Man Mvua
JF-Expert Member
- Apr 12, 2016
- 2,179
- 3,525
Unazungumzia Nchi gani ? Kama ni TZ sahau kabisa sio kwa hawa watz labla wakenya, kama ilishindikana 1995 na 2015 na bado Watz walikuwa kimya basi hata 2025 hakuta kuwa na jipya.Bila shaka kila Mtanzania wa leo anaguswa na machungu mbalimbali yanayotokana na ULEGEVU wa Viongozi wetu waliopo sasa.
Mbaya zaidi, Wabunge waliotakiwa kutusemea na kututetea sisi Wapigaji kura wao, wametugeuka na wameungana na watawala.
Kwa hiyo sasa, Wabunge badala ya kututetea sisi Wapigaji kura wao, wanaitetea Serikali zaidi.
Kwa udhaifu huo, Serikali inafanya inachoweza kwa sababu hakuna wa kuikemea.
Hatma ya haya yote ni Uchaguzi wa mwaka 2025.
Hapo Tanzania utaandika Historia mpya kabisa.
Hatuwezi kuendelea na hali hii.
Kila Mbunge atakayegombea tena 2025, lazima kwanza aeleze amefanya nini katika kipindi cha miaka mitano iliyopita?
TOZO zimejaa kila kona, je, yeye kama Mbunge alifanya jitihada gani kuzuia uhalifu huo?
Ni kuomba Mungu katiba ibadilishwe basi kwa sasa hivi.