Uchambuzi: CCM hesabu zimekataa kusomeka?

Uchambuzi: CCM hesabu zimekataa kusomeka?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
12,151
Reaction score
44,081
Wakati wa kampeni sasa unewadia, kila kitu kiko wazi na kitaendelea kuwa wazi. Hapa ni uchambuzi mfupi sana kuelezea namna mahesabu ya CCM yalivyokwenda kombo mpaka kufikia sasa.
Kifupi hesabu zilizopigwa na CCM hapo kabla hazisomeki kabisa. Kwa mfano.

1/ MCHAKATO WA KUTEUA MGOMBEA URAIS.

Mpango wa CCM ulikuwa ni kumpata mgombea wake wa urais na hapo hapo wote watakaoshindwa wabaki ndani ya CCM ili kuleta ushindi.

Pasipo kutegemea kabisa, Edward Lowassa akiwa ndiye mgombea mwenye nguvu, ushawishi na watu wengi zaidi ndani ya CCM aliamua kuhamia CHADEMA na sasa ndiye mgombea urais wa CHADEMA.
Hili ni pigo zito sana kwa CCM kimahesabu.

2/ KUSAMBARATIKA KWA UKAWA.

CCM ilipanga na kujizatiti kabisa kuhakikisha UKAWA inavunjika kabla ya kampeni kuanza, mahesabu ya CCM yalionyesha kuwa ni rahisi sana kushinda kama wapinzani hawatakuwa pamoja. Bahati mbaya sana kwa CCM hilo halijatokea na UKAWA wako pamoja, tena imara zaidi. Hili ni pigo kubwa sana kwa CCM kimahesabu.

3/ MGOMBEA MWENZA MWANAMKE.

CCM kwa makusudi kabisa kiliteua mgombea Mwenza mwanamke(Samia Suluhu) kwa lengo la kutafuta kura za wanawake, ikitegemea kuwa ni rahisi sana kuingia kwenye kampeni kwa hoja ya kuwa CCM inawajali sana wanawake.

Bahati mbaya sana kwa CCM, tayari chama cha ACT kimemteua mwanamke(Anna Nghwira) kuwa mgombea wake wa urais ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama hicho, hivyo kuua kabisa agenda ya CCM ya kutaka kutumia uanamke kama kigezo cha kupata kura kwa wanawake wasiokuwa na upeo mkubwa.

Bahati mbaya kabisa kwa CCM ni kuwa mgombea wake mwenza(Samia Suluhu) sio mwanasiasa maarufu au mwenye ushawishi, hakubaliki kabisa kwa wazanzibar na anafahamika zaidi Tanzania bara kama mtu aliyetumika kuharibu maoni ya watanzania katika mapendekezo ya rasimu ya katiba, wakati wa bunge maalum la Katiba.
 
CCM hata sisi wenyewe tunajua kuwa mtiti wa mwaka huu ni kiboko, tumaini letu limebaki
kwa mwenyekiti wetu kutumia gori la mkono kwa refarii NEC.
 
Kwa mtanzania yyte mwenye akili nzuri na mapenzi mema kwa taifa hili na uzao wake hawezi kuxhagua mgombea au chama klicho simamia kwa nguvu zote kuikataa katiba tunayotka wananchi! Hiyo misululu yao wakachimbie mawe huko. Na hizo pombe zao watazinywa sana wakiwa mtaani wakijiliwaza baada kubwagwa na hasira za watz!!
 
Jaman hivi ule wimbo wa ccm wa "TUMEJIPANGA MWAKA HUU WATAISOMA" hv kweli kwel msanii aliyeuandaa hakuwageuka hawa jamaa?
 
Uchambuzi wa kisomi sana huu. Umesahau na hoja ya MGAO WA UMEME WA MASAA 13 kwa siku. Huu unaimaliza CCM asubuhi kabisa, saa nne Lowassa anaanza sherehe
 
Una hoja nzuri, nimeipokea.

Kweli kabisa hata mm nakubaliana naye,huyo mgombea mwenza ndo walijichanganya kabisa kwa sababu ndo alikuwa makamu mwwnyekiti bunge la katiba,ushiriki wake ndo chanzo cha kuanzishwa UKAWA.
 
