Uchimbaji mafuta na nchi ya 'MAJUHA'

Tigga mumba, habari ya blocks and whatever huwezi jua unless otherwise! Tukitangaziwa ndio tutajua, inawezekana yapo!
 
Tigga mumba unajua maana ya belgium disease? It has something to do with mafuta! Hata kama blocks are obvious huwezi jua
 
Chukua mfano huu "usio hai"
Nina safisha mafuta lita 500,000 kwa siku.
BP,Shell,Engen,Oilcom,etc wanaweza kuuza lita 300,000 kwa siku.
Hizo lita 200,000 zina pelekwa wapi?

Kumbuka hizo marketing companies hawana uwezo wa kutunza mafuta mengi
kwa wakati mmoja.

Land Locked countries zinazoizunguka Tanzania hizo lita laki 2 haziwatoshi kabisa.... jibu liko wazi. Hata Burundi tu inayamaliza
 
Kiufupi mafuta yaliisha gunduliwa tanzania, bahati mbaya sio pemba! Ni maeneo ya huku bara, tunasubiri tangazo tuu!
 
Bahati mbaya nachangia kwa kimobile kidogo! Ila kuna hidden agenda nyiingi saana kuhusu suala la mafuta hapa tz!
 
Land Locked countries zinazoizunguka Tanzania hizo lita laki 2 haziwatoshi kabisa.... jibu liko wazi. Hata Burundi tu inayamaliza

Kama ume ni -quote vizuri nimetoa mfano "usio hai".
Ni kwa ajili ya hesabu ndogo tu za kumfanya aliye uliza kwanini yana hifadhiwa
aelewe why.
 
Ha ha,hizo NGO ni njia nyingine ya wizi tu.
Hakuna NGO inayo fanya kazi kwa makusudi iliyo anzishiwa,
waki jitahidi ni 10% watafanya ila 90% ni matumbo yao tu.

Naogopa sana kuwa tapeli.

Cha kusikitisha ni hicho brother, tupo kwenye msitu wa manyang'au....
Watz wengi ni wezi sana tumerithi toka kwa "viongozi" wetu,
upigaji ni moja ya tamaduni zetu mpya, ukiwa sio mpigaji watu wanakushangaa kama umejipaka kinyesi vile....
Bila kurekebisha eneo hili la utamaduni itakuwa kazi sana kufanya mabadiliko kwenye eneo lolote hata kiongozi wetu akiwa ni miongoni mwa mitume wale wakubwa kabisa katika masimulizi yetu ya dini au ya mizimu.
 
Inasemekana kwamba Mafuta yamegundulika ndani ya Tanzania.


Mungu sasa inatosha, ILAANI kidogo Tanzania.

Kwanini kutupa mafuta ilihali tu MAJUHA?
..
Mkuu, napenda sana watu wanaopost vitu vyenye AKILI humu jamvini, sio kushupalia huyu kasemaje kisiwa Cha Zimbabwe Sijui huyu kaloanisha nanii, lakini Mustakabali wa watanzania ambao uko ndani ya weledi wa uwezo wetu hatujaugusa hasa hasa..

Katika Orodha ya Mabilionea Wa Duniani moja Kati ya biashara zao kiongozi ni Mafuta Na pili Madini, tukatae tukubali mafuta Na Madini ni Nguzo Za uchumi wa serikali yoyote katika DUNIA ya Leo, kuongelea mafuta ni kuongelea vitu vyenye akili .. I support you..

Nirekebishe kauli kwamba Kwamba Mungu ailaani Tanzania kidogo, no Tanzania tumeshajilaani,kujichukia Na kujikataa tena sana tu si kidogo, Mwenyezi Mungu katupa kila kitu jamani, lakini sisi ndio tumejikataa Kwa kukubali kuongozwa Na watu Wenye fikra mfu.. Unajua ukiongizwa Na watu Wenye fikra mfu hata Jamii inakuwa ya kimisukule tu..

Sisemi Kwa Ubaya wala simwonei Mtu ila Kwa Sasa CCM iko madarakani, Na kuna watu maelfu tu wanajiita wakereketwa au washabiki Wa chama hiki, LAKINI count my words, CCM ikiondoka madarakani, chama kingine kikaingia Na kuwafungua wananchi macho Kwa kile chama hiki Na serikali yake vimewatendea wananchi wake, nakwambia hata wale wanaojiita wakereketwa Kama sio wakeketwa Wa chama hiki watajutia Na kulilia wakati wao walioupoteza kuunga mkono wasichokijua..I mean it

NCHI zilizoendelea zilishaapa kujiimarishia ichumi wake Kwa kuzifanya NCHI zinazoendelea kuwa soko Na mashinary zao. Na hii ikienda sambamba Na kuhakikisha zinanyimwa Elimu AMA ya darasani au ya kazini, hii ni pamoja Na kuwahadaa Vijana wao Wenye AKILI kutoka vyuoni Na kuwapatia dhihadi Za elimu (scholarship) Na kuhakikisha wanasomea Kada ambazo sio vumbuzi Na sizizo Na mguso filirishi. Na baada ya hayo huajiriwa Na serikali
Zao ka kukamatwa Na pepo Jamhuri..

