'Uchuro' waingia CHADEMA

CHADEMA kitaongozwa na watu makini wanaojua nini umuhimu wa demokrasia, Chadema kikiwa na waasisi walio komaa kwenye demokrasia na wakijua kukua kwa chama ni pamoja na kuheshimu katiba na kuilinda, kuheshimu uongozi na kuchaguana kwa kufuata misingi imara ya uhuru wa haki na usawa.

Lwakatare ni mwanachama sawa na yeyote. Na si dhani kweli Mbowe amekuwa na njozi na ya kuhakikisha kwamba mambo atayapeleka atakavyo pasipo chama, amekuwa jemedari licha ya kuandamwa na CCM na wapambe wake.

Tunajenga chama makini na si umangimeza, na kama ikijulikana yupo mangimeza basi chama kitafuata taratibu na kutokomeza hila zote za kishenzi na kipuuzi. Ni matumaini yangu kuwa Lwakatare hajaingia chadema kutuvuruga bali kutekeleza azma yake ya mapinduzi ya kisiasa na demokrasia ya kiuchumi ya mtanzania wa leo.
 
JF mnawaendekeza sana hawa ChAdEmA... Bandiko hili si lilikuwa kule kwenye habari na hoja binafsi? Limehusu nini kuwepo hapa ukumbi wa siasa?
 
Lakini Lwakatare hana hata miezi miwili kwenye Chadema hajaijua katiba na mfumo wa Chadema. kwanini asipewe KITILA MKUMBO?
mtu hamjamjua mnampa madaraka makubwa bila kupitia njia au ngazi walizopita wengine.
 
JF mnawaendekeza sana hawa ChAdEmA... Bandiko hili si lilikuwa kule kwenye habari na hoja binafsi? Limehusu nini kuwepo hapa ukumbi wa siasa?

Hata unapofanyika uchaguzi au jambo lolote ni Chadema ndio wanapewa umuhimu mkubwa hapa.hujiulizi kila kada wa Chadema anakuja hapa kuwa member hadi mzee Mtei,unafikiri inatokea kwa bahati tu?
 
Hata unapofanyika uchaguzi au jambo lolote ni Chadema ndio wanapewa umuhimu mkubwa hapa.hujiulizi kila kada wa Chadema anakuja hapa kuwa member hadi mzee Mtei,unafikiri inatokea kwa bahati tu?
Kanda,
Mbona na wewe upo? Na wewe ni CHADEMA?
 
Vipi kuhusu Kitila Mkumbo? Nafikili ni wakati wake kumake a move... there is no tomorrow!

Au arudi chama kubwa CCM
 
Kitu muhimu cha kuangalia kwenye siasa zetu, ni watu wanaohama chama kwa nia ya kupewa madaraka. Si vibaya kugombea au kuchukua form ya kugombea uongozi wowote kwenye chama unachokipenda, ila isiwe ndio chanzo cha kuhama chama kimoja kwenda kingine. Hii ni tabia mbaya na inadhoofisha sana jitahada za wengi. Mtindo wa ahadi za kupewa vyeo na uongozi hutumika CCM pale wanapotaka kudhoofisha upinzani, sidhani kama ni mchezo mzuri kwani mtindo huu haujengi misingi bali unakuza ufisadi haswa msukumo unapokuwa ni uongozi na marupurupu, hupati vichwa vinavyofikiri bali maboga yaliyoishiwa maji yanatafuta ardhi yenye rutuba.

Chama kiweke mazingira mazuri ya kupokea wanachama wapya bila kujali wanatoka wapi bila kuwaahidi chama kitawafanyia nini bali wao waseme watafanyia nini chama na wananchi.

Duniani watu wasio na misimamo wanaogopewa sana isipokuwa Tanzania. Ikumbukwe kila mahali kiongozi mahiri lazima aonyeshe uwezo wake hasa wa kupambana na matatizo na jinsi ya kuyatatua sio kuyakimbia.

Chadema kitajengwa na wanachama waaminifu na wanaoheshimu utawala wa katiba na sheria waliojiwekea wenyewe kuwaongoza na kuongoza nchi.
 
Kuna uvumi kuwa Chadema itagawika kutokana na kundi linalomuunga mkono Zitto na lile la wahafidhina ambao wanadai chama ni chao na hakuna wa kuwapangia .
 
Hawa chadema nao wameanza vizuri saivi wanatoana macho kwa vihela vya ruzuku karibu wataishia kama Mrema kama hawatotanabahi mapema.
 
Kuna uvumi kuwa Chadema itagawika kutokana na kundi linalomuunga mkono Zitto na lile la wahafidhina ambao wanadai chama ni chao na hakuna wa kuwapangia .

Si kweli huu ni uvumi na njia ya CCM kuona chadema chama makini kinayumba, hayo hayatatokea. CCM walitegemea hivyo walipomchukua Dr walid walipandikiza chuki haikufanya kazi. Vilevile walitumia kifo cha Wangwe kukigawa chama walishindwa sasa wanahaha kama mbwa koko aliyekosa chakula. CCM wanaogopa kwani Chadema wanajipanga vizuri na wanamwelekeo unaoeleweka ni chama kichanga kinachoweza kujadili mambo yake kwa uwazi na kutatua matatizo yake bila ya kishindo cha mpasuko kama huo wa wana CCM- fisadi
 
Kitila na Zitto huwezi kuwaweka pamoja (kuongoza) na Mbowe kwa muda mrefu wakaelewana bila kuliweka sawa tatizo la shule la the later. Wanamuacha mbali Mbowe kwa shule na vision.
 