Ccm ni kama kuku wa kienyeji anayemilikiwa na mchunga ngombe kazi yake ni kula ndoroobo wanaouma ngombe na mbuzi akinenepa analiwa yeye kama chakula cha mgeni, ccm ishanenepeana inabidi lowasa aile kichwa kiwe kitoweo cha mgeni wa ikulu ukawaaaa.
 
Wakati wa kampeni sasa unewadia, kila kitu kiko wazi na kitaendelea kuwa wazi. Hapa ni uchambuzi mfupi sana kuelezea
.
.
Tanzania bara kama mtu aliyetumika kuharibu maoni ya watanzania katika mapendekezo ya rasimu ya katiba, wakati wa bunge maalum la Katiba.
Mkuu tafadhali tufafanulie kwa undani zaidi - wewe hupo katika kamati hipi ya CCM inayo kufanya uamini kwamba mahesabu yanawapiga chenga? Hivi unaijua vizuri CCM au unaisikia kwenye radio tu, come October mtashangaa. Mnacho sahau ni kwamba Chama tawala akitegemei mbinu za kitoto za kutumia mapandikizi kwenye social networks wenye alias names lukuki kuzuga wasomaji,pili hawategemei magazeti ya kuchonga kufikisha ujumbe kwa wapiga kura walio wengi vijijini ambao hawana mihemuko ya kijinga jinga ya kisiasa, Chama tawala kipo level headed kinajua wapi pa kuwa corner wapinzani wake wa kweli na wale wanaopania 2 get even come rain or shine! Sooner or later they gonna regret their own FOLLY.

Narudia kuwakumbusha kwamba killer tactics za kampein ya CCM zipo kwenye grassroots za viongozi wao huko vijijini sio mijini,wanakwenda kwa wapiga kura walio wengi na wanahamasishwa kweli kweli, oh yes bado wanategemea a stone age mbinu kufikisha ujumbe wao huko vijijini mbinu hizo ni effective by 100%.
 
Shida ya JF ni kwamba wengi humu ni watoto. Hawajui historia ya Nchi hii zaidi ya kuota Ndoto ya kupewa maisha bora na UKAWA.

Ukiwauliza kwa nini CCM iondoke madarakani wanasema iondoke tu kama kula na wengine wale! UTOTO!

Wakati wa kampeni sasa unewadia, kila kitu kiko wazi na kitaendelea kuwa wazi. Hapa ni uchambuzi mfupi sana kuelezea namna mahesabu ya CCM yalivyokwenda kombo mpaka kufikia sasa.
Kifupi hesabu zilizopigwa na CCM hapo kabla hazisomeki kabisa. Kwa mfano.

1/ MCHAKATO WA KUTEUA MGOMBEA URAIS.

Mpango wa CCM ulikuwa ni kumpata mgombea wake wa urais na hapo hapo wote watakaoshindwa wabaki ndani ya CCM ili kuleta ushindi.

Pasipo kutegemea kabisa, Edward Lowassa akiwa ndiye mgombea mwenye nguvu, ushawishi na watu wengi zaidi ndani ya CCM aliamua kuhamia CHADEMA na sasa ndiye mgombea urais wa CHADEMA.
Hili ni pigo zito sana kwa CCM kimahesabu.

2/ KUSAMBARATIKA KWA UKAWA.

CCM ilipanga na kujizatiti kabisa kuhakikisha UKAWA inavunjika kabla ya kampeni kuanza, mahesabu ya CCM yalionyesha kuwa ni rahisi sana kushinda kama wapinzani hawatakuwa pamoja. Bahati mbaya sana kwa CCM hilo halijatokea na UKAWA wako pamoja, tena imara zaidi. Hili ni pigo kubwa sana kwa CCM kimahesabu.

3/ MGOMBEA MWENZA MWANAMKE.

CCM kwa makusudi kabisa kiliteua mgombea Mwenza mwanamke(Samia Salum) kwa lengo la kutafuta kura za wanawake, ikitegemea kuwa ni rahisi sana kuingia kwenye kampeni kwa hoja ya kuwa CCM inawajali sana wanawake.

