Udhaifu Wa JK: Tafsiri Yangu

Maggid, with due respect, everyone perceive various issues in this world basing on his/her point of reference. Kwangu mimi, kwa kuwa katiba inampa madaraka makubwa sana Rais basi ni lazima taasisi ya urais ionyeshe uhai na kuwa on top of issues.

Kila kitu kinaenda kwa ghasia sasa hivi na tupeane sifa kwasababu ya uhuru wa kutoa maoni bila kujari watu hawali na maisha yanakuwa magumu siku hadi siku? Putin pamoja na ubabe wote alionao,awamu yake ya kwanza kama rais wa Russia alihakikisha anatumia natural resources za Russia, ikiwemo gas na mafuta kuwapa watu wake mkate wa kutosha wa kila siku. Kumbuka kabla ya Putin, enzi za Yetsin maisha yalikuwa ni magumu sana Russia. Hivi unafahamu pamoja na udikteta wake Putin alipata kupendwa sana siku hizo?

Times change kwahiyo sijui sasa hivi itakuwaje...ninachotaka kusema ni kuwa Rais ahakikishe watanzania kwanza...hata kama wavivu na magoigoi, na wasiojua kusoma, lazima itumike mbinu mbadala ya kubadili muonekano wa mambo. Tunajisikiaje kila siku hela ya walipa kodi inapoingizwa TRL, ATCL na halmashauri za wilaya zetu halafu zikaishia kuliwa tu???
Vinginevyo kama wewe unavyoona uko sahihi, na MNYIKA pia anaona yuko sahihi....
 
MHESHIMIWA MBONA NA WEWE unatukana. hata mavuvuzela pia yana umuhimu wake pale mechi inapopamba moto. siasa za tanzania zimepamba moto pia lazima wawepo watu wa aina hiyo lakini kutukna c vema wacha wananchi waseme maana wangewakataa wasingefika mbali hivo kuwatukana pia unatukana wananchi
Tanzania ina watu milioni zaidi ya 40 na mimi ni mmoja wao, na hayo ndiyo niliyoyasema.
 
Acheni kuita wananchii wa Tanzania ni dhaifu ili tu kumlinda Rais na viongozi wake katika kuvaa suti hii ya UDHAIFU.
Binasfi kitendo hicho nakiona ni uhuni mkubwa.

Katiba ya nchi, katiba iliyowekwa na wachache wanao dhani wao ndo nchi, inampa Rais wa Tanzania Madaraka makubwa mno ya kufanya chochote atakacho kwa zaidi ya 90% ya maamuzi yake. Pia inampa uwezo wa kimungu wa kutohojiwa kwa nini amefanya alicho fanya na mtu yeyote au chombo chochote kirahisi bila maumivu.

Viongozi wote muhimu ndani ya serikali wanateuliwa na Rais.
Taasisi zote muhimu Tanzania zina mikono yote miwili ya Rais.
Rais hawezi kukataa kuhusika na udhaifu wa taasisi yeyote Tanzania.
Kama kuna ulegevu kiuongozi katika serikali ya Tanzania kiini chake ni Udhaifu wa Rais

Rais mwenye dhamira njema hawezi kuteua watu Maboya kuongoza taasisi yeyote, sembuse taasisi muhimu?
Viongozi wengi wa kuteuliwa ni dhaifu mno kiasi cha kushangaza na kuzusha maswali ni nini kimepelekea Rais kuwateua waongoze taasisi muhimu!!!???

Je ni vyeo vyenye uteuzi wak kichupichupi???
Nimemteua Dr Yusufu Idi Nguruwe ili aongoze ile taasisi ya kuzuia rushwa kwa sababu kijana wa mwisho wa Nyanangu mdogo upande wa hawala yangu wa Kinondoni alizaa na dada yake mkubwa mabinti wawili,mmoja katika hawa mabinti wawili aliwahi kuwa girfriend wa kijana wangu wa nje na mwngine nimezaa naye mtoto mmoja kwa siri.

