Jina la kitabu.ABRAMOVICH THE BILLIONAIRE FROM NOWHERE
Mwandishi.DominicMidgley and ChrisHutchins
Mchambuzi.Nanyaro EJ
CHAPTER THREE
HITTING THE JACKPOT
Mwandishi anasema kuwa moja ya sifa kubwa ya Abramovich ni uwezo wake wa kutambua mtu sahihi kwa wakati sahihi na kufanya nae urafiki.Jamaa alikuwa zaidi ya mwanasaikolojia,ukichanganya na upole wake na utaalamu wa kupangilia maneno kulimfanya aaminike zaidi
Unaambiwa jamaa anajua jinsi ya kupangilia maneno yenye hoja na mvuto wa hali ya juu!
Baada ya kuchukua biashara ya mafuta na kufanikiwa sasa ilikuwa muda wa kuzama zaidi ndani ya mfumo wa utawala wa Urusi.Katika jitihada hizi alikutana na kijana Aven aliyekuwa mtaalam,ambaye alimfanya Abramovich kutoka kuwa milinionea mfanyabiashara wa mafuta na kumfanya kuwa bilionea na gwiji wa biashara na viwanda,Mtu mwingine muhimu ni Olgarch Boris Berezovsky (huyu walikuja kusalitiana vibaya)
Unaambiwa Abramovich ni mtu wa mahesabu makali kila hatua anayopiga ni hatua ya uhakika,hana papara wala upesi...anaweka shabaha kwanza ndipo anaachia mshale au risasi!
Sasa Boris alimshawishi Abramovich waingie ubia,wakati huo Boris alikua na miaka 40± na Abramovich alikuwa na miaka 20±lakini Boris aliona umuhimu wa Abramovich akaona amfanye awe mshirika wake.Hali ya Uchumi iliendelea kuwa mbaya kufikia serikali kushindwa kulipa mishahara ya watumishi wake pamoja na pensheni! Boris ambaye alikuwa networker mzuri akatumia fursa vizuri,alikuwa tayari ni Olgarch mwenye biashara ya kuuza magari,akatumia washauri wa Rais Yelsin akawapa mchongo.....mchongo wenyewe ilikuwa wamshauri Rais akubali kukopa kwa kuweka dhamana ya hisa ya mashirika ya umma! Kwa hiyo serikali idhaminishe mashirika yake kisha zile hisa zake ndio ziwe dhamana kwa mtu au kampuni itakayokubali kutoa mkopo wa fedha ili serikali ipate ela ya kuwalipa watumishi,wazo hili lilikubaliwa na serikali na mashirila ya umma yakawa yanawekwa dhamana ambako yeye Boris na Abramovich ndio walitoa fedha kupitia makampuni yao tofauto tofauti waliyounda! Kwa mfumo huu walijikuta wananunua kampuni na mashirika ya umma kwa bei sawa na bure......mfano kampuno ya mafuta ya Sibneft ilinunuliwa kwa njia ya kukopesha serikali jumla ya dola milion 300 mwaka 1997 na mwaka 2003 dhamani yake ilikuwa dola bilioni 75
Yaani ni kama wale jamaa wanaokopesha fedha za riba kubwa alafu unaweka gari pamoja na kadi yake Orijino...kisha unasaini mkataba kuwa ikifika ile tarehe kama hujalipa badi mkopeshaji anakuwa na haki zote na
Anguko la ujamaa lilitajirisha wachache huku.likiwaacha warusi 150mil wakiwa katika umaskini na mali zao kuuzwa kwa bei ya kutupwa mithili ya yale yalifanyika Tanzania wakati wa serikali ya awamu ya tatu
Jina la kitabu.ABRAMOVICH THE BILLIONAIRE FROM NOWHERE
Mwandishi.DominicMidgley and ChrisHutchins
Mchambuzi.Nanyaro EJ
CHAPTER FOUR
AN ORPHAN JOINS 'THE FAMILY'
Yelstin aliongoza Urusi kuanzia 1991-1999 katika kipindi chote hiki sio bunge,wala baraza la mawaziri wala vyombo vya ulinzi na usalama vilivokuwa na nguvu...kulikuwa na watu wachache miongoni mwa Olgarch walioitwa
the family hawa ndio walikuwa wanaongoza nchi,miongoni mwao ni yule Bwana Boris mshirika wa Abramovich.Hawa ndio walipanga na kuratibu kampeni za mwaka 1996 za kumrejesha mtu wao Yelstin madarakani kwa gharama yoyote!