Bahati mbaya sana kwa CCM, tayari chama cha ACT kimemteua mwanamke(Anna Nghwira) kuwa mgombea wake wa urais ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama hicho, hivyo kuua kabisa agenda ya CCM ya kutaka kutumia uanamke kama kigezo cha kupata kura kwa wanawake wasiokuwa na upeo mkubwa.

Bahati mbaya kabisa kwa CCM ni kuwa mgombea wake mwenza(Samia Salum) sio mwanasiasa maarufu au mwenye ushawishi, hakubaliki kabisa kwa wazanzibar na anafahamika zaidi Tanzania bara kama mtu aliyetumika kuharibu maoni ya watanzania katika mapendekezo ya rasimu ya katiba, wakati wa bunge maalum la Katiba.
 
Mkuu tafadhali tufafanulie kwa undani zaidi - wewe hupo katika kamati hipi ya CCM inayo kufanya uamini kwamba mahesabu yanawapiga chenga? Hivi unaijua vizuri CCM au unaisikia kwenye radio tu, come October mtashangaa. Mnacho sahau ni kwamba Chama tawala akitegemei mbinu za kitoto za kutumia mapandikizi kwenye social networks wenye alias names lukuki kuzuga wasomaji,pili hawategemei magazeti ya kuchonga kufikisha ujumbe kwa wapiga kura walio wengi vijijini ambao hawana mihemuko ya kijinga jinga ya kisiasa, Chama tawala kipo level headed kinajua wapi pa kuwa corner wapinzani wake wa kweli na wale wanaopania 2 get even come rain or shine! Sooner or later they gonna regret their own FOLLY.

Narudia kuwakumbusha kwamba killer tactics za kampein ya CCM zipo kwenye grassroots za viongozi wao huko vijijini sio mijini,wanakwenda kwa wapiga kura walio wengi na wanahamasishwa kweli kweli, oh yes bado wanategemea a stone age mbinu kufikisha ujumbe wao huko vijijini mbinu hizo ni effective by 100%.

Bahati mbaya ccm imeshindwa katika uchaguz was serikali za mitaa so mlichotaraji hakipo mkatae mkubali mpo katika mazingira magumu ya kupata ushindi supporters wa kampain kama wahindi na vigogo wasiolipa kodi hawaelewi nan mshindi wanaogopa kutupa fedha zao ccm ya Leo inatawaliwa na ukata hazina wanaogopa kutoa hela sababu ya hofu ya kutojua mshindi pia magufuli hafungamani na vigogo was ccm ukitaka kumshinda kesi tajiri mfilisi kwanza
 
Mkuu tafadhali tufafanulie kwa undani zaidi - wewe hupo katika kamati hipi ya CCM inayo kufanya uamini kwamba mahesabu yanawapiga chenga? Hivi unaijua vizuri CCM au unaisikia kwenye radio tu, come October mtashangaa. Mnacho sahau ni kwamba Chama tawala akitegemei mbinu za kitoto za kutumia mapandikizi kwenye social networks wenye alias names lukuki kuzuga wasomaji,pili hawategemei magazeti ya kuchonga kufikisha ujumbe kwa wapiga kura walio wengi vijijini ambao hawana mihemuko ya kijinga jinga ya kisiasa, Chama tawala kipo level headed kinajua wapi pa kuwa corner wapinzani wake wa kweli na wale wanaopania 2 get even come rain or shine! Sooner or later they gonna regret their own FOLLY.

Narudia kuwakumbusha kwamba killer tactics za kampein ya CCM zipo kwenye grassroots za viongozi wao huko vijijini sio mijini,wanakwenda kwa wapiga kura walio wengi na wanahamasishwa kweli kweli, oh yes bado wanategemea a stone age mbinu kufikisha ujumbe wao huko vijijini mbinu hizo ni effective by 100%.