Huyu Salima Mogola inabidi awe mkuu wa mkoa, si unajua wakati wa kampeni nilikuwa napiga yeye na dada yake kwa mpigo bila wao wenyewe kujua?? Mwenzie imebidi nimpe milioni 100, mtaji wa biashara ya kwenda Dubai, ili kuua soo zima

Huyu Masala Kulangwa inabidi awe balozi kwa sababu, tangu niukwae, amekuwa akintafutia mademu vigoli bomba wa kujirusha nao, Mungu anipe nini?? Gunia la chawa?? halafu ni mtunzaji mzuri sana wa siri na udhaifu wangu


It all about CHUPI

Kwa namna katiba yetu ilivyo, Rais anapewa uwezo wote wa kuonyesha dhamira na utashi wake bila pingamizi.
Rais anapewa uwezo wa kupangua uongozi wote wa kitaifa aliorithi kutoka kwa rais aliyepita.
Rais ana uwezo wa kupeleka Bungeni kurekebisha sheria yeyote inayotoa mwanya wa kuharibu mambo kiutendaji
Rais anauwezo wa kuunda Baraza la mawziri imara hata ikibidi nusu yake kuwa watu wenye hekima ambao ni wabunge wa kuteuliwa.
Rais Tanzania hafungwi mikono yake, hafungwi akili yake hafungwi mdomo wake, hafungwi mawazo yeke wala hafungwi maono yake. U rais wa Tanzania una madaraka yaliyo karibu sawa na yale ya Kisultani.

Ukiona Rais katika joho lake la Urais anjikanya vibaya katika vyombo vya kmataifa repeatitively,kwa mfano anaulizwa swali na mwandishi wa habari wa kimataifa kwa nini nchi yake ni masikini na kuishia kusema I don't even know why!!!!! Unajua wazi kwamba hilo ni jibu lake la kutoka moyoni na ni jibu la uwezo wake wote wa kufikiri na kuchambua mambo.Jibu linalo ashiria moja kwa moja kwamba ni dhaifu na hajui potentials zilizo ndani ya Taifa analo liongoza. Ukiliangalia Tatizo lolote kwa umakini ni lazima upewe fununu za namna ya kulitatua, si kila utatuzi ni rahisi kama kumsukuma mlevi kuna tatuzi nyingi zinazohitaji juhudi za makusudi.

Ukiona Rais anatamani angepata walau $1,000,000,000.00 ndani ya KAPU lake la MATONYA kutoka kwa wahisani wa Dunia ya kwanza kwa mwezi, Eti ili aifanye nchi yake iwe Pepo ya duniani, huku zaidi ya 75% ya vyanzo vya mapato vikiwa havijaguswa kwa ulegevu wake???
Basi ujue rais huyo ni Dhaifu na hajui kwamba ni dhaifu jambo linalo mfanya awe MSUKULE wa Wazungu na Ukoloni mambo leo unaosimamiwa kwa pochi na Makapuni ya kimataifa kama Barick Gold Mine.

Tuna Mbuga nyingi zenye wanyama kibao Tanzania serikali inapata Tshs ngapi kwa mwezi??
Serikali ina dhamira ya kukusanya Tshs ngapi kwa mwezi kutoka katika mbuga hizo? Hakuna mipango na hakuna data za maana kuna Maneno ya mipasho ya Akina Ole Sendeka na Lusinde.
Tuna mlima mrefu kuliko yote barani Afrika, unapandika kiraisi na karibu kila mtu hata wale wenye Udhaifu wa viungo kama miguu. Tunapata Tshs ngapi kwa mwezi kutoka kwenye mlima huu??

Tuna Tanzanite, sisi ni nchi pekee duniani tunaotoa Tanzanite yenye soko la uhakika. Tunakusanya Tshs ngapi kutoka katika Tanzanite?? Tuna dhamira yeyote ya kuboreha ukusanyaji kwa mipango thabidi ya kitaalamu???

