Uchumba wangu umevunjwa

Tuliza akili, huyo mchumba wako kama yuko serious atakuelewa, na ukitumia nguvu kubwa kumuelewesha mchumba wako anaweza kukukubalia ila ataishi kwa mashaka sana. Sasa wewe huyo mchumba wake muache achambue mwenyewe asiporudi atakuwa kakuepusha na janga kwani hata yeye atakuwa ni tatizo.


pia inawezekana yey ndo kaunda picha hilo kutaka kujua reaction yako kwa matukio kama hayo, kwa hiyo utulivu unahitajika sana katika hilo.
 

umeshajiuliza swali, Je kama huyo mchumba wako amecheza huo mchezo na rafiki yake kwa nia ya kuvunja uchumba na wewe?
 
You have a point. Kila mtu ana react kivyake. Ushauri wangu ni kuwa asijarib kumlazimisha bibie amwelewe bali aendelee kimya kimya kumtafuta mbaya wake. Atakapomjua basi amalizie kesi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hivi.....
Kwani ulikua na wachumba wangapi...!!??
Maana kwa uzowefu wangu kwenye hii sector ya viwanda, kabla hauja oa unapaswa walau ukuwe na wachumba watatu...tehteehh

 
Mkuu, kabla sijakushauri chochote naomba kujua kwamba je hilo ni kosa lako la ngapi kwake kukuta sms kama hiyo kwenye simu yako??? Au kuna siku umewahi pigiwa simu za utata ukiwa nae huyo mchumba wako???
 
kwanini ulimruhusu kuangalia simu yako huyo mwanamke? njia rahsi ya kutafuta sababu ya kumuacha mke/mme wako ni kudukua simu yake
 
Mpaka nimpe mwanamke simu hata ashike tu nimeficha kila kitu sms zinaingia kimya kimya hamna notification iwe ya whatsapp au call simu inakuwa kama ipo kwenye airplane mode
Na sijawahi feli coz yalionikutaga hayatajirudia tena nilijifunza
Pole mkuu najua inavyouma duh
 
Hahahah huyo ni manzi anaekujua na ameamua kukuharibia style makusudi tu. Tuliza kichwa taratibu utamgundua otherwise wataalamu watakuja na ngonjera za jini mahaba. Sasa sijui majini wanatumia smartphone sikuhizi!
ndio majini yanatumia smat siku hizi kuna mdau alipost juzi kati jini limemtumia hela na linachat nae

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila mkuu usimwamini mwanamke % zote kushikashika simu yako wengine wanapenda ugonvi tu hata akikuta picha ya famila mko mama, baba, dada na mabro ataulizia hao wanawake nikina nani wako haamin mpaka hawaone aamin
 
Hivi huo ulimwengu wa mchumba wako unaujua wote? Unafikiri atatoa namba ys demu wa karibu ili umjue! Yeye anaweza kuwa dar huyo vero yupo Arusha kapewa mchongo huo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajua nakusikiliza na kwa kuwa Umekiria kuwa Umebobea kwenye hiyo sekta sina Shaka na kweli wote bado wanakupigania, Confirmatory test done . Big up brother
 
Mkuu huyoalaikuwa mpenzi wako wa Muda mrefu au Mchumba wako? Level ya Uchumba wako ikoje? Ulishato mahali na kutambulishana pande zote za Familia? Ukinijibu nitakuja na Majibu ya kilichotokea.

Ila tofautisha Mahusiano ya Kingono ambayo wengi mnayaita ( Mapenzi, Upenzi) na mahusiano yaliyoruhusishwa na familia za pane=de zote mbili ambazo ndizo zinazaa neno (Mchumba/Uchumba) baada ya kutoa Posa au kitu chochote ambacho mila husika zinakiheshimu...

Nawasilisha
 
Unajua nakusikiliza na kwa kuwa Umekiria kuwa Umebobea kwenye hiyo sekta sina Shaka na kweli wote bado wanakupigania, Confirmatory test done . Big up brother
Kupiganiwa sio sifa, na katika safari ya mahusiano naamini kuna watu wengi hasa wanaume (wanafiq) ambao hupendelea kujionyesha kwamba wao ni wasafi na hawakuwahi kukisea ama kuwa na wachumba zaidi ya mmoja wakati wa ujana wao.
Hapa nadhani ni wakati muafaka wa kumuelekeza kijana ili ajifunze kupitia mimi/sisi, na asije akafanya makosa kama nilio ama tulio kwisha kuyafanya.
Haya wewe ambae ni msafi and perfect, ebu tupe maekelezo sisi wazinifu na wachafu (kwa kauliyako tunao gombaniwa) ebu natamani nijifunze ama tujifunze kutoka kwako wewe Mr perfect.
 
Mkuu, sioni sababu ya kumuuliza maswali mengi mleta mada.
Hapa kwa jinsi alivyo elekeza, hai hitaji hata shule kubwa ili kubaini kinacho jiri kwenye mawazo ya mchumba wa mleta mada.
Naaa...... jf tujifunze kuheshimu mawazo ya yeyote mleta mada, hii hutokana na wakati mwingine mwenye threads hajisikii kuanika baadhi ya mambo zake kwa undani.
Nivyema tumshauri kwa kiwango cha maelekezo alio yatoa mleta mada, na kwaku mchimba nadhani ni kutaka kuingilia yale ambayo mleta mada hakupendi tuyafahamu.
 
Pole Sana kwa mchezo aliokuchezea huyo mchumba wako it's a game ili akae mbali na wewe na hakupendi kabisa na hayuko tayari kuwa mke wako. Kama huamini jaribu kumuita Kisha mweleze Kila kitu alafu mpe jukumu na yeye la kumtafuta huyo Malaya wake aliye mtuma Kama atakubali. Kama kweli anakupenda atakubaliana na wewe ili mtatue Hilo tatizo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…