Unaiongelea ccm ipi hii iliyoparaganyika au ccm ipi? Kwa sasa ccm ina maadui ndani ya chama na nje ya chama acha kujipa matumaini
 
Uloi nga mâché68;13709971 said:
Shida ya JF ni kwamba wengi humu ni watoto. Hawajui historia ya Nchi hii zaidi ya kuota Ndoto ya kupewa maisha bora na UKAWA.

Ukiwauliza kwa nini CCM iondoke madarakani wanasema iondoke tu kama kula na wengine wale! UTOTO!
Nadhani hujajibu hoja bali umeonyesha dharau kwa wachangiaji wa humu JF.
Kama ungejua jukwaa hili la siasa lina watu wengi wenye upeo na ufahamu mkubwa sana wa kisiasa nina hakika usingesema hayo.
Kuhusu watanzania kuwa na matumaini ya maisha bora kupitia UKAWA, binafsi naona ni sawa kabisa kwa sababu wamekuwa na matumaini hayo kwa zaidi ya miaka 50 kupitia CCM lakini hawakuyapata, sasa wakiweka matumaini yao kwa UKAWA kwanini uwaone wamekosea?
Wewe ulitakaje?
 
Unaiongelea ccm ipi hii iliyoparaganyika au ccm ipi? Kwa sasa ccm ina maadui ndani ya chama na nje ya chama acha kujipa matumaini
Sijipi matumaini ukweli unabaki pale pale, wapinzani wataongeza idadi ya Wabunge lakini linapokuja suala la URAIS hilo wasahau kibisa - hamuwezi kudharau watu walio jenga CHADEMA mkafikia hatu ya kuwaondoa madarakani kiaina bila kujali demokrasia mnatumia ubabe tu kutekeleza malengo yenu, dhambi ya kumdhalalisha Dr.Silaa itawatafuna na actually kitendo hicho kinahashilia the begining of the end ya Chama cha upinzani chenye nguvu Nchini.
 
Mkuu tafadhali tufafanulie kwa undani zaidi - wewe hupo katika kamati hipi ya CCM inayo kufanya uamini kwamba mahesabu yanawapiga chenga? Hivi unaijua vizuri CCM au unaisikia kwenye radio tu, come October mtashangaa. Mnacho sahau ni kwamba Chama tawala akitegemei mbinu za kitoto za kutumia mapandikizi kwenye social networks wenye alias names lukuki kuzuga wasomaji,pili hawategemei magazeti ya kuchonga kufikisha ujumbe kwa wapiga kura walio wengi vijijini ambao hawana mihemuko ya kijinga jinga ya kisiasa, Chama tawala kipo level headed kinajua wapi pa kuwa corner wapinzani wake wa kweli na wale wanaopania 2 get even come rain or shine! Sooner or later they gonna regret their own FOLLY.

Narudia kuwakumbusha kwamba killer tactics za kampein ya CCM zipo kwenye grassroots za viongozi wao huko vijijini sio mijini,wanakwenda kwa wapiga kura walio wengi na wanahamasishwa kweli kweli, oh yes bado wanategemea a stone age mbinu kufikisha ujumbe wao huko vijijini mbinu hizo ni effective by 100%.

Bukyanagandi acha kutishia watu na kupotosha hapa JF. CCM sio chama makini kabisa kwa sasa, na pia uelewa wa watu wengi kisiasa umekuwa sana, wanaweza kutofautisha mambo mengi sana.
Mimi sipo kwenye kamati yoyote ya CCM ya siasa, mimi ni msomaji, mfuatiliaji na mchambuzi wa mambo ya kisiasa na kijamii.

Hata siku moja mipango(Hesabu) za CCM kupata ushindi hazifanyiki kwenye Grassroot bali ndani ya Secretariety, kamati kuu na halmashauri kuu. Huko mashinani kazi yao ni kupokea na kutekeleza tu maagizo kutoka juu.

Kila kitu kiko wazi sana, kama unasubiri kuambiwa mipango ya CCM na Kikwete ndio uamini, basi utakuwa umechelewa sana.
Juzi, Kikwete kasema yale Mafuriko ya watu ya UKAWA na Lowassa ni picha za kutengeneza kwenye kompyuta, vipi wewe unaamini hayo?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom