wengine walikunywa mpaka kulazwa hospitali,je mimi ni wa lini?Ilikuwa ndo mara yangu ya kwanza kuona TV na ilkuwa imetupwa karibu Oysterbay Police.

Nimefurahishwa sana na uungwana wako katika kuchangia tuendelee hivi.
Mkuu Mig mimi pia nashukuru kwa uungwana wako na uwezo wako wa kuyapokea mawazo ya wenziyo hata kama wewe ni mzee wa miaka 50+

Taifa letu lipo kwenye kipindi kigumu, kibaya na cha hatari kuliko kipindi cha vita ya Kagera. Hizo ndege mbili zilizodunguliwa kule Musoma ni mvua za manyunyu.. sasa hivi kuna ndege zaidi ya mara 2 mara 10 zinazodunguliwa kila siku na hazitangazwi. EPA ilidungua ndege ngapi? Dowans/Richmond ni sawa na ndege ngapi mkuu? Rada je? ....

Karibu kwa mijadala zaidi na ubarikiwe sana mkuu
 

Maana, tumefika hapa kutokana na mfumo dhaifu unaozaa Serikali dhaifu, unaozaa Bunge dhaifu na unaopelekea pia kuzaa vyama dhaifu vya siasa ikiwamo chama tawala. Na chimbuko lake ni Katiba ya Nchi iliyo DHAIFU. Ndio, tatizo la nchi yetu ni tatizo la kimfumo. [\QUOTE]

Hapo natofautiana na wewe. wakati wa awamu ya kwanza ya Nyerere, kilichokuwa kinatuongoza ni IDEOLOGY, siyo KATIBA. kulikuwa na misingi inayotuongoza: Azimio la Arusha. kulikuwa na miiko ya uongozi. sasa hivi hivyo vyote havipo, na mbaya zaidi, hakuna kilichowekwa badala yake. tunalia ufisadi, lakini mfumo wetu umeruhusu viongozi wafanye wanavyotaka. mfumo huo haujawekwa na Nyerere, ila mfumo uliokuwepo wakudhibiti uliondolewa na CCM ya Mwinyi na kuweka mfumo wa sasa, ulioastawishwa na CCM ya Mkapa. sasa ukisema tu kwa ujumla matatizo yameanzia kwa Nyerere yamekuja mpaka leo na kusababisha JK awe hivyo, hapo unatuhadaa.


Afrika Rais anategemea sana wasaidizi wake katika kuifanya kazi yake. Hivyo, mfumo dhaifu huzaa wasaidizi dhaifu pia. [\quote]

Marais na watawala wengine wote wanategemea wasaidizi wao. Nyerere alikuwa na wa kwake, akiwemo yule mama wa Kiingereza, Joan Wickens. tatizo ni kwamba Rais ndiye anaamua asaidiwe na nani, na anaweza kusaidiwa tu kama yeye anajua anatoka wapi anakwenda wapi, na kama ana msimamo unaoeleweka na madhubuti. ni rahisi sana kusingizia wasaidizi, kama Nyerere alivyoweza kumtupia Rashid Kawawa abebe lawama mambo yanapokuwa magumu. hiyo ni mbinu tu ya kisiasa, lakini ukweli unabaki Rais atahukumiwa kwa vision aliyonayo, mikakati anayoiweka kutekeleza vision hiyo.

Ni kweli mfumo dhaifu unazaa viongozi dhaifu, lakini naamini hata sasa hivi tunao watu makini wengi tu ambao wangeweza kutusaidia kwenda kule tunakotaka. kama wote tungekuwa dhaifu nani angeona haya tunayoona? viongozi wetu wapo nyuma zaidi kuliko wananchi wao. wamelewa na kuwa vipofu. tunahitaji mabadiliko makubwa jinsi ya kuendesha nchi yetu. hii itatokea pale tutakapopata critical mass ya wananchi wanaodai mabadiliko na wapo tayari kuyasimamia.

Naam, tunaweza kuondokana na mfumo dhaifu kupitia Katiba mpya ijayo. Inawezekana.[\quote]

Sina matumaini makubwa namna hiyo juu ya hicho kianchoitwa "katiba mpya". sababu umeitoa mwenyewe: kwa kuwa mfumo huu wa kifisadi na kidhaifu ndio unaosimamia zoezi la kuandaa katiba mpya, ni dhahiri tutapata KATIBA DHAIFU MPYA. tunachohitaji kwanza kabisa ni muafaka wa kitaifa juu ya hatma ya nchi yetu. tunahitaji kujua misingi inayotuongoza. hii ndio itatusaidia kuandika katiba mpya kwelikweli, ambayo itatupeleka huko tunakotaka. hii katiba ya Warioba itatupeleka wapi? ni dhahiri maoni yatatolewa lakini kitakachotokea ni yale yanayohitajiwa na watawala walioko katika mfumo huu dhaifu.

 
Back
Top Bottom