Mpango huu ulikuwa wazi hata Mwalimu aliueleza sana sana, lakini kusema bila matendo hakusaidii mbele ya macho yake viwanda vikaanza kuuliwa ivi ivi akiona, vya nguo,vya nyama, vya zana Za kilimo Na hatimaye Leo tunashuhudia NCHI imeshageuzwa gulio la bidhaa Za nje, hadi vijiko..

Fikiria tu kwamba ili Mtu astawi Kwenye chama anahitaji fedha kutoka kwa wale wale wanaotuuzia vitu vyao, NCHI haina bajeti ya uchaguzi hadi viongozi wenu mletewe fedha Za kiwachagua unadhani hii sio LAANA ??!

Tanzania inahitaji Mtu anayejua Nini kiwe Nini na lini..

CCA
 
Ulikuwa hujazaliwa. Alikuwepo JK wa ukweli aka Mwalimu Nyerere.

Ha ha ha.
sina usemi,kesha pumzika huyo,na ambao hatukubahatika hata kumuona
na hatuamini katika "ukweli wa historia" (refer risala yoyote kumhusu marehemu msibani)
hatuamini kama aliwahi kuwepo mzalendo.
Nilio waona wanatosha kuamini Tanzania ni nchi yenye kila kitu ila haina watanzania.
 
Usidanganye watu. Nijibu yafuatayo na usiwe mshabiki:

1. Yamegundulika block gani
2. Operator gani ameyagundua?
3. TVD(total vertical depth) na MD(measured depth) ni ngapi?
4. Nipe size ya reservoir

Msiwe washabiki maandazi....

Process za exploration/drilling na discovery kwa bahati gas au mafuta yakiwepo tena offshore sio kama kukuna ngozi yako.....

Ni process nzito zinazohitaji resources kibao.

Acheni maneno ya vijiweni
Nyie ndo huamini kuwa maneno yasosemwa na authority ni uongo ni ya kijiweni, Ni ujinga tu kuambiwa kuwa nduguyo kafa kwa ajali unasubiri taarifa ya RPC ya kuthibitsha ajali na vifo ndo uamini, wala usijione kwa kutisha watu na technical terms kila mtu ana fani yake humu, kuwa zitazuia watu kuujua ukweli nenda Mtwara useme ujinga huo eti mafuta hayajagundulika offshore kama hata wakulima hawatakuona juha gani msomi asiyejua yliyo wazi namna hiyo?! Kama hujui fanya utafiti. Msomi kama wewe unasubiri waziri athibitishe ndiyo ukubali kuwa mafuta yapo! Ama kweli wasomi wetu hawa heri ya Mangungo wa Msovero. Au hujaona kampuni za ujenzi barabara za kigeni zikigundua madini kwenye kuchimba kokoto huchelewesha ujenzi zikigida madini ya majuha yasojua na kushangaashangaa TVD na MD yalipo madini kama wewe
 
Kwanza ni vizuri uelewe kuwa mafuta (crude oil) hajagunduliwa Tanzania mpaka sasa. kilichogunduliwani gesi asili. Pili, si kweli kwamba kuwepo kwa TIPER kulikuwa na faida kiuchumi. Kiwanda hicho kilikuwa kinaendeshwa kwa hasara kutokana na teknolojia yake kuwa duni, kiwanda uwezo wake ulikuwa mdogo mno kuweza hata kukidhi mahitaji ya nchi (It lacked economics of scale) na ukilinganisha na kuagiza mafuta yaliyosafishwa kutoka nje gharama zilikuwa nafuu zaidi kuagiza kuliko kusafisha mafuta ghafi katika kiwanda cha kiwanda cha TIPER. kwa mtazamo huo utaona kuwa ilikuwa ni busara kukifunga kiwanda hicho kuliko kutumia kodi za watanzania kufidia hasara. Natumai maelezo haya yamekuweka sawa.
 
Hizo lita 200,000 zina pelekwa wapi?

