UDASA wakiri mdahalo wa katiba UDSM ulichezewa rafu na CCM

Dec 11, 2010
3,321
6,328
Wakuu.

Jumuiya ya wanataaluma wa chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) wamekiri kupitia kwa aliyekuwa moderator wa mdahalo ambaye ni mhadhiri wa chuo hicho kuwa mdahalo walio uandaa kuhusu mchakato wa katiba ulihujumiwa na CCM kwa kukodi vijana kutoka mitaani kuja chuo kikuu kushangilia na kupiga makofi.

Mdahalo ule uliharibiwa na CCM ikiwa ni pamoja na kuwapendelea makada wa chama hicho kutoa michango yao kuliko hata wanataluma wabobezi walio hudhuria kongamano lile na hivyo nafasi ya UDASA kupokwa na CCM mpango ambao ulipangwa mahususi kujenga taswira kuwa jumuiya ya chuo kikuu iko pamoja na ccm na hivyo wanakubaliana nao kwenye mchakato wa katiba mpya.

Tafsiri ya makala hiyo...

Kwenye bandiko hapo chini jumuiya ya wanataaluma wa chuo kikuu cha Dar es salaam (UDASA) kupitia kwa katibu wake Bwana Faraja Kristomus ameliambia gazeti la "The Citizen" kuwa makada wa CCM waliuhujumu mdahalo wao kwa kuwaingiza/kupenyeza vijana wa kukodi (waliolipwa) kutoka mtaani ili kuharibu michango ya baadhi ya washiriki.

Bwana Faraja amekiri kwa kusema ni kuwa "...Ni kweli mkutano ule wa mdahalo ulivamiwa na vijana ambao hawakualikwa ambao walilalamikiwa kuwa walikodiwa na wanasiasa..."

Ufafanuzi wa Bwana Faraja unakuja baada ya kusambaa kwa habari kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusiana na kilicho gubika tukio la jumapili lililotawala na kuzomea, vurugu za kushangilia na hatimae kutoka nje.

UDASA ililalamikiwa kama chambo cha kukisaidia chama tawala kusonga na ajenda yake ya muundo wa muungano wa serikali mbili kinyume na matakwa ya umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA).

Bwana Faraja anasema kwamba "...jumuiya yao haikujua mipango ya CCM mapema na walikuja kujua kabla ya kuanza kwa mdahalo ulio jadili nini kifanyike ili nchi ipate katiba yake mpya...". Mawaziri Stephen Wassira, Prof Anna Tibaijuka na William Lukuvi pamoja na Mwigulu Nchemba walihudhuria na kuzungumza.

"...Tulishtushwa na kundi la vijana walioshushwa kwenye mabasi ya UDA kwenye eneo...waliingia ukumbi wa Nkurumah mapema saa nne asubuhi..." alidhibitisha pia kuwa, vijana walio shushwa walionekana wakigawana fedha walizopewa.

Mheshimiwa Lukuvi ambae pia alikuwa mgeni rasmi na miongoni mwa vigogo wa CCM walio hudhuria alipo ulizwa akasema "...hakujua kuwa watu walisombwa au kukodiwa ili wahudhurie.."

"...niikuwa Dodoma kuhudhuria vikao nilipo alikwa na wahadhiri kuhudhuria mdahalo, sikupokea mualiko wowote kutoka CCM na kwa kweli nilishangaa kukuta wanachama wa CCM wamehudhuria..." amesema.

Ripoti zina sema vijana waliokodiwa kutoka maeneo mbalimbali ya Dar es salaam walilipwa kati ya shilingi elfu 50 na kada wa umoja wa vijana wa chama hicho tawala.

Kazi kubwa ilikuwa kuzomea yoyote aliyetoa mchango kuunga mkono UKAWA kuhusu katiba mpya, kikundi hicho kilipaswa kushangilia hoja za mjadala kutoka kwa viongozi wa CCM waliotoa maoni yao kwenye mdahalo huo.

--Nimejaribu kuitafsiri makala hiyo kwa kiswahili ili kuzidi kukazimia maarifa na kuonyesha obwe (vacuum) lililoko kwenye jumuiya iliyoheshimika na kuwa kitovu cha fikra mbadala enzi hizo tungali makinda.

Mtakumbuka siku ile ile mara tu baada ya mdahalo niliweka status hapahapa kulaani mdahalo ule ambao UDASA walitumika kama mhuri wa CCM huku wanazuoni kama Dr Lwaitama na Prof Sheriff uwepo wao ukionewa kinyaa.

Jisomee yaliyo andikwa kwenye makala hiyo hapo chini.
 

Attachments

  • 1407500833691.jpg
    1407500833691.jpg
    83.8 KB · Views: 1,994
Maintarahamwe wanajua fika hawana hoja kwenye mambo yote muhimu nchini ikiwemo hili la katiba mpya. Hivyo popote pale watakapohudhuria kwenye mjadala muhimu ni lazima wafanye hila ili kujaribu kuuteka mjadala au kuuharibu kwa minajili ya kujionyesha wameshinda mjadala huo.


