Uchambuzi - Sheikh Ponda Issa Ponda

Uchambuzi - Sheikh Ponda Issa Ponda

Mwenyezimungu atamlipa Sheikh Ponda kwa Juhudi zake za Kutetea Mali za Waislamu.
Huyu Sheikh ni mfano mkubwa sana wa Kuigwa na Kizazi hiki.
Na Serikali itambue kuwa Kila Wakifanyacho juu ya Huyu Sheikh kitakuja warudia wao kwa wao.
Haki ya mtu haipotei bure. Iko siku watayaona haya madhila wanayompa huyu muungwana.

Mungu yuko pamoja nae hata km MAKAFIRI watachukia.

Shukran sana Mzee Mohamed kwa Taarifa hii
uko sahihi kahtan in shaa Allah I like sheikh ponda na wapiganaji wote kama yeye takbiiir
 
Ni Kweli Kabisaa Hilo Ndilo Chimbuko La Sheikh Ponda Issa Ponda Kuandamwa Na Vyombo Vya Dora!! Lkn SWALI, Hivi Kama Hili Suala Halina Mkono Wa BAKWATA, Ambao Ndio Walitoa Maagizo Ya Kumdhibiti Sheikh Ponda, Kutokana Na Kusimamia Kwake Kwa Dhati Mali Za Waislam, Ili Ziweze KULETA Maendeleo Kwa Jumuiya Nzima Ya Waislam Na Dini Yao!! Badala Ya Kutumiwa Na BAADHI Ya Viongozi Wa BAKWATA Kwa Maslahi Yao BINAFSI!! Najiuliza Hivi DPP ANAWEZA Vipi KUZUIA DHAMANA Ya Sheikh Ponda!! Kwa Zaidi Ya Mwaka Mzima, Huku BAKWATA WAMEKAA Kimyaa!!! Kama Lenyewe Ndilo Baraza Kuu La Waislam Wa Tanzania!!! Iweje Sheikh Ambaye ANAYESEMA UKWELI Na Kuwatia Hamasa Waislam Wenziwe Kudai Mali Zao Zilizoporwa, Anakamatwa Na Waumini Wenziwe Na Kufunguliwa Mashitaka Ya Wizi, Wa Nondo, Kokoto, Matofali, Mchanga, Mbao, Mabati Na Misumari!! Na Kunyimwa DHAMANA Pale Mahakama Ya Kisutu!! Hadi Hukumu Ilipotoka Sheikh Ponda Akafungwa Kifungo Cha Nje Mwaka 1 Na Waumini Wengine Cha GEREZANI!! Wkt. Sheikh Ponda AKIENDELEA Na Kifungo CHAKE!! Ndio Yakazuka Hayo Ya Moro!! Eti Anashitakiwa Kwa Kukiuka Masharti Ya Hukumu Ya Mahakama Ya Kisutu!! Na KUFANYA Mkutano Usio Na Kibali, Kusema Maneno Ya UCHOCHEZI Na Yenye Kuudhi Watu Wengine!! Tukashuhudia Sheikh Ponda Akisafirishwa Kwa CHOPA Toka SEGEREA Mahabusu, Kwenda MAHAKAMANI Moro, Mara IKAWA Kwa Msafara Wa Magari!! Hatimaye Mahakama Ya Kisutu Akalitupa Shitaka La Kukiuka Masharti Ya Hukumu Ya Kifungo Cha Nje, Iliyotolewa Nayo!! Imebakia Hayo Ya Moro!! Ndio Akahamishiwa Mahabusu Ya Moro HADI Leo, Ambapo Ndio Tarehe Ya Hukumu Yake!!! Kama BAKWATA Haina Mkono Ktk. Kadhia Hii, Mbona Wako Kimyaa!!!?? Je, TAASISI Hiyo Sio Ya Waislam Na Mali Zao!!!??? Je, BAKWATA Iko Kwa Maslahi Ya Waislam Wa Aina GANI TANZANIA!!!?? Nini Kifanyike, Kwanza Waislam Wa TANZANIA Tudai Baraza La Waislam Wa TANZANIA Lenye MFUMO Ambao Linashirikisha Waislam WOOTE, Taasisi Zoooote, Jumuiya Zoooote Na Madhehebu Yooote!! Pili Kuundwa Kwa Baraza Lenye Sura, Malengo, Fikra, Mtazamo Na UMOJA! Kwa Kuwashirikisha Waislam WOOTE NCHINI, Ktk. Mchakato Wa Undwaji Wake Na Kupatikana Viongozi Wake!! SIO KAMA ILIVYO Sasa, WATU WACHACHE Ndio Wanaamua Na Kusimamia Mambo Ya Waislam WOOTE NCHINI!! Tatu Waislam Tuache UNAFIKI, Huu Ndio Unaotutafuna Jmn! HIVI Madhira YOTE Haya, Tokea Miaka Ya 90 Pale Wahadhiri Wa Kiislam Walipofungwa Miaka 3 GEREZANI Kwa Mashitaka Ya Kuvunjwa Mabucha Ya Nyama Ya Nguruwe!! Ambao Wakikamatwa Pale Msikiti Wa Mwembechai, Akiwepo Na Sheikh Mazinge Shaban! Baadae Wakaachiwa Kwa Msamaha Wa Rais MWINYI!! Lkn Likifika Suala La Uchaguzi Wa Viongozi, Tunaonekana Kuyumbishwa Na Maslahi YETU BINAFSI Badala Ya WOOTE!!! Kama TUTAENDELEA Kuwa WANAFIKI Tu, Basi Tukubali Tu Kudhurumiwa Na Kunyanyasika MILELE!!!!!