Rais Yelsin alikuwa na binti yake aliyeitwa Tanya ambaye alikuwa anaongoza moja ya idara nyeti pale ikulu,huyu ndio alikuwa roho ya Rais na mtu anayeaminika zaidi,ili ufanikishe mambo ilikuwa lazima kupitia kwa Tanya!huyu binti alikuwa mshauri wa Rais(baba yake)na Rais Yelsin hakuwa na hofu hasa baada ya kujulishwa kuwa hata huko Ufaransa Rais Chirac amemteua binti yake Claude kuwa mshauri wake! Olgarch Boris alipanga mpango wa kuwakutanisha hawa mabinti yaani Tanya na Claude ili Tanya ajifunze mambo ya magharibi aachane na ushamba kutoka kwenye ujamaa!Ziara ya Paris ilizaa matunda,na aliporejea Tanya alikuwa mtu wa kisasa aliyebadilisha mwonekano wa Rais na ikulu kwa ujumla!
Kwa msaada wa the family na Olgarch wengine Yelsin alishinda awamu ya pili kwa zaidi ya asilimia 50%!ni hawa Olgarch ndio walitumia kila aina ya mbinu na kutoa mchango wa fedha pamoja na kupanga watu wao kwenye kila nafasi
The family waliingia ikulu,na kufanya babeque na vinywaji kila siku,walitumbua raha..kwenye hivi vikao vya mara kwa mara Abramovich alijikuta karibu sana na Tanya na familia nzima ya Rais Yelsin,miongoni mwa the family yeye Abramovich ndie aliaminika zaidi,akawa mtu wa karibu na mshauri wa karibu na anayeaminika na Rais! Abramovich aliendelea kujisimika zaidi kibiashara na kisiasa!
Ilifika pahali the family ikawa ndio Abramovich na Abramovich ndio the family!
Jina la kitabu.ABRAMOVICH THE BILLIONAIRE FROM NOWHERE
Mwandishi.DominicMidgley and ChrisHutchins
Mchambuzi.Nanyaro EJ
CHAPTERSIX
PLAYINGPOLITICS
Mwandishi anasema kuwa mwaka 1999 Putin aliteuliwa na Rais Yelisn kuwa wazir mkuu wa Urusi kwa msaada wa Abramovich,na ndie pia aliyesimamia uundwaji wa Serikal mpya chini ya waziri mkuu Putin.Mara kadhaa amejitahidi kukataa kuwa anahusika na siasa ila ushahidi wa uwepo wake Kremli upo wazi sana!wakati huu alitumia muda mwingi Kremli na aliingia bila appointment!
Wakati huo Urusi iliomba kampuni fulani ya political Consultants ya USA iwasaidie kujua nani alifaa kuwa mbadala wa Rais Yelsin,baada ya utafiti walishauriwa wateue mtu mwenye nguvu(Warusi wanapenda sifa sana) miongoni mwa majina pendekezwa Putin hakuwepo,walikuwa watu kama Yuri Lukhoz meya wa Moscow na wengine wengi.Jinsi ambavo Abramovich alichanga karata zake kwa weledi mkubwa hado kumfanya Putin kuwa si tu Rais bali miongoni wa Marais wenye maguvu duniani imebaki kuwa siro yake tu!
