Udahili elimu ya juu unahitaji tathmini ya wazi

Masiya

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
7,578
7,281
Baada ya kufuta Central Admission System (CAS) na kuweka uombaji wa vyuo moja kwa moja chuoni (Direct Application to Institutions-DAI) naamini sasa tumepata uzoefu unaotuwezesha kufanya tathmini itakayo tuwezesha kuamua mfumo wa kutumia(CAS, DAI au mfumo mwingine). Tuliambiwa CAS inawafanya waombaji wapangiwe program wasizo omba (tukapewa mifano ya rushwa hata kama hakuna ushahidi uliowekwa wazi).

CAS ikaondolewa na sasa tuna hiyo DAI (siyo jina rasmi).Tumesguhudia tatizo kubwa la multiple selection ambalo matokeo yake ni pamoja na kutibua calendar ya udahili (mwaka wa jana na huu tumefika round ya nne), vyuo kabla ya kujua wana nafasi zipi raundi ifuatayo huanza, wenye multiple selection hushika nafasi zaidi ya moja na kila round wapo.

Jana TCU wameonyesha kuna kama vijana 5000+ hawaja confirm round ya 1-3. Dakika ya mwisho kutakuwa na nafasi wakati tuna vijana wana ufaulu wa kuweza kujaza hizo nafasi lakini watakosa. Bodi ya mikopo nayo hauwezi kutoa mkopo kwa mtu ambae hawajui amechaguliwa wapi na wao wana muda muafaka wa kutoa majina ya waliopata mkopo.

Hivyo wengi ambao wanakadhia ya multiple selection si ajabu itakula kwao. Na je kila mtu anaepata chuo anapata anachotaka?

Nafikiri ni wakati muafaka kuwe na tathmini ya mifumo hii na uwazi katika hili ili tujue tunakwenda wapi. Waizara ya Elimu , TCU, NACTE, na Vyuo ni baadhi ya wadau. Ni imani yangu zoezi kama hili likifanywa kwa uwazi litasaidia. Na hili liendane na vyuo kuna na uwazi mtu akikosa ajue amekosaje.

Naweka baadhi ya mijadala iliyopita kuhusu kuondolewa kwa CAS-mapovu yalitutoka lakini kuna historia ndani yake na labda njia za kutatua baadhi ya haya mapungufu.

Nini hatma ya TCU baada ya kauli ya Rais Magufuli? - JamiiForums

Kuondolewa CAS ni chanzo udahili mbovu - JamiiForums

TCU mnaturudisha nyuma. Kwa mfumo wenu mpya wa udahili vyuoni, mnatuonea wananchi - JamiiForums
 
Nitachangia kwa hoja chache, nyepesi na zenye kueleweka:
1. CAS iliondolewa kwa sababu nyepesi mno.
2. Kuondolewa kwa CAS hakukuzingatia tathmini ya faida na hasara zake bali kulizingatia ''kutii maagizo ya Mkoi''
3. Kwa tunayoyashuhudia sasa, CAS ilikua ni bora mara nyingi mno kuliko mfumo uliopo sasa.

Naamini hapa tuliteleza, tujitafakari upya na tufanye maamuzi sahihi zaidi, CAS will be once again waiting for us.
 
nimeona UDOM kozi wanazodai hazijaja nikakasirika sana maana kuna watu nawajuwa wameomba kozi hizo mara 3 wanaambiwa zimejaa na hawakupata hlf leo wanasema hazijaja.

Tena kozi moja bado ina nafasi 263 watu wameomba kozi hiyo zaidi ya mara 2 wakakosa na wana ufaulu mzuri.

kozi ya MD bado haijaja kuna nafasi 5 ila watu walikuwa wanalalamika wamekosa kozi hiyo.

sielewi kinachoendelea huko hlf ukiwapigia wanajibu simple tu..
NIMEANZA KUELEWA KWA NINI WATU WANAKUWA MAGAIDI..wanaamua kama mbwayi iwe mbwayi.
 
Yan...mimi mpaka sasa sijajua hakika vigezo nadhan ninavyo ila sijapata kudahiliwa mpaka dkka hii yani sielewi ..unakuta mtu kapata vyuo vitatu mpaka saiv hajaconfirm kapata muhas...udom....kcmuco....kinaniuma ....mimi Nina diploma plz hizo systems zifanye bas inavostahili watu tukasome.. ..
 
Why ppl aren't admitted....if there are available slots...kama kozi ya md 18 slots in udom zipo.....n if a student has qualifications y is ds happening ....y ppl hawaachii wenzao nafas....may they confirm plz.....kama inakugusa nadhan utaelewa...afu unakuta you dont know who to tell kwamba y?is it issue ya equivalent qualifications.....diploma nao mconsider
 
nimeona UDOM kozi wanazodai hazijaja nikakasirika sana maana kuna watu nawajuwa wameomba kozi hizo mara 3 wanaambiwa zimejaa na hawakupata hlf leo wanasema hazijaja.

Tena kozi moja bado ina nafasi 263 watu wameomba kozi hiyo zaidi ya mara 2 wakakosa na wana ufaulu mzuri.

kozi ya MD bado haijaja kuna nafasi 5 ila watu walikuwa wanalalamika wamekosa kozi hiyo.

sielewi kinachoendelea huko hlf ukiwapigia wanajibu simple tu..
NIMEANZA KUELEWA KWA NINI WATU WANAKUWA MAGAIDI..wanaamua kama mbwayi iwe mbwayi.
Why ppl aren't admitted....if there are available slots...kama kozi ya md 18 slots in udom zipo.....n if a student has qualifications y is ds happening ....y ppl hawaachii wenzao nafas....may they confirm plz.....kama inakugusa nadhan utaelewa...afu unakuta you dont know who to tell kwamba y?is it issue ya equivalent qualifications.....diploma nao mconsider
Haya ya nafasi kuonekana zipo baada ya kuambiwa mtu umekosa yanatokana na kiasi kikubwa-multiple selection. Chuo kikisha fanya selections zake kinaona nafasi imejaa, majina yakienda TCU ndipo wanagundua multiple selections na hapo kila Chuo huamini hao watakuja hapo hivyo kwao nafasi imejaa. Baada ya baadhi yao kukonfirm ndio wanaona nafasi ambazo hazija jazwa. Na itakuwa hivyo mpaka round ya mwisho NAFASI ZITABAKI NA WENGINE WATAKOSA CHUO. Sioni hili unalikwepa vipi kama kila chuo kina mchakato wake kwanza na huja pamoja wakati wa uhakiki. Hapo kwenye nafasi 263 bado sijaelewa labda kama waombaji hawakutosha au waliamua kukimbia chuo wakati wa ku-confirm (hii inahitaji review ya undani).
Code number ingetumika vizuri inge ondoa tatizo la muombaji kuambiwa ameconfirm chuo zaidi ya kimoja inayoweza kutokea kama kuna mtu mwingine au chuo kuamua ku-konfirm kwa niaba yako,lakini haiondoi multiple selections msingi wa matatizo makuu ya mfumo wa sasa. SIAMINI VICHWA VYA WADAU VIKILIKALIA HILI LITATUSHINDA, LA MSINGI TUWEKE WELEDI MBELE NA SIO SIASA.
 
Tatizo la sisi Watanzania ni wanafiki sana. Wakati mkulu akitoa yale maagizo watu walipiga makofi sana na tena wengi ni wanafunzi wa vyuo kipindi hicho. Mkulu alijulia wapi matatizo ya CAS kama si watu kulalamika?

Tatizo ni ushamba wa watu kuona kwamba ameonewa akitemwa na CAS. Eti walikua wanasema watu wanahonga ili kupata nafasi. Sasa je huu mfumo wa saizi na CAS upi una nafasi nyingi za kuhonga.

Nilikua nikiwaona wengi wanavyofura kwa hasira baada ya CAS kuwatupa second round. Lawama zilikua zinawaangukia TCU. Wakawa wanadai eti TCU wanawapangia vyuo wasivyopenda. Sasa mtu msomi anatoa kauli kama hizo huku akijua kabisa CAS haiwezi kukuchagua chuo ambacho hukuomba.

Mimi nasema hivi TCU wasilaumiwe kabisa katika hili. Ushamba wetu wa kuona kila kitu tunaonewa ndio umetuleta hapa. Ndio maana nchi hii ni nadra sana kuona mgombea akikubali kushindwa hata kama hana ushahidi wowote wa kudhulumiwa.

Wakati nchi nyingi zikihamia CAS Sisi tukaihama na kurudi mfumo wa kale kwa sababu ya unafiki wa mijitu fulani. Tena baada ya kutuingiza chaka saizi naona nao wanaulaumu huu mfumo na TCU
 
