Uchaguzi mkuu kanuni wapi au mambo valu valu tu?

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,825
35,827
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Uchaguzi ndiyo hivyo unajongea kampeni nazo zinaendelea. Kila mtu na kila chama na lake.

Wakati wa teuzi palikuwa na fomu yenye kanuni za maadili ya uchaguzi. Nini contents za fomu hii?

Ilikuwa vyema kilichomo kikafahamika kwetu wapiga kura pia. Ili tuweze kuwapima wagombea na hata kuitathimini tume.

Pana mambo mengi ambayo kweli - ni mambo valu valu ya Dr. Remmy (rip).

Pana wagombea wanaongea kutumia lugha za makabila ya kwao. Pana nyimbo zinaimbwa kutumia lugha za makabila ya wagombea kama zilizo rasmi katika kampeni hizi.

Pana upendeleo wa wazi katika matumizi ya radio na tvs zote za binafsi na taifa. Pana kupendelea baadhi ya vyama kutokana na shinikizo la wagombea na vyama fulani fulani.

Pana matamko ya utekelezwaji yanayotolewa kiserikali katika kampeni. Ni ziara za ufuatiliaji za serikali au ni rushwa badala ya kampeni? Ni vipi ufumbuzi wa kiserikali unaweza kutolewa na mgombea yeyote kwenye jukwaa la kampeni?

Pana hata vitisho vya waziwazi kwa wapiga kura vinavyotolewa katika majukwaa ya kampeni. Tume wapo kimya tu.

Hatua zipi tume inaweza kuchukua ili tujiridhishe kuwa haki inatendeka na kuwa hata tutegemee pia kuwa haki itaendelea kutendeka hadi mwisho?

Tume mna wajibu mkubwa katika kulinda haki ili amani iendelee kuwapo.

Taratibu kwa kufumbia macho maovu mengi ya wazi, hii nchi mnaipeleka kusiko.
 
Magufuli ndio mvunja sheria za uchaguzi namba moja hapa nchini, na hiyo tume ya uchaguzi haina la kumfanya. Magufuli anaongea kisukuma jukwaani na hakuna yoyote anamkataza au kumchukulia hatua. Katika mazingira haya tume itaweza kutangaza matokeo tofauti na matakwa yake? Bado katiba yetu inapaswa kuacha matokeo ya rais kutohojiwa mahakamani, na rais kutoshitakiwa kwa makosa atakayofanya akiwa madarakani?
 
Magufuli ndio mvunja sheria za uchaguzi namba moja hapa nchini, na hiyo tume ya uchaguzi haina la kumfanya. Magufuli anaongea kisukuma jukwaani na hakuna yoyote anamkataza au kumchukulia hatua. Katika mazingira haya tume itaweza kutangaza matokeo tofauti na matakwa yake? Bado katiba yetu inapaswa kuacha matokeo ya rais kutohojiwa mahakamani, na rais kutoshitakiwa kwa makosa atakayofanya akiwa madarakani?

Muhimu tupate contents ya kanuni za uchaguzi sisi kama wapiga kura.

Safari hii tutaelewana tu.
 
Mabibi na mabwana heshima kwenu.

Uchaguzi ndiyo hivyo unajongea kampeni nazo zinaendelea. Kila mtu na kila chama na lake.

Wakati wa teuzi palikuwa na fomu yenye kanuni za maadili ya uchaguzi. Nini contents za fomu hii?

Ilikuwa vyema kilichomo kikafahamika kwetu wapiga kura pia. Ili liweze kuwapima wagombea na hata kuitathimini tume pia.

Pana mambo mengi ambayo kweli sasa ni mambo valu valu.

Pana wagombea wanaongea kutumia lugha za makabiliano ya kwao. Pana nyimbo zinaimbwa kutumia lugha za makabila ya wagombea kikabila kama zilizo rasmi katika kampeni hizi.

Pana upendeleo wa wazi katika matumizi ya radio na tvs zote za binafsi na taifa. Pana kupendelea baadhi ya vyama kutokana na shinikizo la wagombea na vyama fulani fulani.

Pana matamko ya utekelezwaji yanayotolewa kiserikali katika kampeni. Ni ziara za ufuatiliaji za serikali au ni rushwa badala ya kampeni? Ni vipi ufumbuzi wa kiserikali unaweza kutolewa na mgombea yeyote kwenye jukwaa la kampeni?

Hatua zipi tume inaweza kuchukua ili tujiridhishe kuwa haki inatendeka na kuwa hata tutegemee pia kuwa haki itaendelea kutendeka hadi mwisho?

Tume mna wajibu mkubwa katika kulinda haki ili amani iendelee kuwapo.

Taratibu kwa kufumbia macho makavu mengi ya wazi, hii nchi mnaipeleka siko.

Tume iamue inataka uchaguzi ufanyie au usifanyike, sisi tumejiridhisha katika majimbo yetu yote 62 ya ubunge, wagombea wetu wamejaza fomu sawasawa na hakuna mgombea ambaye amekose chochote".Zitto Kabwe.
 
Tume iamue inataka uchaguzi ufanyie au usifanyike, sisi tumejiridhisha katika majimbo yetu yote 62 ya ubunge, wagombea wetu wamejaza fomu sawasawa na hakuna mgombea ambaye amekose chochote".Zitto Kabwe.

Hii ni dalili mbaya sana. Hasa kama wataendelea kumfumbia macho huyu anayejitanabaisha kwa ukabila wake kuwa eti nao ni dili.

"Kwani ana mpango wa kufanya matambiko huko?" In Nyerere's words. Maana umuhimu wa ukabila ni kwenye matambiko tu.
 
Mkuu, ukisikia mtu anaitwa "Bulldozer" basi huyo ni kama mitambo ya ujenzi wa barabara. Mtambo wa aina hii unafaa sana wakati wa ujenzi wa barabara, lkn barabara ikisha kamlilika, mtambo huu hautakiwi tena kutembea wenyewe barabarani, bali hubebwa na malori makubwa na tena tahadhari hutolewa iwapo unasafirishwa.

Nafikiri tunaona mtambo umeaminiwa kutembea wenyewe barabani. Unapondaponda kila kilichopo mbele yake. Si injinia wala dereva ambaye anaweza kuhoji kuhusu uharibifu ambao mtambo unaufanya.
 
Mkuu, ukisikia mtu anaitwa "Bulldozer" basi huyo ni kama mitambo ya ujenzi wa barabara. Mtambo wa aina hii unafaa sana wakati wa ujenzi wa barabara, lkn barabara ikisha kamlilika, mtambo huu hautakiwi tena kutembea wenyewe barabarani, bali hubebwa na malori makubwa na tena tahadhari hutolewa iwapo unasafirishwa.

Nafikiri tunaona mtambo umeaminiwa kutembea wenyewe barabani. Unapondaponda kila kilichopo mbele yake. Si injinia wala dereva ambaye anaweza kuhoji kuhusu uharibifu ambao mtambo unaufanya.

Ni shida. Huu ndiyo wenziwe walimwita sawa - ni mshamba!
 
Back
Top Bottom