Tuna Madini ya Dhahabu. Mikataba tuliyoingia na wachimbaji ambayo Rais Kikwete anaitetea ambayo ni DHAIFU mno na yenye kuonyesha kila Dalili ya Rushwa Dhamira mbaya ya wazi na kutojari ya kumneemesha muwekezaji na kuikosesha mapato serikali. Je ni lini Rais Kikwete atasimama kidete kama Rais na kusema tunapoteza fedha nyingi kwa sababu ya ujinga wa watu wachache sana ndani ya serikali yeye akiwemo?
Tunakosa Mamilioni mngapi kwa uzembe huu wa kijinga?
Rais akitembelea mgodi anapewa zawadi ya kilo kadhaa za dhahabu hiyo si Rushwa ya wazi???

Tuna Natural Gas Nyingi sana inayoweza kutumika kuzarisha umeme na kuondoa kabisa tatizo la umeme wa mgao Tanzania na kuboresha uchumi wa wananchi na nchi kwa ujumla. Rais Kikwete kwa uwezo wote alio rundikiwa kikatiba anafanya nini kuliwezesha hili?
Gas inaweza kumaliza kabisa tatizo la ukosefu wa mbolea Tanzania in less than 5 years. Rais wetu amewahi hata kuota kujenga kiwanda kikubwa cha Mbolea Mtwara?????
Mauzo ya Gas ya ndani na nje ya nchi yakiboreshwa kidogo tu serikai ina chanzo safi cha mapato,rais kikwete anafanya nini kuliwezesha hili???

Kuna Kodi za Bidhaa zinazoingizwa kutoka nje. Zaidi ya asilimia 90% ya bidha na mali ghafi zinazo tumika nchini Tanzania zinaagizwa kutoka nje. Bidhaa hizi hutakiwa kutozwa kodi. Je Rais Kikwete alisha wahi kuwaza kwamba ile Billioni moja anayo ota Wazungu wampe nusu yake imejificha katika kutoza ushuru wa kawaida wa bidhaa hizi???

Dogo Maggid amejitahidi kuandika na kufafanua Udhaifu wa Rais kwa wepesi tu. Kama angezingatia katiba ya nchi na jinsi rais alivyo na uwezo kikatiba na uzembe mwingi wa taasisi za serikali ambazo wakuu wake ni uzao wa utashi na dhamira ya rais mwenyewe; sidhani kwamba angethubutu hata kujaribu kumtetea kimtawanyiko na kumfanya awe mtu wa kuonewa huruma kwamba anadhamira nzuri ila mfumo una let down. Mfumo upi aliousimika mwenyewe?

Rais wetu ana madaraka makubwa mno ajabu kikatiba lakini binafsi kama Kikwete na kama mkuu wa taasisi yake ya Urais ni DHAIFU mno mno. Udhaifu wa Rais Kikwete ni sawa na jogoo aonaye punje 7 za mtama ni bora mara millioni kuliko jiwe la karati 100 la Almasi.
 
Maggid ulivyosema ni sawa. Lusinde, Lema, Wassira, Heche, Slaa, Nape, Nassari, Lowassa na sasa Mwigulu na Mnyika ni typical vuvuzelas.
Mianasiasa ya Tanzania haina respect wala uelewa, sisi watanzania hatutaki ugomvi fanyeni kazi mafala nyie!!

kobello, nimekuelewa vyema sana, ila nini kisa cha kuwatusi waheshimiwa?
 
Last edited by a moderator:
kobello, nimekuelewa vyema sana, ila nini kisa cha kuwatusi waheshimiwa?
Kuna mtindo wa hao waheshimiwa unaowaita, kukejeli na kutukanana mbele za hadhara. Wanadharau watu walio na wasiochaguliwa.
Sasa mimi naona bora nianze kuwatukana na wao halafu tuone kama watarudisha majibu .... hii haijalishi umetoka chama gani. Ukiwaambia sijui watu watashikishwa ukuta au watu fulani wapuuzi,basi na wewe kaa tayari kutoheshimiwa tena naogopa ban, I wish hii ingekuwa yahoo! ambako chochote unachotaka kusema unasema.
 
