Uchaguzi 2020 Uchambuzi wa hotuba ya Lissu - Kawe

eddy

JF-Expert Member
Dec 26, 2007
15,050
9,969
Leo nimefurahishwa Lissu kaongea huku ametulia tena kawa mpole, naona keshasoma upepo.

Katika hotuba yake naomba nichambue kidogo maelezo yake, kimsingi hayo aliyoyaelezea yaliwahi kutekelezwa na awamu zilizopita na yakashindikana, ni maneno yakuombea kura tu sio yakiutekelezaji.

1. Kuhusu fao la kujitoa, zipo changamoto za kiutendaji hasa uwezo wa mifuko yenyewe hivyo anaposema mtu ukipugwa tu ukachukue fedha zako. Labda angetueleza kiwango cha labour turnover kikoje, kama wanao acha kazi ni wengi kuliko wanao ajiriwa basi itakuwa pyramid financing, itafika sehemu ita collapse yenyewe. Kwanza tuangalie kwanini kijana afanyekazi miaka kumi halafu apoteze ajira yake na iwe mwisho wa tumaini lake kimaisha, tatizo ni nini? Kinacho mfanya asifanye kazi hadi uzeeni ni nini tunapaswa kuangalia "job security" ya watumishi wetu na sio kukimbilia kuwapa fedha ili wakafie mbele. Kabda ya kufikia huo uamuzi tunapaswa kuwa na labour data base kwanza tujue uwezo wa nguvukazi ya taifa.

2. Vitambulisho vya machinga, kule mbeya alisema atavifuta leo kasemea dosari zake hivyo naamini wazo lake la kuvifuta kaliondoa hivyo siwezi kuzungumzia kwani hajasema atafanya nini juu ya hilo

3. Kuhusu upunguzaji kodi, naona kaongea kienyeji sana labda mikutano ijayo atalitolea ufafanuzi, kasema importers wana kodi 15 yeye atazifuta ibaki moja, kwa kuwa kazitaja kwa idadi basi anazijua vizuri ni vyema akatuambia atafuta kodi zipi? Kwa uchache kuna import duty, exercise duty, vat, income tax etc. Hizi kodi zingine ni mfumo wa kimataifa chini ya WTO hiyo mifumo inafanana duniani sasa sijui anamaanisha Tanzania itajiondoa WTO, ipo mifumo ya SADC na EAC common customs kauli yake ni too skeleton na haijitoshelezi. Mfumo huu aliutumia Rais Mwinyi na ndio chanzo cha kuua viwanda vyetu vya ndani sasa anataka kuturudisha kulekule kwenye ruksa sio?

4. Kulipa fidia kwa maana ya kutibu vidonda, akumbuke kuna wahindi walinyanganywa nyumba zao wakati wa azimio la arusha nao watafidiwa? kuna makampuni ya Rockefeller na Mackenzie yalitaifishwa mashamba ya chai kahawa pareto je nayo yatafidiwa? vipi kuhusu bank ya Barclays UK ambayo ilitaifishishwa na kuanzishwa BOT nayo itafidiwa? Mgodi wa Geita Mine nao ataurudisha kwa Wajerumani? Ni vyema Chadema wakatafakari upana wa tatizo wanalotaka kulitengeneza.

5. Kuvutia wawekezaji, huu mfumo ndio alioutumia mzee wetu marehemu Mkapa, sote tunajua yaliyotupata na hatujasahau naomba usiturudishe huko, hakuna mazingira rafiki ya uwekezaji tusidanganyane. Kwanza ukilegeza mfumo wa kodi hakuna mwekezaji atakuja wekeza labda wachimba mafuta gesi na dhahabu. Mambo amabayo yeye Lissu amekuwa akiyapiga vita tangu zamani huko ubelgiji wamempa nini? Kiujumla mawazo ya Lissu ni yakienyeji sana na yaliyopitwa na wakati.
 
Hapo umechambua au unasema haiwezekani? Unadhani unaongea na wajinga? Tumeshasome codes

Wakati wa Elimu Bure, mlisema haiwezekani. Alipoingia magufuli akajaribu.

Embu Chambua basi na Hotuba ya Magufuli leo tujue akili yako inawaza nini.

Tumeshtuka.

#Niyeye
 
Nimesoma kwa makini hapo kwenye namba nne nikajua unaongozwa na mihemko. Amesema fidia kuanzia 2015-2020. Sasa unaongelea mambo ya BoT na yaliyotokea miongo kadhaa inahusianaje na hotuba ya leo?

Oh! Usimwamini mwanasiasa yeyote.
 
Lissu siyo mzalendo hata kidogo, ukiangalia sera zake zipo kujenga taifa tegemezi na sio taifa linalojitegemea. Tunataka Tanzania yenye uwezo wa kujitegemea kwa kila kitu katika siku za usoni, na sio taifa tegemezi.
 
Nimesoma kwa makini hapo kwenye namba nne nikajua unaongozwa na mihemko. Amesema fidia kuanzia 2015-2020. Sasa unaongelea mambo ya BoT na yaliyotokea miongo kadhaa inahusianaje na hotuba ya leo?

Oh! Usimwamini mwanasiasa yeyote.
Hapo kutaka kuleta imbalance
 
Taratibu naona mnaanza kupaki basi, Lissu fanya mashambulizi makali sana. Na tunaomba aandaliwe mubashara kipindi kwenye TV ajibu maswali kwa ufasaha. Hayo uliyoongea ni kutaka kufananisha mambo ya Lisu na udhaifu wa CCM. Lissu atatumia modality yake kufikia ufanisi wa anachokisema. Huwezi kuifananisha cdm na chama cha wapigaji CCM.
 
Lissu siyo mzalendo hata kidogo, ukiangalia sera zake zipo kujenga taifa tegemezi na sio taifa linalojitegemea. Tunataka Tanzania yenye uwezo wa kujitegemea kwa kila kitu katika siku za usoni, na sio taifa tegemezi.
Huyo ni Robert Amsterdam wa Mbagala.
 
Nimesoma kwa makini hapo kwenye namba nne nikajua unaongozwa na mihemko. Amesema fidia kuanzia 2015-2020. Sasa unaongelea mambo ya BoT na yaliyotokea miongo kadhaa inahusianaje na hotuba ya leo?

Oh! Usimwamini mwanasiasa yeyote.
Toeni ilani yenu hata kwenye mtandao tuisome kama anayosema yamo au hayamo
 
Mkuu nimeishia kusoma hapo kwenye fao la kujitoa,eti unasema fao la kujitoa haliwezekani kwa kuwa mifuko Ina pesa kidogo kwani mtu anayejitoa anachukua pesa ya mfuko au pesa zake alizoweka hapo?
Nimesema badala ya kukimbilia kuwalipa wakafie mbele tujiulize kwanini wanafukuzwa kazi? Kule kahama vijana 1600 walifukuzwa kazi kupisha wazungu 300 walioletwa kutoka ulaya Mambo Kama hayo hatuwezi kukubali
 
Lissu siyo mzalendo hata kidogo, ukiangalia sera zake zipo kujenga taifa tegemezi na sio taifa linalojitegemea. Tunataka Tanzania yenye uwezo wa kujitegemea kwa kila kitu katika siku za usoni, na sio taifa tegemezi.
Mkuu unajua nini maana ya elimu kwa maana ya ujuzi na maarifa badala ya hii ya vyeti inayotolewa na Magufuli? Au wewe unadhani tutajitegemea kwa kukopa na kujenga madaraja na reli? Mkuu kujitegemea kunatokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa watu wako.ficha ujinga
 
Mkuu nimeishia kusoma hapo kwenye fao la kujitoa,eti unasema fao la kujitoa haliwezekani kwa kuwa mifuko Ina pesa kidogo kwani mtu anayejitoa anachukua pesa ya mfuko au pesa zake alizoweka hapo?
Nimesema badala ya kukimbilia kuwalipa wakafie mbele tujiulize kwanini wanafukuzwa kazi? Kule kahama vijana 1600 walifukuzwa kazi kupisha wazungu 300 walioletwa kutoka ulaya Mambo Kama hayo hatuwezi kukubali
 
Nimesoma kwa makini hapo kwenye namba nne nikajua unaongozwa na mihemko. Amesema fidia kuanzia 2015-2020. Sasa unaongelea mambo ya BoT na yaliyotokea miongo kadhaa inahusianaje na hotuba ya leo?

Oh! Usimwamini mwanasiasa yeyote.
Hawa ni watu waajabu kidogo 😀😀😀😀
 
Nimesema badala ya kukimbilia kuwalipa wakafie mbele tujiulize kwanini wanafukuzwa kazi? Kule kahama vijana 1600 walifukuzwa kazi kupisha wazungu 300 walioletwa kutoka ulaya Mambo Kama hayo hatuwezi kukubali
Mkuu Kuna wengine tunafanya kazi ili tupate mtaji au pesa ya kujenga.mfano unapata kazi unaingia mkataba wa miaka mitano mitano,nssf unapeleka 3m every month kwa maana ya yako 1,5 na mwajiri 1.5,kwa mwaka unakuwa umeweka 36 m so baada ya miaka mitatu unakuwa na 108 unaacha kazi unachukua pesa yako unaenda kufanya Mambo mengine.Nyuma zangu tatu za hapa dar mbili nimezijenga kwa mtindo huu
 
Lissu siyo mzalendo hata kidogo, ukiangalia sera zake zipo kujenga taifa tegemezi na sio taifa linalojitegemea. Tunataka Tanzania yenye uwezo wa kujitegemea kwa kila kitu katika siku za usoni, na sio taifa tegemezi.
Uzalendo ni nini ndugu yangu? Mana mnaongea ongea tuu inawezekana hata maana ya uzalendo huijui
 
Mkuu Kuna wengine tunafanya kazi ili tupate mtaji au pesa ya kujenga.mfano unapata kazi unaingia mkataba wa miaka mitano mitano,nssf unapeleka 3m every month kwa maana ya yako 1,5 na mwajiri 1.5,kwa mwaka unakuwa umeweka 36 m so baada ya miaka mitatu unakuwa na 108 unaacha kazi unachukua pesa yako unaenda kufanya Mambo mengine.Nyuma zangu tatu za hapa dar mbili nimezijenga kwa mtindo huu
Kwahiyo mshahara wako Ni 15m kwa mwezi sawa na 180m kwa mwaka na 9000m kwa miaka mitano bado unalilia 108m ili ujenge?
 
Leo nimefurahishwa Lissu kaongea huku ametulia tena kawa mpole, naona keshasoma upepo.

Katika hotuba yake naomba nichambue kidogo maelezo yake, kimsingi hayo aliyoyaelezea yaliwahi kutekelezwa na awamu zilizopita na yakashindikana, ni maneno yakuombea kura tu sio yakiutekelezaji.

1. Kuhusu fao la kujitoa, zipo changamoto za kiutendaji hasa uwezo wa mifuko yenyewe hivyo anaposema mtu ukipugwa tu ukachukue fedha zako. Labda angetueleza kiwango cha labour turnover kikoje, kama wanao acha kazi ni wengi kuliko wanao ajiriwa basi itakuwa pyramid financing, itafika sehemu ita collapse yenyewe. Kwanza tuangalie kwanini kijana afanyekazi miaka kumi halafu apoteze ajira yake na iwe mwisho wa tumaini lake kimaisha, tatizo ni nini? Kinacho mfanya asifanye kazi hadi uzeeni ni nini tunapaswa kuangalia "job security" ya watumishi wetu na sio kukimbilia kuwapa fedha ili wakafie mbele. Kabda ya kufikia huo uamuzi tunapaswa kuwa na labour data base kwanza tujue uwezo wa nguvukazi ya taifa.

2. Vitambulisho vya machinga, kule mbeya alisema atavifuta leo kasemea dosari zake hivyo naamini wazo lake la kuvifuta kaliondoa hivyo siwezi kuzungumzia kwani hajasema atafanya nini juu ya hilo

3. Kuhusu upunguzaji kodi, naona kaongea kienyeji sana labda mikutano ijayo atalitolea ufafanuzi, kasema importers wana kodi 15 yeye atazifuta ibaki moja, kwa kuwa kazitaja kwa idadi basi anazijua vizuri ni vyema akatuambia atafuta kodi zipi? Kwa uchache kuna import duty, exercise duty, vat, income tax etc. Hizi kodi zingine ni mfumo wa kimataifa chini ya WTO hiyo mifumo inafanana duniani sasa sijui anamaanisha Tanzania itajiondoa WTO, ipo mifumo ya SADC na EAC common customs kauli yake ni too skeleton na haijitoshelezi. Mfumo huu aliutumia Rais Mwinyi na ndio chanzo cha kuua viwanda vyetu vya ndani sasa anataka kuturudisha kulekule kwenye ruksa sio?

4. Kulipa fidia kwa maana ya kutibu vidonda, akumbuke kuna wahindi walinyanganywa nyumba zao wakati wa azimio la arusha nao watafidiwa? kuna makampuni ya Rockefeller na Mackenzie yalitaifishwa mashamba ya chai kahawa pareto je nayo yatafidiwa? vipi kuhusu bank ya Barclays UK ambayo ilitaifishishwa na kuanzishwa BOT nayo itafidiwa? Mgodi wa Geita Mine nao ataurudisha kwa Wajerumani? Ni vyema Chadema wakatafakari upana wa tatizo wanalotaka kulitengeneza.

5. Kuvutia wawekezaji, huu mfumo ndio alioutumia mzee wetu marehemu Mkapa, sote tunajua yaliyotupata na hatujasahau naomba usiturudishe huko, hakuna mazingira rafiki ya uwekezaji tusidanganyane. Kwanza ukilegeza mfumo wa kodi hakuna mwekezaji atakuja wekeza labda wachimba mafuta gesi na dhahabu. Mambo amabayo yeye Lissu amekuwa akiyapiga vita tangu zamani huko ubelgiji wamempa nini? Kiujumla mawazo ya Lissu ni yakienyeji sana na yaliyopitwa na wakati.
Lisu tapeli wa kisiasa
 
Back
Top Bottom