Huyu meya Yuri alikuwa na nguvu na mwaminifu kwa Rais Yelsin lakini alikuwa mwiba kwa watu wa karibu na Yelsin akiwepo Abramovich na Boris,hivo ilibidi waingie kazini kupambana kwa nguvu zote hadi kufanikiwa kumweka Putin ili wawe salama wao binafsi na biashara zao.
Baada ya Ushindi wa Putin mambo yalibadilika kwa Oligarch wengi,siku moja Putin akiwa Rais aliwaita wote,walikuwa zaidi ya Olgarch 30,Rais Putin akawaambia kuwa anawashukuru sana kwa msaada wao, lakimi wajue kuwa sasa yeye ni Rais,kama mtu angetaka kuendelea kufaidi afanye mambo kadhaa
Mosi.Asitumie rushwa na maofisa mawaziri wasiokuwa waaminifu kujipatia mali ya umma
Pili.Asiingilie serikali,wala kuikosoa bila staha
Tatu.Alipe kodi stahiki
Kushindwa kufanya hivo mali zitataifishwa na wao kuozea jela kwa kesi ambazo hazina dhamana.Olrgarch waligawanyika baada ya kikao,wengi waliona wamesalitiwa,wengine waliona waanzishe uasi,almradi kila kundi lilikuwa na mtazamo wake,Abramovich yeye aliamua kufuata maelekezo mapya ya utawala mpya
Baada ya kikao ilitokea kitu cha ajabu Meli kubwa ya kivita ambayo ilikuwa fahari ya Warusi,ikiwa na wanamaji zaidi ya mia moja,ilizama baharini,wakati inazama Rais Putin alikuwa likizo,waziri wake wa mambo ya ulinzi alimpigia simu na kumjulisha kuwa chombo kimepoteza mawasiliano ila wanahangaika kutafuta tena,na akamwambia Putin kuwa sio ishu kubwa hivo yeye Rais aendelee na likizo(Alimficha na haijulikani kwa nini),baada ya siku mbili Rais Clinton alimpigia Rais Putin na kumpa pole na kumtaka wakubali kupata msaada wa kijeshi.Wakati huo.wanamaji wote zaidi ya mia walishazama maji na chombo,ilibidi Putin akatishe likizo na baada ya wiki moja alienda kuonana na ndugu wa wafiwa,ambao walikuwa na hasira Kali kutokana na ukimya wa serikali,Putin aliwaambia watalipwa mshahara kwa miaka kumi kwa kila aliyepoteza mpendwa wake,kwa Mara ya kwanza Rais was Urusi alivumilia maneno mabaya kutoka kwa waombelezaji kwa zaidi ya SAA sita.Kuzama kwa meli kuligeuka skendo kwa Serikali mpya ya Putin,Dunia mzima ililaani jinsi ambavo serikali.ilichelewa Kuchukua hatua,vyombo vya Urusi vilivomilikiwa na Olgarch Boris pia viliandika kuikosoa Serikali,Putin hakuwa na uwezo wa.kuhimili kukosolewa akiwa na Hasira Kali alimpigia Oligarch Boris simu na kumtaka aende ikulu,alipofika tu Oligarch alikutana na katibu mkuu viongozi ambaye alimpa maelekezo ya Rais,kuwa Rais anavitaka vyombo vyako vya habari viwe vyake,unapewa wiki moja tu...Boris alihakikisha anaonana na Rais na kwa mstuko mkubwa Rais Putin alimwambia kuwa anavitaka vyombo kwa namba yoyote ile,Boris hakuwa ma ujanja zaidi ya kuviuza kwa bei ya hasara kwa mshirika wake Abramovich kisha yeye Boris akakimbilia London ambako alipata haki ya mkimbizi wa kisiasa.Huku nyuma alifunguliwa mashtaka ya kila sina....na huko London alifuatiliwa na KGB(FSB) auwawe...hivi ndivo Putin alijikuta anakuwa.mtu mwenye nguvu zaidi Urusi...na hivi ndivo Mwanafunzi alivomzidi mwalimu wake.Leo Abramovich ni mtu wa pili mwenye nguvu zaidi Urusi baada ya Putin