Maggid,

Kama kawaida inapokuja kwa JK anakuwa kama mgonjwa aliyepigwa sindano ya kulainisha misuli ( muscle relaxant). Halafu anasema " Wanadamu tunapaswa kuhukumu dhamira ya mtu na si matokeo."

Kusema ukweli hii ni statement moja ya kitoto ambayo nimeshawahi kuisikia katika maisha yangu. Dhamira ni kitu ambacho kisicho quantifiable (hakiesabiki) na mtu akitaka kukipima basi majibu yatakuwa tofauti kutoka mtu mmoja mpaka mwingine (subjective). Huyu bwana anasema tusijali matokeo? Haya ni mawazo potofu na finyu kabisa, na ni mawazo kama haya ndiyo yanayofanya watu wa pwani wasiwe na maendeleo. Hii kauli imenichefua kabisa!
k
 
" OUR President is important; but, he is not Tanzania. All of our people organaized together are Tanzania"- (Julius Nyerere, Julai 29, 1985)

Ndugu zangu,
Watanzania wengi hatuna mazoea ya kusoma, hata makala za magazetini ukiachilia mbali vitabu vya taarifa na hadithi. Ndio, tu wavivu wa kusoma.

Kigong'onda ni aina ya ndege. Ndege huyu ana mdomo mrefu na anapenda sana kugongagonga mti kwa mdomo wake. Ndivyo anavyojipatia ridhiki yake.

Lakini, kwa hulka yake ya kugong'onda kila kilicho mbele yake, basi, hata ukimwekea mti wa chuma porini, kigong'onda atahangaika nao mpaka damu zimtoke mdomoni. Ni hulka yake. Kiongozi hapaswi kuwa kama kigong'onda...
MALECELA HANA JIPYA. HUYU KAHSA ZEEKA SANA. Kikwete hebu vunja PCCB, halafu weka mahakamani David Jairo na wiliam LUhanjo. Hakikisha Nizar kalamagi, Chenge na Maige wanakwenda mahakani wakisindikizwa na wezi wa Radda. Hapo utamuumbua Mnyika na Hoja yake. Lakini ukizidi kukaa kimyaa utampatia ujiko kuliko pele alivyowapatia ujiko wabrazil mwaka 1958!
 
Ndg Maggid,
Uhuru wa kuongea ni haki yako na endapo hukuwa nayo basi ulininywa tu na si kuwa umebahatika kuipata sasa.
Katika dunia ya leo hakuna kiongozi anayeweza kusema amefungua milango ya uhuru. Hakuna, kwasababu Mfalme wa Saudia Arabia ambaye si mfalme tu kiutawala bali pia ni mwenye mahusiano ya kidini naye amepingwa achili mbali mikono ya chuma kama wa Gadafi na Mubark kwauchache tu.

Wimbi la mageuzi ya uhuru wa kujieleza halikwepeki na labda JK apewe sifa ya kuilona wakati likija na si kuwa mwerevu wa kulitengeneza.

Sikubaliani na Maggid kuwa hakuna kiongozi aliyefanya mambo mengi kama Jk, kinyume chake ni kiongozi aliyeshindwa kufanya mambo mengi kuliko watangulizi wake. Matahalani, ndiye kiongozi aliyewahi kupinga hatua za bunge kwa mambo yanayolihusu taifa.

Udhaifu wa JK si ule wa kimwili bali kifikra. JK kama Rais ameshindwa kusimamia sheria, taratibu na maadili ya kitaifa kama nitasema kwa uchache. Ni kiongozi anyependa kujificha nyuma ya wenzake na asiyependa kuonekana mbaya kwa kila mtu

Ni kutokana na udhaifu huo ndipo neno 'Ombwe' la uongozi lilipotokea. Ukweli ni kuwa neno Ombwe limesemwa mara nyingi sana, tofauti ni kuwa JJ Mnyika alisema bila haya. Wale wanaosema Ombwe wanasema udhaifu na pengine ombwe ni neno baya kuliko.

Kama unadhani JK ahukumiwe kwa dhamira basi wewe hufai kuwa wakili wake hata kidogo. Hufai kwasababu dhamira ya JK ndiyo inayomhukumu kabla ya hukumu yenyewe. Dhamira ni nuizo la kutenda na nakuhakikishia JK hana hilo.
Nikupe mfano, aliposema pesa za Rada zitarudi na waliohusika watafikishwa mbele ya sheria, dhamira yake ilikuwa kulinda rasilimali za taifa. Alipoketewa orodha ameificha hadi leo, sasa hapo JK alikuwa na dhamira ya kushughulikia tatizo kweli!

JK alisema anadhamira ya kumaliza mgogoro wa muungano, leo muungano umefikia mahali pa kuhasimiana na kuchomana viberiti na JK kakaa kimya! hapo kulikuwa na dhamira kweli!

Orodha ya udhaifu wa JK inaweza kujaza kurasa 999 na hakika ni wakili dhaifu wa mawazo anayeweza kuzichukua karatasi 999 na kuzijengea hoja ya kumsafisha JK.

Hili la Bunge kumtimua Mnyika nakubaliana nawe kabisa kuwa busara haikutumika. Kilichopaswa kufanywa ni kuthibitisha kuwa JK si dhaifu na hiyo ni nafasi adhimu sana CCM wameikosa. Kinyume chake wamemtoa nje Mnyika na sasa hata sisi tusiojua udhaifu wa Rais wetu tumeanza kudodosa na kupata fikra ya pili.

Tatizo ni CCM kuhamaki na kiwewe cha maziko ya chama hivi karibuni. Matokeo yake wanatumia ile mbinu ya kivita inayosema 'shoot any moving object' sasa hapa wanajikuta wakiwa na friendly fire
 
" Wanadamu tunapaswa kuhukumu dhamira ya mtu na si matokeo." Hivi katika nchi yetu tumewahi kupata rais mwenye dhamira safi kama Nyerere? Mbona watu wengi ikiwemo na wewe Majid huwa mnamhukumu kwa matokeo na si dhamira? Majid kwanini unabadilisha kipimo linapokuja suala la JK?

Ukweli ni kwamba, baada ya uongozi wa kibabe wa Mkapa, waTZ walitamani sana kuwa na rais ambaye yupo karibu nao na anayewasikiliza. Ndio maana alipojitokeza JK kugombea, walimpa kura nyingi sana. Kumbe JK hakuwa amejiandaa kuongoza kwa maana ya "vision" na wananchi walipogundua hilo wakaanza kuona ni heri hata ya mbabe aliyetangulia maana maisha yalikuwa afueni.

Pili nashanga kumpa sifa kibao JK kwa suala la katiba "mpya", kama kawaida yetu tumeshasahau kwamba JK alikubali baada ya shinikizo kubwa sana kutoka kwa wapinzani. Yeye mwenyewe hakuwa na mawazo hayo (vision). Tunasifia gari linalopita barabarani na sio tingatinga lililochonga barabara! Tuna uhakika gani kwamba hata hiyo katiba mpya tutaipata? Mbona imeanza kutiwa viraka (e.g. hakuna kujadili muungano)? Naamin kuna suprise kubwa sana huko mbele kuhusiana na katiba mpya. Very likely, haitakuwa tayari by 2015 kwa sababu hakuna dhamira ya dhati ya kutengeneza katiba!

Kuhusu uhuru wa maoni, nyakati zimebadillika sana. Naamin hata Mkapa au "dikteta" Nyerere wasingeweza kuzuia mafuriko ya uhuru wa kujieleza kwa mikono yao! Si tumeona "Arab spring"? Pia Jk ni beneficiary wa uhuru wa maoni na vyombo vya habari, asingekuwa hapo alipo leo kama si vyombo vya habari. Kwa hiyo hawezi "kuuma mkono unaomlisha". JK anavihitaji vyombo vya habari, pengine kuliko vinavyomhitaji yeye!A populist will always embrace the press!
 
Maggid ameeleza mtizamo wake binafsi nawe umetoa maoni na maeneo ambayo unaona yanasababisha JK asipate sifa za Maggid,hapa ndo raha ya mjadala.
.
Mkuu Mig hapo umedadavua vyema kabisa na umenifurahisha sana ndugu yangu.. lakini ulichosema hapo chini ...