Ksuley 1411,
Unaweza kupata mengi kuhusu BAKWATA hapo chini:
Mohamed Said: Historia ya Bakwata - Mtambani -Part 1
 
Hii makala ya zamani kama inasema Sheikh Ponda amefungwa mwaka mmoja. Nakumbuka miaka miwili iliyopita Butiama nilikuwa naongea na waandishi wa habari naiomba Serikali imuachie huru Sheikh Ponda.Niliongea kuhusu mambo mawili siku ile:Magufuli na Sheikh Ponda. Kuhusu Magufuli watu walikuwa wameanzisha vugu vugu la kumfukuza kazi wanasema Magufuli hana rafiki,kazi yake kubwa ni kusema,hii nyumba imejengwa karibu na barabara,nataka ibomolewe. Nikaongea kumtetea Magufuli. Kuhusu kuwafunga Waislamu hii siyo mara ya kwanza.Wakati katika kampeni ya Mkapa walikuwepo Waislamu waliofungwa kwa akili ya maandamano. Na mimi nilisema wakati ile CCM sasa hivi haina tatizo kubwa kuliko wale Waislamu waliofungwa. Na ni nasema wale Waislamu wataachiwa huru kabla ya siku ya kupiga kura. Na kweli ndiyo ilivyokuwa wale Waislamu waliachiwa kabla ya Uchaguzi..


Sema basi waachiwe na hawa kabla ya uchaguzi.mimi ni muislam na kura yangu hawapati.


cc foxy

Swissme
 
Tatizo la Shaikh Ponda na wanaharakati ni kutoangalia maslah na mafsad
 
Sema basi waachiwe na hawa kabla ya uchaguzi.mimi ni muislam na kura yangu hawapati.


cc foxy

Swissme
Leo ndiyo hukumu itasomwa, kuna dalili za kuachiwa huru ili kupata kura zetu sisi waislamu tunaojitambua, wameshachelewa.
 
Si waislamu wakaombe serikalini kiwanja kingine?Mbona mapori yapo kibao huko Mvuha na Kinole?

Hyo ndio ukomo wa Akili yako katika kufikiria. Kwanini wawe ombaomba wakati mali yao wanayo????
Haki haiombwi ila haki inachukuliwa.
Tatizo la kubwa la maendeleo ya waislam Tanzania ni Bakwata ambao ni kutumika kama tawi la CCM!
 
kwanini wasiende wao uko mapolini?we unapumuliwa mgongoni nenda kwenyefani yako.....

Haya endeleeni kupigania hiyo haki. Kwa taarifa yako Ponda ataendelea kukaa jera kwa maslahi ya taifa.

Chagua Lowasa....
 
  • Thanks
Reactions: T11
Si waislamu wakaombe serikalini kiwanja kingine?Mbona mapori yapo kibao huko Mvuha na Kinole?

Hapa Mkafiri anaona katoa wazo la maana sana.

Kwa busara hizi za kuku Ndio maana mnapeleka wake zenu kuombewa na Viongozi wenu wa Imani kisha kubwa zima linaambiwa "mpitie mkeo baada ya masaa manne" nalo linashukuru na kutoa pesa za maombi juu yake.

Nyie viumbe siku mkiamka dunia Inamalizika kabisa.
 
Si waislamu wakaombe serikalini kiwanja kingine?Mbona mapori yapo kibao huko Mvuha na Kinole?

Ingekuwa ni wewe ndiye mmiliki uhalali wa kiwanja hicho na ikatokea mtu anakitaifisha utakubali kichukuliwe nawe ukayafuta kingine huko maporini?.Kwa muislam ukikubali kudhulumiwa bila kutetea haki yako nawe umetenda dhambi ya kutopingania haki yako.
 
Haya endeleeni kupigania hiyo haki. Kwa taarifa yako Ponda ataendelea kukaa jera kwa maslahi ya taifa.

Chagua Lowasa....
Huu mvinyo wa dini unalewesha kuliko viroba? unafahamu maana ya ardhi au mali za wakfu? Taifa lipi linalonufaika kwa Ponda kukaa jela?
 
Sooth,
Ukianza na ''Wewe Mzee...'' ni kuwa umeghadhibika na umetokwa na staha.
Ukishaniita, ''Mzee,'' basi tambua nastahili heshima.

Bila ya heshima hatutaweza mimi na wewe kufanya mjadala wa maana.
Labda ukisoma hapa chini tutaelewana kuhusu uchaguzi:

Mohamed Said: MBUNGE MTARAJIWA WA NEWALA: MWALIMU JAFFAR MNEKE KIJANA MDOGO MSOMI WA MASUALA YA DIPLOMASIA

Mohamed Said: IS TERRORISM A PAWN FOR THE GENERAL ELECTION IN TANZANIA?

Mohamed Said: KUTOKA JF: WAISLAM NA UCHAGUZI MKUU 2015 2

Ahsante sana Sheikh Mohamedi Said, wewe ni kati ya wasomi wachache kama sio wa kwanza kufanya uchambuzi wa kina juu ya uhusiano wa Serikali, Chama na bakwata kwa upande mmoja na matatizo ya waislamu kwa upande mwingine na uhusiano huo unavyoendelea kuathiri maendeleo ya waislamu na uislamu. Makala zako huwa za kusimua sana.
 

Historia ya Waislam wa Tanzania itakapokuja kuandikwa


"Historia ya Waislam wa Tanzania itakapokuja kuandikwa," kwani historia ya Waislam wa Tanzania haijaandikwa?

Tumesoma mashuleni uislam Tanzania umeanza karne ya tisa or thereabout, zaidi ya miaka elfu moja iliyopita, historia hiyo itakuwa haijaandikwa?

Anajitahidi tahidi sana kuandika mambo ya Uislam wa Tanzania huyu Muhamed Said, tatizo shule yake nayo ni ya mashaka mashaka sana. Kwa hiyo unapomsoma sentensi ya kwanza tu, kama hapo juu, anapoteza credibility ya kuendelea kumsoma.

Ulitakiwa kusema "historia mpya" itakapokuja kuandikwa, au kwa lugha nyingine "revisionist history..." Hiyo haikufungi kuulizwa na msomaji historia ipi hiyo ambayo haijaandikwa, vinginevyo inabidi uwe very specific ni kipindi ama historia ipi hiyo unadai haijaandikwa.

"Historia itapokuja kuandikwa..." inatumika kwa tukio linaloendelea au lililotokea muda mfupi sana ambapo bado hakujawa hata na nafasi ya kusema historia yake imeandikwa. Mfano, "historia ya uchaguzi wa Urais wa mwaka huu itakapokuja kuandikwa..." Umeelewa bwana Muhamed Said?
 
Back
Top Bottom