Hizo lita 200,000 za surplus zitajaa kwenye ma tenki mpaka zitamwagika unless kila siku ya Mola unajenga tenki jipya la lita 200,000, which is demonstrably senseless! Kama rate ya kuzalisha inazidi rate ya consumption by 200,000 liters kwa siku basi hakuna haja ya kuzalisha surplus ya lita 200,000 ambazo humuuzii mtu, yatabubujika! hahahaaaa....

Kumbuka hizo marketing companies hawana uwezo wa kutunza mafuta mengi kwa wakati mmoja.
Hata kampuni ya refining yenyewe haina uwezo wa kuhifadhi surplus ya mafuta yanaoongeza kwa lita 200,000 kwa siku, yataenda yakiongezeka infinitely mwishowe yata over flow na kupita chini ya milango kuingia maofisini mwa kiwanda hatimae watu watazama kwenye refined mafuta! Do you understand me? There is no such thing as "wanasafisha mafuta halafu wanahifadhi kidogo" ili kusubiri ya kwenye vituo yauzwe... doesn't make a shred of sense!
 
tanzania kweli ni taifa la majuha tumebarikiwa rasilimali nyingi sana lakini ujuha wetu ndo unatufanya tunaendelea kuwa maskini,kwa mfano swala la madini kila siku najiuliza ni kwanini wasipeleke watu nje ya nchi kujifunza mambo ya madini na baada ya miaka kadhaa tukaweza kuendesha wenyewe migodi yetu,ukienda kwenye makampuni ya madini mbalimbali utakuta wanaleta watu wa kada zingine kama vile watu wa mazingira,ugavi,uhasibu wakati kuna watanzania ambao wanaweza kufanya kazi hizo kweli taifa letu hili ni ujuha tu kuanzia kwa wananchi mmojamoja hadi kwa viongozi wetu,kwanini nasema hivi kwa sababu sisi kama wananchi wa kawaida kabisa tunaweza kufanya mahamuzi ambayo baadaye yatabaki kuwa historia kwa vizazi vijavyo tuondokane na UJUHAAAAAAAAAAAA

Kwa maana hiyo hakuna sababu ya kung'ang'ania hilo ziwa Nyasa. Wapeni tu hao wamalawi manake hakuna faida yoyote hata kama kuna mafuta. May be wamalawi watapiga hatua zadi na kufaidika na hilo wese kuliko bongo
 
Tunatokaje hapa tulipo, coz ni uzembe kutegemea ccm wafanye lolote kutatua haya wakati wao ndo wametengeneza haya matatizo
 
Kwanza ni vizuri uelewe kuwa mafuta (crude oil) hajagunduliwa Tanzania mpaka sasa. kilichogunduliwani gesi asili. Pili, si kweli kwamba kuwepo kwa TIPER kulikuwa na faida kiuchumi. Kiwanda hicho kilikuwa kinaendeshwa kwa hasara kutokana na teknolojia yake kuwa duni, kiwanda uwezo wake ulikuwa mdogo mno kuweza hata kukidhi mahitaji ya nchi (It lacked economics of scale) na ukilinganisha na kuagiza mafuta yaliyosafishwa kutoka nje gharama zilikuwa nafuu zaidi kuagiza kuliko kusafisha mafuta ghafi katika kiwanda cha kiwanda cha TIPER. kwa mtazamo huo utaona kuwa ilikuwa ni busara kukifunga kiwanda hicho kuliko kutumia kodi za watanzania kufidia hasara. Natumai maelezo haya yamekuweka sawa.

Well said. Nimewauliza maswali hapo juu wanaosema mafuta yamegunduliwa hawajanijibu maana majibu hawana...... Ushabiki maandazi
 
Tigga mumba na speaker! Suala la mafuta siku zoote ni nyeti saana, rais wa nchi husika ndio anakuwa na mandate kutangaza

Sio kweli...... Sio rais wa kutangaza..... Rais atatangaza kisiasa tu baadae kabisa. Amini nakwambia tukipata mafuta in less than a day taarifa zitatoka. Na kingine kumbuka haupati diesel au petrol chini. So production inahitajika na ni anothet project
 
Usidanganye watu. Nijibu yafuatayo na usiwe mshabiki:

1. Yamegundulika block gani
2. Operator gani ameyagundua?
3. TVD(total vertical depth) na MD(measured depth) ni ngapi?
4. Nipe size ya reservoir

Msiwe washabiki maandazi....

Process za exploration/drilling na discovery kwa bahati gas au mafuta yakiwepo tena offshore sio kama kukuna ngozi yako.....

Ni process nzito zinazohitaji resources kibao.

Acheni maneno ya vijiweni

tueleze basi mafuta yamegundulika wapi, maana nimesoma hizo link naona habari za gesi tuu huko mtwara na si mafuta.msaada kama unajua
 
Back
Top Bottom