Binafsi kama nilivyochangia mwanzoni naafikiana na Mjengwa kuhusu udhaifu wa mfumo lakini nisaidie kuchangia katika uliyogusia.
Nakupongeza kwa kuafikiana na Mjengwa. Mimi sikuafikiana naye. Mimi na wewe tunatofautiana. Sisi ni watu wawili wenye mawazo huru lakini akili zetu zinahifadhi models tofauti inapofika wakati wa ku-analyse mambo mbalimbali.

Hoja uliyoichomeka juu ya udhaifu wa mfumo ni mjadala tofauti na mrefu. Kinachonishangaza mara kwa mara ni namna mijadala inayomhusu Mh Dr Kikwete kupindishwa na kuelekezwa kwa vitu au watu mbadala ili kumnusuru na kumsaidia kuepa lawama na laana za watu. Naona anawatumia vizuri sana watetezi wake. Kumbuka kuwa, tumekuwa tukisikia mara nyingi :
(1) Rais Kikwete ni kiongozi msikivu lakini wasaidizi wake ndio wanaomwangusha! Hapo amesafishwa kwa hoja dhaifu kabisa!
(2) Rais Kikwete sio dhaifu ila mfumo uliopo ni dhaifu na ameurithi toka awamu ya kwanza! Hapo tena ametakaswa!
(3) Rais Kikwete ndiyo kiongozi pekee aliyeweza kuchukuwa maamuzi magumu kuwafikisha katika vyombo vya sheria mafisadi! Hapo tena amekuwa hero na shupavu! Huu ni usanii tu...watu wanataka kuhadaa watoto waende kulala usingizi.

Mfumo huu anaotumia Mh Kikwete, ndio aliotumia Mkapa, ndio aliotumia Al~Hajj AH Mwinyi, ndio aliotumia Mwenyeheri JK Nyerere, je unadhani hawa nao walionesha udhaifu wa kiuongozi kama tunaouona kwa Col Kikwete? Fafanua ukizingatia matukio yafuatayo:
(i) Ndege ya kijeshi kutua nchini na kuondoka na wanyama hai bila kipingamizi chochote
(ii)Wezi wa pesa ya EPA kuombwa kurudisha pesa kwa hiari na bila kufikishwa mahakamani
(iii)Orodha ya wafanya biasha ya madawa ya kulevya kufikishwa kwa rais na yeye kukaa nayo miaka 7 bila hatua yoyote
(iv)Richmond: Kikwete.. "simjuwi mmiliki"...Lowasa: "Unakumbuka nilikupigia simu ...ili nisitishe mkataba lakini ukanizuwia.."
(v) Luhanjo, Jairo, etc

Kikwete ndiye Rais ambaye ameteua Majaji wengi kuliko Rais mwingine yoyote,je hapo amebomoa au amejenga mfumo wa mahakama?
Kuteua watumishi wa serikali na mahakama ni jukumu la rais kwa mujibu wa katiba iliyopo. Kuteua wengi au wachache ni hekima inayoongozwa na mahitaji ya taifa. Siyo hisani ama sadaka. Ni wajibu.

Lakini, je rais amefuata kanuni za uteuzi wa majaji hao wengi kupindukia? Je, falsafa yake katika kutenda hivyo ni nini? Ni kuboresha mahakama kweli? Je matokeo ya uteuzi huo yanaafiki hoja ya uboreshaji wa mahakama? Naomba ufafanue zaidi hoja yako mkuu

