UDART mbona hamtangazi kuzidiwa?

UDART mbona hamtangazi kuzidiwa?

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,556
Jana ilikuwa patashika kwa tunaotumia usafiri wa Mwendokasi, kuanzia kituo cha Gerezani tulijazana abiria wengi mno huku ikionekana wazi kabisa gari nyingi hazipo barabarani.

Hapo gerezani gari zimejaa kituo kizima wanasema ni mbovu, vituo vyote watu wamejazana wameshalipia na kuhaha kupata usafiri.

Nikahamia kituo cha Fire pale tulisubiri gari ya Ubungo kwa zaidi ya dakika 30 halikutokea gari, watu wa kwenda Kimara ilibidi wagombanie bus za Kivukoni ili kugeuza nazo, hali ilikuwa mbaya mno kwa jana labda na leo.

Cha kujiuliza kwanini kampuni hawatangazi hali hii mbaya na kwamba wamezidiwa? Je kwa trend hii na kasi ya hizi gari kuharibika huku na kasi ndogo ya services tutafika miaka kumi?

Hali ni mbaya jamani usafiri huu umekuwa mateso makubwa serikali imulike mradi huu.

Tujiulize itakuaje mradi huu ukitanuka hadi njia ya Kilwa ambako ndio kunaaminika kuwa na wakazi wengi zaidi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ndivyo hali ilivyo leo.
IMG_20200106_072309_1.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii nchi inakwama sana kwenye Uongozi na Menejimenti.

Ni Jambo la aibu Sana kwa Menejimenti ya huu mradi

Inachukiza sana kuona mradi ambao hela ya walipa kodi iliyotumika kwenye huu uwekezaji inadumbukia shimoni.

Rais JP Magufuli naomba anipe usimamizi wa huu mradi ili kwa miezi 3 Hadi 6 kwa ushirikiano na wadau niweze kuleta mapinduzi ya huu usafiri hapa DSM
Tungepata Uzi mmoja wa kutolea malalamiko maana huo usafiri Ni adhabu kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine tunapotoa angalizo kuhusu management kwenye taasisi za umma huwa tunatukanwa na kuitwa majina ya kashfa. Tatizo lililopo UDART ndilo hilo hilo lililopo karibu kwenye taasisi nyingine za umma: poor and incompetent managements ambazo unfortunately msingi wake ni dhana ya kuwa aliepo kwenye madaraka HAWEZI kukosea.
Hatuwezi kupiga hatua kwa kuendelea kufanya kazi kwa kutumia methodologies za miaka ya 50. Daladala zipo relatively efficient kwa kuwa wamiliki wapo profit-oriented na wafanyakazi wake wanakuwa rewarded au kuadhibiwa kulingana na performance. Ukiweka kiwango cha mshahara kwenye taasisi kama UDART LAZIMA ushindwe hata kabla ya kuanza: ukimpa dereva mshahara wa 400,000 kwa mwezi (iwe ameendesha route 2 au 20 kwa siku) unadhani ni kitu gani kitakachomfanya aendeshe route 20+ badala ya 2?

Nchi inahitaji mabadiliko ya kimfumo na kimtazamo. Sitashangaa kusoma hapa kauli za "Mheshimiwa Rais ingilia kati" kama pendekezo la kutatua matatizo ya UDART.
We have a very looong way to go.
 
Wengine tunapotoa angalizo kuhusu management kwenye taasisi za umma huwa tunatukanwa na kuitwa majina ya kashfa. Tatizo lililopo UDART ndilo hilo hilo lililopo karibu kwenye taasisi nyingine za umma: poor and incompetent managements ambazo unfortunately msingi wake ni dhana ya kuwa aliepo kwenye madaraka HAWEZI kukosea.
Hatuwezi kupiga hatua kwa kuendelea kufanya kazi kwa kutumia methodologies za miaka ya 50. Daladala zipo relatively efficient kwa kuwa wamiliki wapo profit-oriented na wafanyakazi wake wanakuwa rewarded au kuadhibiwa kulingana na performance. Ukiweka kiwango cha mshahara kwenye taasisi kama UDART LAZIMA ushindwe hata kabla ya kuanza: ukimpa dereva mshahara wa 400,000 kwa mwezi (iwe ameendesha route 2 au 20 kwa siku) unadhani ni kitu gani kitakachomfanya aendeshe route 20+ badala ya 2?

Nchi inahitaji mabadiliko ya kimfumo na kimtazamo. Sitashangaa kusoma hapa kauli za "Mheshimiwa Rais ingilia kati" kama pendekezo la kutatua matatizo ya UDART.
We have a very looong way to go.
Nimekuelewa; hao madereva wanatakiwa walipwe kulingana na idadi ya ruti wanazofafanya, but ninahisi huwa wanafanya hivyo kwa maelekezo toka sehemu fulani, au wao madereva binafsi; kwasababu km hawabebi abiria basi ni bus zaidi ya moja hufanya hivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo letu hatujifunzi mambo ya Posta na Simu tunaendelea kumonopolize transportation bness, ukienda Cairo kuna mwendokasi kama hz zetu walichofanya wao mafarao wameweka makampuni matatu tofauti yana operate hvyo kuleta ushindani udart ikilala xy company ingebeba abiria wote hao soln ni kuanzisha kampuni ishindane na udart

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa sijui wanafanya makusudi? maana tender ilishatangazwa tangu Nov.2019 ya kutafuta mwendeshaji mwingine, kutoka ndani hadi nje ya nchi.
 
Aibu ni mradi tumekopa billions from World bank kwa pink elephant project!
 
Huu mradi wangemtafuta tajiri kama bhakresa aundeshe...hawa jamaa wameshindwa.....tunakaa vituoni muda mrefu sana...na magari yakifika tunaingia kama ng'ombe...watu wanapoteza vitu vyao kama viatu..saa..wengine wanaumia...bila kusahau wazee wa ndole...wazee..wanawake.. na watoto ndio wanaoteseka sana..Au wangeruhusu daladala hasa asubuhi na jioni.
 
Back
Top Bottom