 
CCM ni chama cha kigaidi sawa na Hamasi walivyoiteka Palestina, ISIS wanavyoteka Syria na Iraq, Alshabab Somalia , na mengine mengi. ccm waliteka mdahalo na kujifanya ni wa kwao huku wakijua hawakubaliki. Si uvamizi wa kigaidi huo?
 
Udasa ni chadeam mdahalo wao vijana wazalendo waliwawahi
 
MKUU HAWA WATU WA UDASA ni ngumu sana kutushawishi , japo ni kweli vijana wengi WALISOMBWA BUGURUNI KWA MNYAMANI nyuma ya ROZANA BAR , LAKINI HAO WALIKUWA WAZOMEAJI TU HAWAKUWA WAZUNGUMZAJI .
 
Angalia tu front line,Wasira,Mwigulu Nchemba,Ana Tibaijuka,Lukuvi etc magamba!!

Wakina Mama waliovaa shungi na ndala kutoka buguruni na vijana pale jukwaa la chini walioletwa na UDA!!

Kitila Mkumbo kama condom iliyotumika alifahamu fika na ndio maana upangaji wa watu kuzungumza ulikua ni kwa watu wa CCM,rejea hata nafasi ya kufunga mdahalo kupewa Lukuvi,Mwigulu kupewa kuongea pasipokuomba na hivyo hivyo kwa the rest gambas!!!
 
UDASA ilishajifiaga zamani toka Uongozi wake watoke akina Lwaitama na kushikwa na wahuni ambao wanazidiwa akili mpaka na ma ccm, kweli UDASA ya sasa ni mfu!
 
Wasomi wanatumika sana.

Ukiona msomi anatumiwa kwa maslahi binafsi fahamu wazi kuwa ama alibebwa na kupewa sifa ya hiyo ama amesoma lakini hakuelimika. Sifa ya msomi ni lazima awe anaweza kuchambua mambo na kuishi kwa uchambuzi wake na kusimamia kile anachoamini na kukubali kukosolewa katika kile anachoamini bila kupigana. Kimsingi UDASA wamedhihisha kuwa wao siyo wasomi ni watu wenye shahada za kwenye karatasi zinazowapa uhalali wa kuwa wakufunzi. Wanayoelimu ya vyeti lakini hawakuelimika na kwa msingi huo hawana sifa ya kuitwa wasomi.
 
CCM inabidi wawe na moto wao maalumu siku ya Kiama, Wallah hawa jamaa sijui wana roho gani aiseee
 
UDASA! Walishiriki kikamilifu katika kuharibu mjadala.
Habari za hujuma zilitolewa hapa mtandaoni. Walikuwa na wajibu wa kujiridhisha kuwa ni za kweli au si kweli.

MMoja wa waandaji wanajua historia yake na upinzani. UDASA walipaswa kujiridhisha kuwa mtu huyo ana credibility katika jamii yetu kuandaa shughuli kama hiyo. Kiongozi huyo ana mizigo mizito mabegani ilikuwa ni aibu kwa UDASA kumtwisha mzigo mwingine.

UDASA imekuwa platform ya wanataaluma kutafuta nafasi za kunyooshewa vidole. Kila siku akina BB na wengine wamegeuza taaluma zao kuwa vichaka vya CCM.
leo UDASA Wanataka kusema kitu gani! mbona hawakemei wanataaluma wanaotafuta kuteuliwa kwa kunyooshewa vidole.

UDASA ya leo si ile UDASA. Zamani UDASA ilikuwa chimbuko na kisima cha fikra, siku hizi ni kama genge la wahuni tu waliovaa tai. Imegeuzwa kuwa chaka la wanasiasa uchwara.

Siyo UDASA ile ya akina Thabo Mbeki kwenda kuchukua mbinu na mikakati. Si UDASA ya akina Walter, Cuthbert n.k.

Ndiyo maana anapokuja mtu kama Prof Lumuba, ataonekana kuwa na uwezo mkubwa sana.
Sababu kubwa ni kujitofautisha na UDASA

UDASA wangepaswa kujisikia aibu sana kama anatoka prof nje ya nchi yetu na watu kumwelewa kuliko wale wa UDASA.

Jamani, UDASA ya leo ni genge tu la watu waliovaa tai safi, the least to say. Siyo UDASA Tuliyoifahamu wengine

Sad!
 
..... Nilikua Naangalia, Kulikua Na Vitoto Vidogo Vinanuka Mikojo Tu, Akina Mama Wamevaa Ndala, Yaan Ma Uda Yaliyo Wasomba Yalikua Matano
 
Jamani, mnasahau kwamba VC wa UDSM na mzee wa "pua" pale PSPA ni makada?! Kitila Mkumbo aliondolewa kwa sababu ya "kudhaniwa" kuwa gwanda!

UDASA imeharibu hadhi ya UDSM kwa 100%
 
Back
Top Bottom