Kikwete ametoa uhuru mkubwa mno wa kutoa maoni,baba zangu aliwekwa rumande kwa kuhoji ujenzi wa shule na alichukuliwa kama mpinga maendeleo.BWM alitoka povu wakti wa kujadili report ya Jaji Kisanga na watu tukafikia hatua ya kumshauri Kisanga atangaze kujiuzulu kwani ulikuwa udhalilishaji wa wazi,unaikumbuka hiyo?
Je, huo uhuru mkubwa mno kama ulivyosema:
(1) Unatokana na hisani yake?
(2) Ni ishara ya utawala bora?
(3) umeleta maendeleo zaidi?
(4) Umeleta mazingira ya kuhishimiana zaidi na utengamano kama raia wa taifa moaj?
(5) umeleta manufaa gani? Mimi nilisema mwanzo kuwa uhuru huu ni ishara ya udhaifu wa ki-uongozi wa Col Kikwete. Hakuna uhuru usio na mipaka; yeye ameacha mipaka yote imevunjwa! Ameleta uhuru wa kutapakaa kwa majungu na fitna.. Kama siyo hivyo naomba urudi kufafanua zaidi hapo

Kuhusu baba zako kuwekwa rumande, nawapa pole sana. Je, ulikuwa na umri gani wakati wanawekwa ndani? Je, una hakika baba yako alihoji tu ujenzi wa shule? au kuna jambo la ziada alilofanya na hakutaka kukufahamisha, au wewe hutaki kutufahamisha? Hili naomba liwe kazi ya mahakama kuliamuwa. Ushahidi wa mtu mmoja hauwezi kutowa natural justice kwa pande zote zinazohusika. Kwahiyo hili mimi siwezi kulijadili...

Suala la Judge Kisanga na Mkapa ninalifahamu. Ni hoja nyingine, na inahitaji mjadala mwingine. Wala hoja hiyo siyo utetezi wa udhaifu wa Kikwete..

Katika utawala huu tumeona untouchables wakipanda karandinga la Polisi, member wa Saigon club (kaitafue hii) akisimama Kisutu Mahakamani.
Kwa wana CCM (mimi si mmoja wao) inabidi wamshukuru sana kwani anajua ku pre empty,angalia suala la katiba mpya.Tungekuwa na mhafidhina hii ingekuwa issue ambayo si ajabu damu ingeshamwagika na kwa mtindo huu CCM itaendelea kwa muda.
Nakiri ana mapungufu kama binadamu lakini mfumo una mapungufu zaidi.
Tuendelee kujadiliana

Haya maelezo yako ya mwisho, naomba nikuachie kama zawadi. Sitayagusa kwa sasa. Karibu sana mkuu Mig
 
Kwa tafsiri kama hii ya Maggid, mfalme anaendelea kutembea akiwa uchi hadi anatokea toto tundu! Sasa shuhudia washikaji kama Maggid wanakavyohangaika wakitafuta pa kuficha nyuso kwa aibu, iliwezekanaje wasiuone utupu wa mfalme? Unafiki aah!
 
....Ni kutokana na udhaifu huo ndipo neno 'Ombwe' la uongozi lilipotokea. Ukweli ni kuwa neno Ombwe limesemwa mara nyingi sana, tofauti ni kuwa JJ Mnyika alisema bila haya. Wale wanaosema Ombwe wanasema udhaifu na pengine ombwe ni neno baya kuliko.

Mkuu Nguruvi3, umerusha makonde mazito mno ndugu yangu ha ha haha
Hoja yako ina nguvu za hoja tangu mwanzo mpaka mwisho, lakini hapa umenikuna zaidi..

Ombwe (O) = Dhaifu (D)

Dhaifu liliwahi kutumiwa kwa Rais Hasan Mwinyi

Ombwe limekuja kutumika wakati wa Col Kikwete (K) na kisha kuongezewa na bakshishi ya Dhaifu na mh JJ Mnyika.

Mathematically this implies that K = D[SUP]2[/SUP]

Kama O=2D (yaani Ombwe is stronger than Dhaifu),

basi K = 9D[SUP]2[/SUP]
 
hii tabia ya kushabikia kashfa kwa rais sio nzuri,mnyika amekosea sana yaani.hii iko wazi sema kuna watu wanaokula kwake ndio hawaoni alichokifanya kuwa ni kibaya.ipo namna ya kuwasilisha hisia zako lakini sio kwa njia hii ya mnyika,i real hate it.

hawezi kutudhalilisha sisi marais ivo.
 
:embarassed2:Maana, tumefika hapa kutokana na mfumo dhaifu unaozaa Serikali dhaifu, unaozaa Bunge dhaifu na unaopelekea pia kuzaa vyama dhaifu vya siasa ikiwamo chama tawala. Na chimbuko lake ni Katiba ya Nchi iliyo DHAIFU. Ndio, tatizo la nchi yetu ni tatizo la kimfumo.

Maggid kwa hoja hiyo hapo juu nakubaliana kabisa wala haina ubishi. hili ni sawa kwenye jamii yenu kukiwa na asili ya ulevi huwezi kupata shida sana kufikiri kwanini mwanao au ndugu yako ni mlevi. Guys lets workout for new constitutional.
Unapata picha gani chama tawala na serikali yake kupanda majukwaani na kueleza mafanikio ya kiuchumi wakati national debt inaongezeka....!
Tunatambaa tunajisifu wenzetu wanaotembea na kukimbia wako kimya hawajisifu.
:embarassed2:
 
Kikwete anaonekana dhaifu kwa sababu ametoa uhuru mkubwa wa kutukana na kuropoka.wakati wa mkapa na nyerere haya hayakuwepo na ndio wanaoonekana walikuwa imara.ngoja mie rais wa tano niingie madarakani mtaona.
 
" OUR President is important; but, he is not Tanzania. All of our people organaized together are Tanzania"- (Julius Nyerere, Julai 29, 1985)

Ndugu zangu,
Watanzania wengi hatuna mazoea ya kusoma, hata makala za magazetini ukiachilia mbali vitabu vya taarifa na hadithi. Ndio, tu wavivu wa kusoma.

Kigong'onda ni aina ya ndege. Ndege huyu ana mdomo mrefu na anapenda sana kugongagonga mti kwa mdomo wake. Ndivyo anavyojipatia ridhiki yake.

Lakini, kwa hulka yake ya kugong'onda kila kilicho mbele yake, basi, hata ukimwekea mti wa chuma porini, kigong'onda atahangaika nao mpaka damu zimtoke mdomoni. Ni hulka yake. Kiongozi hapaswi kuwa kama kigong'onda...

Maggid pole sana no matter how much you try to be an apologist for the system and JK in particular; one thing is vividly clear; In the absence of proper institutional systems kama unavyodai!!, the public is yearning for leadership; strong leadership for that matter; the lowest common deneominator is the fact that "kwa nini JK anashindwa kutumia hayo mamlaka ambayo tunayaona kwamba ni excessive kuisimamia serikali ipasavyo!?

Akawashukia mafisadi na wala rushwa vilivyo, akawakamata wauza dawa za kulevya ambao alitamka kule Rukwa kwamba anawajua! akasitisha mikataba mibovu kama Dowans badala ya kuliingiza taifa kwenye malumbano yasiyo na tija akisema "Eti hawajui wamiliki wa Dowans lakini walipwe!!, kweli maggid mabo kama hayo yanakuuingia akilini!?
 
Kwa tafsiri kama hii ya Maggid, mfalme anaendelea kutembea akiwa uchi hadi anatokea toto tundu! Sasa shuhudia washikaji kama Maggid wanakavyohangaika wakitafuta pa kuficha nyuso kwa aibu, iliwezekanaje wasiuone utupu wa mfalme? Unafiki aah!

hahaha.., mkuu umenikosha! kwa hio mfalme kumbe yupo uchi af toto tundu kaona nanilii kaishika ndo magid anaona aibu... hahahahaha..
 
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua matofali yaliyotengenezwa kwa mashine ya Hydrafoam kwaajili ya ujenzi wa madarasa katika shule ya sekondari ya Mboga,wilayani Bagamoyo.


Mashine hiyo yenye thamani ya Shilingi Milioni Sabini 70m/- imetolewa na Rais Kikwete kama msaada kwa vijana waliounda ushirika ili kuboresha maisha yao kwa kufanya miradi mbalimbali ya ujenzi na uzalishaji.
(picha na Freddy Maro)

 
Back
Top Bottom