Mchukia Fisadi na Junius...
Tofauti zenu ni sababu za chaguzi zenu----wote mmechagua mwanamke, lakini mmoja kachagua kwa sababu anafaa kuwa mke (marriage material), na mwingine kamchagua kwa sababu ana wowo** nzuri T*** material).
 
nahisi utakuwa mpotoshaji mzuri maana hauna uhakika na unachosema........
 
Kuna uvumi kuwa Chadema itagawika kutokana na kundi linalomuunga mkono Zitto na lile la wahafidhina ambao wanadai chama ni chao na hakuna wa kuwapangia .
Uvumi! uvumi! uvumi! Basi, Lakini Jamaa wanasonga mbele na wananchi wanawaelewa na kuwakubali. Angalia uchaguzi wa Busanda na Biharamulo, hata kama CHADEMA haikushinda, mtu yeyote makini atafahamu kuwa kuna mapinduzi ya kifikra ya meshawaingia wananchi wengi katika kipindi hiki kifupi.
Ok, sawa kuna uvumi, so what?
 
Kitila na Zitto huwezi kuwaweka pamoja (kuongoza) na Mbowe kwa muda mrefu wakaelewana bila kuliweka sawa tatizo la shule la the later. Wanamuacha mbali Mbowe kwa shule na vision.

katiba ya Chadema haijasema kwamba lazima uwe na degree ndio ugombee uongozi, hilo ni juu ya wanachama wa chadema kuona ni kiongozi gani anawafaa kwa wakati gani. Wote wanahitajika kwani uongozi ni hekima na busara na shule inasaidia tu kupambana na mazingira yako, ila inaweza isikupe hekima wala busara, rejea Chenge, Dr balali, Profesa Mbilinyi, Pr. Mahalu, nk. Kweli tunahitaji wengi na wenye uchungu na nchi yao.

Zitto anaweza fanyakazi na mtu yeyeto ni kijana mahiri na hana shida kwenye maelewano na watu, misimamo yake ndio haiba yake na binadamu au kiongozi asiye na msimamo hafai. Kitila namwelewa vizuri ni kijana mwenye busara na hekima na anauwezo mkubwa wa uongozi anaweza fanya kazi na yeyeto. Na ikumbukwe hawa hawatakuwepo milele na kumfanya Mbowe kama vile Chama ni mali yake ni kumwonea, wao wenyewe Chadema ndio waliomwomba agombee uenyekiti hakung'ang'ania na hata kugombea uraisi alibembelezwa sana, haya mengine ni matokeo na dhahama za kuwa kiongozi kwani lazima ubebe dhambi za wengi.
 
Lakini Lwakatare hana hata miezi miwili kwenye Chadema hajaijua katiba na mfumo wa Chadema. kwanini asipewe KITILA MKUMBO?
mtu hamjamjua mnampa madaraka makubwa bila kupitia njia au ngazi walizopita wengine.

Watu wengine bana! APEWEJE?
 
Kuna kitu kinanishangaza hapa,hebu niambieni,nielezeni, Lwakatare anataka kuchukua nyadhafa ya juu kabisa ktk chama cha chadema,chama ambacho si kichanga ni kizoefu na cha muda mrefu,lkn je hakuna kanuni yoyote ndani ya chama inayosema mtu akiingia ndani ya chama mpaka akae muda flani na apitie kwa ngazi za wilaya mpaka afike juu, au kwa sababu Lwakatare ametoka cuf? na je mwanzo ndani ya chadema kulikuwa hakuna watu makini ambao wanaweza kuchukua nafasi za juu mpaka atoke mtu kutoka Cuf? inaonesha Cuf ina viongozi makini kwa maana hiyo?

Kule Cuf kwa sasa huwezi kutoka chama kingine au hata kujiunga tu kwa mwanachama mpya halafu ugombee uongozi,kwanza mpaka uwe mwanachama kwa muda wa miezi 6 na la pili ukianza kugombea lazima uanze kwenye matawi ya chini upitie kwa ngazi hadi ngazi. sasa hili linaonesha cuf ni makni kule chadema..
 


angalia Lipumba bana hamna kitu!!!!!!!!
 
Pdidy, Hii ripoti inayosemekana imeandikwa na Gazeti la RAIA MWEMA, kwa maoni yangu inaizushia Chadema mgogoro ambao haupo. Hata Mwenyekiti Taifa, Mhe. Mbowe amejieleza vizuri tu kwamba Chadema (na Tanzania kwa jumla) wanahitaji vijana wengi wa aina ya Zitto. Na Zitto mwenyewe ametamka kwamba yuko tayari kuendelea na wadhifa wake wa Naibu Katibu Mkuu na ubunge.

Pamoja na kukubaliana na Mhe. Mbowe, ningeongeza kwamba Chadema inahitaji Slaa wengi na pia Mbowe wengi. Na nawapongeza kwa Operesheni Sangara ambayo inaendelea kuvutia Watanzania wengi ktk Chama ambacho kinatoa matumaini kwa Watanzania. Uzi ni huo huo. Hakuna kulala mpaka kieleweke.

Wahasimu wa Chadema wataendelea kupika majungu na kuchochea mifarakano ktk chama kinachoonyesha kwamba ni tishio kwao. Kwa hiyo jambo muhimu ni kupuuza majungu na kuendeleza mikakati ya Chadema kujiimarisha kuanzia ngazi ya chini; na kuhakikisha viongozi wanashikamana, wakitambua kwamba jukumu lao kuu ni kuleta na kuimarisha demokrasia ya kweli na uhuru wa kweli Tanzania.

Nafurahia ukweli kwamba viongozi wa Chadema wanatambua vipaji vya wenzao, na kwamba kila mmoja ana fursa ya kuchangia kwa uwezo wake wote ili kuleta mafanikio. Ushirikiano na mshikamano wa hali ya juu vinahitajika ili nembo ya USHINDI(VICTORY) ya Chadema iweze kudhihirishwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…