Haya ya nafasi kuonekana zipo baada ya kuambiwa mtu umekosa yanatokana na kiasi kikubwa-multiple selection. Chuo kikisha fanya selections zake kinaona nafasi imejaa, majina yakienda TCU ndipo wanagundua multiple selections na hapo kila Chuo huamini hao watakuja hapo hivyo kwao nafasi imejaa. Baada ya baadhi yao kukonfirm ndio wanaona nafasi ambazo hazija jazwa. Na itakuwa hivyo mpaka round ya mwisho NAFASI ZITABAKI NA WENGINE WATAKOSA CHUO. Sioni hili unalikwepa vipi kama kila chuo kina mchakato wake kwanza na huja pamoja wakati wa uhakiki. Hapo kwenye nafasi 263 bado sijaelewa labda kama waombaji hawakutosha au waliamua kukimbia chuo wakati wa ku-confirm (hii inahitaji review ya undani).
Code number ingetumika vizuri inge ondoa tatizo la muombaji kuambiwa ameconfirm chuo zaidi ya kimoja inayoweza kutokea kama kuna mtu mwingine au chuo kuamua ku-konfirm kwa niaba yako,lakini haiondoi multiple selections msingi wa matatizo makuu ya mfumo wa sasa. SIAMINI VICHWA VYA WADAU VIKILIKALIA HILI LITATUSHINDA, LA MSINGI TUWEKE WELEDI MBELE NA SIO SIASA.
Masiya nimependa sana andiko lako. Niongezee tu kuwa wapo wanafunzi waliochaguliwa chuo zaidi ya kimoja lakini toka raundi ya kwanza lakini hawajapata codes hadi leo. Pia kumekua na mvutano mkubwa sana kati ya baadhi ya vyuo na TCU lakini hasa kisiasa na siyo kutatua tatizo na ndicho kilichonipa nguvu ya kuunga mkono andiko lako
 
Aisee...so far nimeona multiple selected applicants....3rd round....na single selected applicants awamu hii ni vyuo vichache vimetoa....kama udsm...kairuki....am not sure of udom coz wamedili sana na multiple 2nd and 3rd selection.....nadhan na sua wametoa ya awamu ya tatu...lakn vyuo kama kcmuco....cuhas..sijaona updates zao...sa sijajua kwamba madirisha yao ni kwamba yamejaa au vipi na wanawezaje kuhamasisha 4th round while awamu ya 3 kunasintofahamu
 
unajua huu mfumo unafanya hadi sisi wa education ambao tumepata multiple selection tusipate mkopo...yaani code wamechelewesha halafu bila kujali bodi ya mikopo ikawapa wale waliopata single selection matokeo yake wale wa priority courses waliochaguliwa multiple wanakosa mkopo kwa kukosa kuconfirm na kosa sio la kwao...halafu baadaye wanasema code hazitumiki tena sasa nimechaguliwa vyuo vitatu..je mkopo wangu wataupeleka chuo gani?..tanzania naipenda ila haiko serious...tcu na heslb ni za serikali lakini hazina uhusiano katika ufanyaji kazi....
 
unajua huu mfumo unafanya hadi sisi wa education ambao tumepata multiple selection tusipate mkopo...yaani code wamechelewesha halafu bila kujali bodi ya mikopo ikawapa wale waliopata single selection matokeo yake wale wa priority courses waliochaguliwa multiple wanakosa mkopo kwa kukosa kuconfirm na kosa sio la kwao...halafu baadaye wanasema code hazitumiki tena sasa nimechaguliwa vyuo vitatu..je mkopo wangu wataupeleka chuo gani?..tanzania naipenda ila haiko serious...tcu na heslb ni za serikali lakini hazina uhusiano katika ufanyaji kazi....
Bado huja confirm ndugu?
 
ndugu huo utaratibu wa kuconfirm haupo tenaaaa...wanasema unaenda mahala unapotaka...je mkopo pia wataupeleka wanapopataka?
Jana "nimesikia" kuwa kwenye chuo kimoja kuna wanafunzi waliojikuta nafasi zao zimejazwa na wandugu wa multiple selection walio wahi kujisajili na wao wame elekezwa watafute wapi kuna nafasi wasajiliwe huko. Sasa kwa hili sijui kama hawa tuta ambiwa wamepata degree na chuo walichokipenda. Bahati mbaya itakuwa vigumu kupata data kamili.
 
jamani mwanangu kachaguliwa saut mwanza kozi ya sheria lkn amefika huko wamemsajili kwa kozi ambayo hata akuomba TCU naombeni ushauri tufanyeje arudishiwe kozi yake ya sheria?
 
jamani mwanangu kachaguliwa saut mwanza kozi ya sheria lkn amefika huko wamemsajili kwa kozi ambayo hata akuomba TCU naombeni ushauri tufanyeje arudishiwe kozi yake ya sheria?
Mkuu naona itabidi uwasiliane na uongozi wa chuo moja kwa moja (kama uko karibu nao uende in person) vinginevyo upitie TCU. Hiyo ipe priority hata kama itakuingiza gharama za kufika huko.
 
jamani mwanangu kachaguliwa saut mwanza kozi ya sheria lkn amefika huko wamemsajili kwa kozi ambayo hata akuomba TCU naombeni ushauri tufanyeje arudishiwe kozi yake ya sheria?
yaani kiufupi wamemnyima haki yake....pia naona uende ukaripoti tcu naamini watakusaidia..yaani mh ndalichako akisikia hiyo ishu..atafukuza wahusika wote...kwa maana huo ni utapeli.
 
Back
Top Bottom